Mke wangu ana HIV nifanyeje?

huyo ni Mkeo? mlioana lini?, mbona katika maelezo yako sijaona hata sehemu moja mnayosema mlioana, mbona tangu mwanzo mmekuwa mkiishi kwa mikwara na fujo tu?

ndugu yangu Mungu ni mkubwa, hapa hapa hakuna wa kukushauri, uhamuzi unao wewe mwenyewe, we kaa chini na futa hisia zako na jipe uhuru binafsi wa kujudge, na mwisho wa yote utapata jibu zuri tu
 

You are not serious! Maelezo yako yana utata sana. Lakini kama ni kweli sikiliza nafsi yako inakwambia nini, mimi binafsi ninavyoogopa HIV sijui hata kama ningejiuliza mara mbili ktk hili!
 
aaahhh bwana kashaondoka mwenywe sasa start new life ushauri unao wewe au wataka mrudia akumalizeeeeeeeeeeee
 


Duuhhh pole sana mzee... lakini Mungu anamakusudi na kila mtu hapa duniani .... kwa hiyo usikate tamaa kabisa ya maisha ... cha kumshukuru Mungu ni kwamba we u mzima. .... Na ninaamini Mwenyezi Mungu alikukutanisha na huyo demu kwa makusudi yake..... kwa sasa nafikiri you need to take care of your self 1st mentally, emotional and physical..
 
Hi Hemed Maronda:

Vipimo vya siku hizi vya HIV viko very sensitive kutokana na maendeleo ya ki-technologia. Ukipima wiki nane toka ufanye tendo la mwisho la ndoa na majibu yakawa negative, basi uwezekano wa wewe kutokuwa na HIV ni mkubwa sana.

Tukija kwenye uhusiano wako na huyo mkeo, uamuzi huko juu yako. Lakini pamoja na hayo yote kumbuka yeye ni binadamu mwenzio, hivyo uungwana ni kitu cha maana kutendeana. Kuna kipindi mlifurahia maisha pamoja. Yeye kukutukana ni kitu kinachoweza kusababishwa na yeye kuchanganyikiwa na hali aliyonayo sasa. Kijana yoyote mwenye afya akipata HIV, anaweza kuchanganyikiwa na kufanya maamuzi yasio ya kawaida.

Kama una uwezo msaidie hili aweze kuishi productive life. Kuwa na HIV sio tiketi ya kifo.
 
Maronda pole kama ni kweli inaelekea umekufa umeoza kwa mpenzio. Pamoja na kuwa hadithi ulotoa ina mapungufu mengi lakini ninachowezakukuomba kwa sasa ni kutuliza moyo na kuomba MUNGU sana. As for your "wife" all I can say ni kuwa pengine yuko kwenye "denial" stage hajaamini na hataki kuamini kuwa ameathirika na ndio maana anaact kimiujiza. So tulia ikiwezekana tafuta watu wamshauri akapate ushauri nasaha .........anaweza akarudiwa na akili zake na kufanya maamuzi yaliyo sahihi.

Pole sana.
 

...Nadhani hakuna ushauri utaozidi hayo ambayo tayari ushatahadharishwa nayo.
Kubwa, uwe na msimamo thabiti kusimamia uamuzi wako wa kuachana nae ingawa bado unampenda.
Hii ni kwa faida yako mwenyewe, wema usizidi uwezo, na usipende ukawa kama mtumwa/mpofu.
Ngumu kwetu sie kuelewa kwanini bado ana chuki mbaya sana kwako na anaendelea kukutukana.
Kama alikutamkia dhamira ya kukuua, nakushauri jiepushe nae kabisa.

Pole sana kwa yote yaliyokukumba na kila la kheri kwenye kusimamia maamuzi na maisha yako..
 
Kama ni mkeo, basi jitahidi kusaidiana naye ili mwisho wa siku ajirudi na akuone wewe kama ni mwenzi wake kuliko mpinzani wake. Kwa bahati mbaya mara nyingi kuelewana inakuwa ni ngumu. Ila ukweli ni kuwa sote ni binadamu na tunafanya makosa. Hakuna aliye bora kuliko mwingine na mwisho wetu sooote ni futi sita chini. Yes, ndio maana nilimlilia sana super coach maana alikuwa mtundu sana na dunia hii.
 
Ndugu yangu kama mkristo katoe sada au kam muislamu sijui wenzangu huwa mnatoa zaka ............na umshukuru mungu kwa yote. Kama mwenzio anahitaji msaada na una uwezo, msaidi maana haya magonjwa wakati mwingine unaletewa bila kujijua. Matatizo yanndoa na familia/wazazi ni kitu cha kawaida tu, kila mzazi huwa anaona mtoto wake ni bora, haswa kama nyie wenyewe hamko strong kiuchumi. Mungu akusaidie, jaribu kupata ushauri kwa wataalamu wakuelekeze nini cha kufanya.
 
Wana JF ninawashukuru kwa mawazo yenu na ushauri,ni kweli ndoa kati yangu na huyo dada wa KINYIRAMBA haikuwahi kufungwa kwa kuwa mimi nilishindwa kulipa MAHALI ya Tshs 4,500,000/= labda wakwe zangu hawakutaka kunioza mtoto wao,mimi kwa Kabila ni MMAKUA,ila tukija kwenye utaratibu mwinginene ni kuwa tumeishi pamoja zaidi ya miaka miwili hivyo naweza kusema ni mke kwa kuzingatia jambo hilo.Waungwana napenda ni washukuru tena na msichoke kuniombea ili nibaki NEGATIVE,kwa upande wa dini mi ni Muislamu na tayari nilishaweka ahadi kuwa nikipima mara ya pili na kuonekana niko salama nimtolee MWENYEZI MUNGU SWADAKA,na tayari nimeshafanya hivyo.
 
Kapime mara tatu kila baada ya miezi mitatu. Halafu ukiwa fresh tafuta mwingine. Realationship is just a predestiny.
 
Mshukuru Mungu kwa kukunusuru na achana na huyo mwanamke kabisa.
 
mkuu kumbe wa kunyumba kabisa "CHIMKO"
 
osijali Mungu atakusaidia tu,unachotakiwa ni kuakaa chini na kuweka mikakati yako ya baadaye,na kujiweka bussy itakusaidia kidogo kumsahau huyo mwenzi wako,kwani najua kuwa sio rahisi kumsahau mwezi wako hata kama anamatatizo gani.
Mungu akutie nguvu na ujasiri zaidi.
Lakini mimi ninahisi kuna uwezekano kuwa wazazi wake (familia yake) walikuwa wanajua ndio maana hawakutaka wewe umuoe( naanisha kukwambia utoe mahali/posa ya milion 4 na nusu) na kumbuka akutukanaye hakuchagulii tusu,kuna uwezekano hawakutaka kukueleza hali halizi ila walivyotoa hiyo mahali walijua kabisa utashindwa na kumwacha mwanamke.:doh:
 
@mbogodume.

lol najaribu kutafakari Avatar yako inamaaninsha nini?? ndo wamekutana au ndo wanachana it look very funny..lol:smile:
 

Great... kuwa makini zaidi next time..
 
Bwana Hemedi me wanchanganya kidogo.Huyo mwanamke si mke wako kwani sijaona mahala kwenye hiyo post panapoonesha mlifunga ndoa,ila ulisema mahari ilikuwa kubwa ukashindwa na mke akakufuata Mbambabay.Kaka bado hujaoa acha ZINAA tafuta mke uoe.Zidisha ibada na umshukuru MUNGU kwa kukuepusha na maradhi hayo,ila usimtenge huyo mwenzio kimisaada.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…