Mkwai
JF-Expert Member
- Feb 29, 2012
- 306
- 96
Wajameni tubadilike. maisha ya sasa siyo ya miaka ya 40 yale waliokuwa wanaishi mababu zetu vijijini. Maisha ya sasa katika nyumba ni mume mke na watoto basi; kuonana au kukutana na ndugu iwe kwa sababu maalum kwa kutembeleana kwa muda mfupi tu; Sio watu kuhamia bila sababu. Migogro mingi ya nyumba zetu inaletwa na ndugu. Mlioana wawili mle raha maisha, leo mnajipa kiwingu kwa kuleta ndugu ndani ya nyumba. Kama ni misaada wasaidiwe wakiwa hukohuko. Ikitokea ni ishu za maradhi hapo sawa, aje atibiwe akipata nafuu safari akaendelee kutumia dawa akiwa kwake. Mtawapa ubaya wake zenu bure wajameni. Watu wanaoongoza kuharibu nyumba ni kina mama wa mabwana maana wanaamini hakuna mke aliewahi kuwa bora kuliko wao. pili mawifi. So if unataka kuishi maisha mazuri na mkeo rekebisha utaratibu kuhusu ndugu. Another thing, no matter what you will do, bado utapata lawama tu