Mahakama ya Wilaya ya Kinondoni imempandisha kizimbani Mkazi wa Mabwepande Jijini Dar es salaam, Shembiu Shekilaghe (38) akikabiliwa na mashtaka ya kutoa taarifa za uongo na kujifanya yeye ni Rais Mstaafu Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete huku akijua sio kweli.
Wakili wa Serikali, Salma Jafari amesema hayo jana September 23, 2024 alipokuwa akimsomea Mshtakiwa mashtaka yake mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Hawa Magesa ambapo amedai Mshtakiwa huyo anakabiliwa na mashtaka 14 huku mashitaka ya kwanza ya pili na tatu yakiwa ni kutoa taarifa za uongo.
Amedai September 02,2024 Mshtakiwa akiwa katika eneo lisilojulikana ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania alitoa taarifa za uongo kupitia Akaunti ya mtandao wa kijamii ya Facebook yenye jila la Mrisho Jakaya Kikwete akisema “Ukiweka akiba ya 49,000 utapata mkopo wa laki tatu marejesho ni Tsh. 30,000 kila mwezi kwa muda wa miezi 10”
Amedaiwa katika tarehe hiyohiyo kupitia akaunti hiyo pia alitoa taarifa ikisema “Ukiweka akiba ya 59,000 utapata mkopo wa Tsh. 400, 000 marejesho ni Tsh. 40,000 kila mwezi kwa muda wa miezi 10, ukiweka akiba ya Tsh. 69,000 utapata mkopo wa laki tano marejesho ni Tsh. 50,000 kila mwezi kwa miezi 10”
Your browser is not able to display this video.
Mashtaka mengine ni ya kutumia laini ya simu iliyosajiliwa kwa jina la Mtu mwingine ambapo inadaiwa kuwa September 3,2024 katika eneo la Mji mpya Mabwepande alikutwa akitumia namba ya simu iliyosajiliwa kwa majina ya Matias Ngowi, Modesta Marumi, Jane Mhanga, James Zephania na Amini Omary na kujipatia fedha kiasi cha Tsh. 100,000 kutoka kwa Samson Mwandawila kwa kudai atampatia mkopo wa Tsh. 800,000 huku akijua si kweli na kujipatia fedha Tsh. 100,000 kutoka kwa Rudi Maduka akidai atampatia mkopo wa Tsh. 1000,000 kupitia taasisi yake ya Jakaya Kikwete foundation.
Baada ya kusomewa mashtaka yake mshtakiwa amekana kutenda kosa hilo na Wakili Jafari amedai kuwa upelelezi wa kesi hiyo umekamilika hivyo ameiomba Mahakama ipange tarehe nyingine kwa ajili ya kusomaa hoja za awali, Hakimu Magesa ameahirisha kesi hiyo hadi October 10, mwaka huu kwa ajili ya kusomwa hoja za awali na Mshtakiwa amerudishwa rumande baada ya kukosa Wadhamini.
Maana mimi sielewi au,ina maana kwa sababu anatumia jina la jakaya ndy wakiambiwa tuma hizo 40000 na 50000 wanatuma
Kwqnza hao watu walitakiwa wapigwe bakora
Maana mimi sielewi au,ina maana kwa sababu anatumia jina la jakaya ndy wakiambiwa tuma hizo 40000 na 50000 wanatuma
Kwqnza hao watu walitakiwa wapigwe bakora
Mkazi wa Mabwepande, Shembiu Shekilaghe (38) amefikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Kinondoni, Dar es Salaam kujibu mashtaka 14 yakiwamo ya kujitambulisha kuwa ni Jakaya Mrisho Kikwete, wakati akijua ni uongo na kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu.
Mshtakiwa huyo amefikishwa mahakamani hapo leo Jumanne, Septemba 24, 2024 na kusomewa mashtaka yake na wakili wa Serikali Salma Jafari, mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Hawa Magesa.
Akisoma mashtaka yake, Jafar amedai kati ya mashtaka 14 yanayomkabili Shekilaghe, mashtaka matano ni ya kutumia laini iliyosajiliwa kwa jina la mtu mwingine, mashtaka matatu ni ya kutoa taarifa za uongo kinyume cha sheria, shtaka moja kujiwasilisha yeye ni Jakaya Mrisho Kikwete (Rais mstaafu wa Tanzania) na yaliyosalia ni kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu.
Jafar amedai Septemba 2, 2024 mshtakiwa akiwa katika eneo lisilojulikana ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania alitoa taarifa za uongo kupitia akaunti ya mtandao wa kijamii wa Facebook yenye jina la Mrisho Jakaya Kikwete aliandika ujumbe unaosomeka, “Ukiweka akiba ya Sh49,000 utapata mkopo wa laki tatu marejesho ni Sh30,000 kila mwezi kwa muda wa miezi 10.”
Wakati Wasambaa wenzake wanapambana kuongeza mbinu za kuingia kwa siri kwenye store za watu kuiba viroba na madumu yeye Mgosi kaona ajiongeze kwa kutumia title za watu,sasa kweli ukachezeshe upatu kwa jina la raisi mstaafu utegemee kutoboa?