Mke wa Rais wa Ghana kurudisha posho yote aliyopokea tangu Rais aingie madarakani ili kulinda taswira yake

Mke wa Rais wa Ghana kurudisha posho yote aliyopokea tangu Rais aingie madarakani ili kulinda taswira yake

Suley2019

JF-Expert Member
Joined
Oct 7, 2019
Posts
2,203
Reaction score
5,610
1626163558479.png
Mke wa Rais wa Ghana, Nana Akufo-Addo, Rebecca Akufo-Addo, amesema atarudisha kiasi chote cha fedha alichowahi kupokea kama posho tangu mumewe aingie madarakani mwaka 2017.

Hatua yake hiyo imekuja baada ya wananchi kulalamikia uamuzi wa Bunge kumuongezea posho na kufikia Dola 3,500 kwa mwezi, kama ilivyotokea pia kwa mke wa Makamu wa rais, kwa madai kwamba wamekuwa wakifanya kazi kubwa nyuma ya viongozi hao.

Kwa mujibu wa Rebecca, ameamua kurejesha Dola 151,618, jumla ya kiasi cha fedha alichokusanya kama posho tangu mumewe awe rais miaka minne iliyopita.

Akifafanua juu ya uamuzi huo, amesema amejisikia vibaya kwa namna watu walivyokosoa hatua ya Bunge kuwaongezea posho yeye na mke wa Makamu wa Rais, hivyo anataka kuilinda taswira yake.
 
Katakuwa ni kafisadi hako!

Kanajua pa kufidia
 
Hamna mwanamke atakayemtukana sababu tunajijua na tunafahamu sehemu atakayozifidia. Hakuna mwanamke anayezira pesa

Soma sababu yake,wakati anaongezewa alikubali ila wananchi walipoanza kulalamika ndipo kajishtukia
Wanawake wa Tanzania watamtukuna huyu mama kwa hii hatua aliyoichukua.
 
Mke wa Rais wa Ghana, Nana Akufo-Addo, Rebecca Akufo-Addo, amesema atarudisha kiasi chote cha fedha alichowahi kupokea kama posho tangu mumewe aingie madarakani mwaka 2017.

Hatua yake hiyo imekuja baada ya wananchi kulalamikia uamuzi wa Bunge kumuongezea posho na kufikia Dola 3,500 kwa mwezi, kama ilivyotokea pia kwa mke wa Makamu wa rais, kwa madai kwamba wamekuwa wakifanya kazi kubwa nyuma ya viongozi hao.

Kwa mujibu wa Rebecca, ameamua kurejesha Dola 151,618, jumla ya kiasi cha fedha alichokusanya kama posho tangu mumewe awe rais miaka minne iliyopita.

Akifafanua juu ya uamuzi huo, amesema amejisikia vibaya kwa namna watu walivyokosoa hatua ya Bunge kuwaongezea posho yeye na mke wa Makamu wa Rais, hivyo anataka kuilinda taswira yake.
Arudishe na riba asitake kudanganya Umma.

Ngapi wameiba na kuhamisha nje ya nchi?
 
Sio kweli kwamba kila rais wa kiafrika ni mwizi sikubaliani na hii dhana. Huyo mama kukubali kurejesha hizo fedha hakumaanishi kwamba yeye au mume wake ni mwizi.

Binadamu tunatofautiana, wapo ambao hawapendi kulaumiwa na wanajisikia vibaya kunung'unikiwa na wengine japo Tanzania hatuko hivyo labda ndio maana tunamshangaa huyo mama.
 
Back
Top Bottom