warumi
R I P
- May 6, 2013
- 16,218
- 18,440
Wakati Diva wa Filamu Bongo , Kajala Masanja ' Kay ' akielezwa kuwa mambo yake hivi sasa yako kwenye mstari kwa kusajili Kampuni yake ya mambo ya Sinema , mwanamke aliyejitambulisha kwa jina moja la Pamela ameibuka na kumtaka muigizaji huyo kuacha kumfuata mume wake , Amani lina data kamili .
Mwanamama huyo , anayefanya kazi ' nzuri ' katika Shirika moja kubwa Nchini , aliliambia gazeti hili kuwa Kajala , amekuwa akitembea na mumewe aliyemtaja kwa jina moja la Tanaluza ambaye kwa sasa yuko ndani katika gereza la Keko kwa kosa ambalo alikataa kulitaja. "Jamani namtahadharisha Kajala , asije kunikuta pale, patakuwa hapatoshi , yeye si hodari wa kwenda kuangalia waume za watu , awe na haya , aende Ukonga akamuangalie mumewe , ushauri wa bure nampa , " alisema Pamela kwa jazba .
Alisema anazo taarifa kuwa Kajala alikuwa akitembea na mumewe kabla hajapatwa na matatizo na baada ya kupelekwa Keko Gerezani , amekuwa akienda hapo kwa kujifichaficha, kitu ambacho alisema siyo kizuri kwa sasa, kwani anaweza kumsababishia mumewe matatizo zaidi .
"Huyo ni mume wangu , ananihitaji kwa hali na mali sasa hivi , nisije nikaacha kwenda kwa ajili ya Kajala , kama aliwahi kumpangishia Nyumba ya kifahari na kumnunulia Gari, ni huko huko , sasa hivi anahitaji kuwa na mimi mkewe , kwanini yeye asiende kwa mume wake na yeye si amefungwa ?, " alihoji Pamela .
Baada ya maelezo hayo kutoka kwa mke , Gazeti hili liliingia mtaani kwa nguvu kumsaka Kay , ambaye mume wake , Faraja Augustino amefungwa Jela miaka saba kwa kosa la utakatishaji fedha na kufanikiwa kumpata kupitia simu yake ya mkononi. "
Mimi mbona simjui huyo mwanaume, wala sijawahi kufika huko Keko , kama anatafuta umaarufu kupitia jina langu aseme , asinisingizie , " alisema Kajala baada ya kusomewa mashtaka yake , majibu ambayo licha ya kuyaheshimu , lakini gazeti hili linaendelea na uchunguzi wake ili kubaini ukweli zaidi .
Mwanamama huyo , anayefanya kazi ' nzuri ' katika Shirika moja kubwa Nchini , aliliambia gazeti hili kuwa Kajala , amekuwa akitembea na mumewe aliyemtaja kwa jina moja la Tanaluza ambaye kwa sasa yuko ndani katika gereza la Keko kwa kosa ambalo alikataa kulitaja. "Jamani namtahadharisha Kajala , asije kunikuta pale, patakuwa hapatoshi , yeye si hodari wa kwenda kuangalia waume za watu , awe na haya , aende Ukonga akamuangalie mumewe , ushauri wa bure nampa , " alisema Pamela kwa jazba .
Alisema anazo taarifa kuwa Kajala alikuwa akitembea na mumewe kabla hajapatwa na matatizo na baada ya kupelekwa Keko Gerezani , amekuwa akienda hapo kwa kujifichaficha, kitu ambacho alisema siyo kizuri kwa sasa, kwani anaweza kumsababishia mumewe matatizo zaidi .
"Huyo ni mume wangu , ananihitaji kwa hali na mali sasa hivi , nisije nikaacha kwenda kwa ajili ya Kajala , kama aliwahi kumpangishia Nyumba ya kifahari na kumnunulia Gari, ni huko huko , sasa hivi anahitaji kuwa na mimi mkewe , kwanini yeye asiende kwa mume wake na yeye si amefungwa ?, " alihoji Pamela .
Baada ya maelezo hayo kutoka kwa mke , Gazeti hili liliingia mtaani kwa nguvu kumsaka Kay , ambaye mume wake , Faraja Augustino amefungwa Jela miaka saba kwa kosa la utakatishaji fedha na kufanikiwa kumpata kupitia simu yake ya mkononi. "
Mimi mbona simjui huyo mwanaume, wala sijawahi kufika huko Keko , kama anatafuta umaarufu kupitia jina langu aseme , asinisingizie , " alisema Kajala baada ya kusomewa mashtaka yake , majibu ambayo licha ya kuyaheshimu , lakini gazeti hili linaendelea na uchunguzi wake ili kubaini ukweli zaidi .