Shamkware
JF-Expert Member
- Nov 25, 2013
- 1,750
- 2,283
Mke wangu ananyonyesha mtoto mdogo wa miezi mitatu sasa! Lakini amekuwa akipatwa natatizo ambolo hata sielewi ndo ugonjwa gani! Amekuwa akiumwa na matiti yani yanavimba halafu yanauma ukigusa tu anapiga kelele na maziwa yanagoma kutoka, yani anakesha analia yakianza kuuma, hospital nilimpeleka dakitari akanipa vidonge vya kutumia tu huku akinipa ushauri ambao eti ni kawaida kwa wamama mtoto akimcheulia kwenye nyonyo huwa maziwa yanauma hivo! Naomba msaada wenu hasa kujua kwa wamama pamoja na madakitari hali hii ni kawaida au ni tatizo linalosababishwa na nini mi nawaza zisije kuwa dalili za kansa ya ziwa naogopa sana aisee!!