Mke hawezi kushindana na ubabe wa mwanaume!

Mtambuzi kwa mwanamke aliyechezwa unyango atakuelewa unachomanisha ni kweli mke anatakiwa awe chini ya mmewe kwa unyenyekevu na si kwa woga, na endapo itatokea kaudhiwa na mmewe basi hutumia busara bila jazba kumweleza, ikiwa mwanaume huyo ni muungwana hukiri kosa lake na maisha yakasonga.
 
Last edited by a moderator:
Mtambuzi vipi mwanamke mpole na mwenye heshima na mwanaume akachukua hali hiyo kumkandamiza mwanamke?
Mimi napenda kila mtu achukue nafasi yake kwenye ndoa. Haipendezi hata kidogo kuwa na mwanamke aliye juu ya mumewe au anayejilinganisha na mumewe, si ukondoo sometimes inatia hata hamasa mwanaume akionesha "uanaume" wake.
 
lemonade
Sasa hapo unamchochea huyu Babu yangu Mtabuzi azidishe kile kimfumo dume chake kwa Bibi yaani anakibesi chenye vituko sana.
 
Last edited by a moderator:
Nimekusoma mzee na nakubaliana na wewe, kuna wengine wanakuwa successful kwenye hii area mpaka unashangaa hiki kidume mbele ya mke topetope. Na kuna wengine wanatumia upole wa mke kumwangamiza zaidi hapo unasemaje?
MadameX ..................Nakubaliana na wewe kwenye Bold, na ndio maana wanawake wanatakiwa kuwasoma wapenzi wao kabla ya ndoa.......... Lakini kama mtaharakisha for the sake of kuvalishwa pete ya ndoa, itakula kwako. Wanaume tunatofautiana sana, kuna wale ambao wakishitakiwa na dhamira hurudi chini na kuyamaliza na wake zao kwa njia ya mazungumzo lakini wengine ni ubabe ubabe tu........ Mwanaume wa aina hii, kama ameoa mwanamke asiye na busara, ndoa hiyo haitodumu...........
 
Last edited by a moderator:
Mabuzuki .................Kumbe wewe umeelewa eh!.......... Kuna watu humu wamesoma wakiwa na mning'inio wa Jumatatu........... hawjaelewa nimezungumzia nini, wamekurupuka kutoa maoni wakidai eti nimesema wanawake wawe makondoo......... Jamani hebu nitakeni radhi.................
 
Last edited by a moderator:
hiyo ilikuwa zamani siku hizi ukimwaga ugali mkeo anamwaga mboga
Na ndio hapo unakutana na mwanamke anakwambia "Nimeolewa vyuo saba mie" yaani kaolewa na kuachwa mara saba..............!
Ninachosema hapa ni kwamba mwanamke akijidai kutaka kushindana na mwanaume kamwe asitarajie kushinda........ Labda kama atatumia kile wenyewe mnachoita LIMBWATA....................LOL
 
mtambuzi,nimekusoma bt ili niwe normal must aombe msamaha hata kama anazuga bila hivyo ni KUNUNA TU mpaka kieleweke.
JOJEETA ....... Mwanaume mbishi na mbabe haombi msamaha haraka , hata kama kosa liko wazi (Kama mimi Mtambuzi nitakupigia hata magoti...LOL). Mara nyingi mpaka akajiulize saAana ndipo atakuja kukuomba msamaha na sio kwa kusema samahani......La hasha.......atajichekesha chekesha, na vizawadi kidogo, na kwa mtu mzima atajua tu kwamba huyu jamaa kajirudi amejua makosa yake, lakini kama atafanya hivyo na bado mwanamke akaonyesha kibri........ atashangaa vituko vyake........... Jamani msitegemee kushinda mbele ya mwanaume mbabe..................
 
Last edited by a moderator:

Yeah hapo kwenye Bold uko sahihi, mwanaume mwoga kiasi cha kukimbia hata kumtoa buibui kitandani huyo hafai.......
na ndio hapo tunaposema mume ni kichwa cha nyumba, sio kumnyanyasa mwanamke mpole na anaye mtii, la hasha nazungumzia mwanaume anayeongoza nyumba kwa busara na hekima......... Lakini pale anapoonyesha uanaume wake kimamlaka na mke akataka kushindana naye......... kamwe hatashinda.........I bet!
 
lemonade
Sasa hapo unamchochea huyu Babu yangu Mtabuzi azidishe kile kimfumo dume chake kwa Bibi yaani anakibesi chenye vituko sana.
TaiJike ..........Yeah......... Uko sahihi, kuna wakati inanilazimu kuwa dikteta katika maamuzi yangu, na kama binadamu nina maudhaifu yangu ....... nilishawahi kusema hapa kwamba mimi sio mkamilifu, bali niko tayari kujifunza kila siku. Mama Ngina ananijua na ameshayajua mauadhaifu yangu, anachofanya ni kuyakemea kwa jina la yesu au kukubaliana nayo kwa sababau hayamzuii kula na kulala usingizi wake mnono..............LOL
 
Last edited by a moderator:

no wonder hiler's and mussolin's blood keeps flowing in your veins! (DICTATORSHIP) Pathetic kwa kweli, nawaonea huruma bby galz wangu kupata waume wa designs za hivi, cjui kama watakuja kuwa na moyo kama wangu! LORD HAVE MERCY!
 

katika makabila ambayo huwa siku zote naomba MUUMBA WANGU JUU awaepushie wanangu kuolewa nao ni hili, TUFIAKWA(najitemea mate kifuani) watoto wangu kamwe wasiolewe huku!
 

Ninavyoamini mimi, kwenye argument sometimes you have to accept to loose. Hii mind ya kutaka kudominate haileti matunda mazuri kwenye ndoa. Nani aliyekwambia kama mwanamke siku zote anataka awe on the loosing part, mwanaume mwenye akili sometimes pia anatakiwa kunyamaza and not to try to win in every battle!

Jengine ni kuwa nature ya mwanamke ni talk and talk hata kwenye malumbano anatumia kama silaha yake, mwanaume ambaye ana kacommon sense ya kumsoma mke wake hatapoteza nguvu zake kushinda nae kwenye hili, he will only try convince when she calm

I am still believing its two thing!
 

Teh teh huko kwenu ishini wenyewe tu...
 
vip kama mwanamume anamkosea mkewe na mke anamweleza kwamba hajapendezwa na alivyofanya halafu mume anapuuzia kesho na keshokutwa anarudia kosa lilelile, mke afanyaje? WANAUME JIELEZENI
 
mtambuzi,yap ni kweli wapo wabishi.wa hivyo naona ningemnunia hata week,yaani mapaka kieleweke LOL!
 
katika makabila ambayo huwa siku zote naomba MUUMBA WANGU JUU awaepushie wanangu kuolewa nao ni hili, TUFIAKWA(najitemea mate kifuani) watoto wangu kamwe wasiolewe huku!

Pole we maana mpaka sasa tayari mwanao ni mkazamwana wangu na mimba tayari.
 
Leo mtambuzi kaja na thread babkubwa, unaona kitu muhimu ni quality sio quantity.

Thread inaongelea ukweli mtupu...Big Up.
 
mbona mi sio mbabe....ndo mana labda mademu hua wananioneaga...itabidi nichange sasa nianze kua mbabe mbabe:spider:
 
As if mwanamke ameumbwa kwa kutumia program tofauti na mwanaume! Kitendo cha kukasirika na aina ya reaction itokanayo na hacra ni sawa kwa binadamu wote tofauti ni kuwa wapo wanaowezakujicontrol na reactions hizo sasa kama mwanaume amekasirika na reaction yake ikawa ni matusi, nn kitamzuia mwanamke asireact the same?

Mi nadhani ubabe unapaswa kutafsiriwa kama kutojiamini, insecure, na hasa kama unatokana na kutokukubaliana na ushindani
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…