Mke wa Frank Mbise, kijana aliyetekwa pamoja na Soka wa CHADEMA aongea kwa uchungu baada ya mumewe kutekwa. Amtaja Rais Samia!

Mke wa Frank Mbise, kijana aliyetekwa pamoja na Soka wa CHADEMA aongea kwa uchungu baada ya mumewe kutekwa. Amtaja Rais Samia!

Mindyou

JF-Expert Member
Joined
Sep 2, 2024
Posts
1,869
Reaction score
4,877
Mke wa Frank Mbise, kijana aliyetekwa zaidi ya siku 40, amemuangukia Rais Samia Suluhu Hassan, akiomba msaada wa kumrudisha mume wake nyumbani.

Akizungumza kwa uchungu, mwanamke huyo alisema kuwa amebaki katika hali ngumu akiwa na mtoto mdogo anayehitaji malezi na matunzo ya baba yake.

Ombi hilo limekuja baada ya Katibu Muenezi wa Baraza la Vijana Taifa, Twaha Mwaipaya, kumtembelea nyumbani kwake na kusikiliza kilio chake.

Soma pia: Mahakama yaamuru Polisi kuwatafuta viongozi wa BAVICHA (kina Deusdedith Soka) waliopotea

Mke wa Frank Mbise alieleza kuwa mume wake alikuwa tegemeo kubwa kwa familia yao, na kutekwa kwake kumeacha pengo kubwa, hasa kwa mtoto wao mdogo.

Kwa masikitiko makubwa, alisisitiza kuwa mume wake alikuwa mwema na alikuwa anatimiza majukumu yake kwa familia, hivyo kumkosa kwa muda mrefu kumeathiri maisha yao kwa kiasi kikubwa.

Amemuomba Rais Samia afanye kila juhudi kuhakikisha Frank Mbise anarudi salama uraiani ili familia yao iweze kuendelea na maisha yao ya kawaida.

 
Mke wa Frank Mbise, kijana aliyetekwa zaidi ya siku 40, amemuangukia Rais Samia Suluhu Hassan, akiomba msaada wa kumrudisha mume wake nyumbani.
Akae chini atulie, avumilie mapito haya.
Yeye siyo mtu wa kwanza na Wala siyo mtu wa mwisho wa kupitishwa kwenye gharika Kama hii. Hizi ni gharama zitokanazo na kuruhusu uwepo wa tawala za kiimla katika nchi.
 
Akae chini atulie, avumilie mapito haya.
Yeye siyo mtu wa kwanza na Wala siyo mtu wa mwisho wa kupitishwa kwenye gharika Kama hii. Hizi ni gharama zitokanazo na kuruhusu uwepo wa tawala za kiimla katika nchi.

Kwamba atulie meanwhile mume wake ametekwa na hajulikani alipo?

Au sijakuelewa mkuu? Kuna ubaya gani kumuomba Rais wa nchi msaada?
 
Akae chini atulie, avumilie mapito haya.
Yeye siyo mtu wa kwanza na Wala siyo mtu wa mwisho wa kupitishwa kwenye gharika Kama hii. Hizi ni gharama zitokanazo na kuruhusu uwepo wa tawala za kiimla katika nchi.
Angekuwa ndugu wa damu kwako mdomo usingethubutu kuropoka, mbaya zaid unayeropoka ni mtoto wa kiume!!
 
Anayemwomba amsaidie ndiye aliyeidhinisha mabilioni kuingia kwenye account za watekaji
Na ndiye aliyeidhinisha na kuthibitisha Sheria ya kuwalinda na kuwatetea Watekaji na Wauaji wasiweze kuwajibishwa kwa namna yoyote ile, Wala wasishitakiwe mahali popote pale mara baada ya kutekeleza vitendo vyao viovu vya utekaji, utesaji na mauaji.
 
Mke wa Frank Mbise, kijana aliyetekwa zaidi ya siku 40, amemuangukia Rais Samia Suluhu Hassan, akiomba msaada wa kumrudisha mume wake nyumbani.
Mbona huyo anayemsihi alikwisha funga mjadala kwa kututaka tuzoee vifo.
 
Anayeua kwa upanga naye atakufa kwa upanga. Wao wana majeshi sisi tuna Mungu.
Ewe Mwenyezi Mungu muumba wa mbingu na ardhi,tunakuomba kama ulivyotuamulia ugomvi wa awamu ya tano utuamulie na huu wa awamu hii kwani kikombe cha maovu yao kimekwisha jaa. Kama ulivyofanya tarehe 17 March 2021 ufanye tena ili utufute machozi ya madhalimu hawa. Amen !!!
 
Anayeua kwa upanga naye atakufa kwa upanga. Wao wana majeshi sisi tuna Mungu.
Ewe Mwenyezi Mungu muumba wa mbingu na ardhi,tunakuomba kama ulivyotuamulia ugomvi wa awamu ya tano utuamulie na huu wa awamu hii kwani kikombe cha maovu yao kimekwisha jaa. Kama ulivyofanya tarehe 17 March 2021 ufanye tena ili utufute machozi ya madhalimu hawa. Amen !!!
 
Back
Top Bottom