assuredly4
JF-Expert Member
- Nov 7, 2011
- 1,216
- 220
huu ushauri nao kiboko..kweli kuna umuhimu wa kwenda church ku-refesh yaliyopita.Wala usiache Mwanamke Mchawi aishi..................................kwahiyo mhurumie kwa kumuachia uhai wake ila mpige chini (achana naye).............uchawi ni roho hawezi kuacha kwa kusemwa au maonyo, watu wengi wanapenda kuacha uchawi, lakini shughuli namna ya kutoa hizo roho. Kama unampenda na hutaki kumuacha mpeleke kanisani afanyiwe maombi ya kuondoa roho chafu, mikataba, na uchawi na pia aonyeshe vitu vyote alivyowahi kupewa na mganga na sehemu alizowahi kuviweka ili navyo viombewe na kuchomwa moto.........
TUNASUBIRI!iDuniani kuna mambo! Mie ni Dadaake mke wangu, binti wa miaka thelathini na kidogo lakini habari zake si nzuri! Jana kanisimulia mambo ambayo sikupaswa hata kuyasikia na sikuamini kuwa ni mshirikina kiasi hicho! Kwa bahati mbaya sitaweza kueleza story yenyewe kwa sasa ila niliishia kuamini tu kuwa MAOMBI yana nguvu hata kama unasali kwa mazoea tu! maana ali-confess mbele yangu kuwa wamenishindwa!! so hata hili nalo laweza kuwa kweli, ntaanzisha thread nikiwa na computer nielezee kwa mtindo wa "rafiki yangu"
Wahenga wanasema ukistaajabu ya Mussa utaona ya Firauni....!!!
Rafiki yangu wa karibu sana jana kidogo agongwe na magari baada ya kumfuatilia mke wake kwa umakini zaidi na kugundua kuwa mkewe anahusudu sana na anashiriki katika mambo ya kishirikina. Kwa sababu mke wake huyo anafahamu kuwa mumewe hapendi haya mambo ya kishirikina, basi ilibidi ayafanye kwa tahadhari sana ili kuhakikisha kuwa mume wake hafahamu kinachoendelea.
Mumewe alikuwa anahisi kuwa mkewe anashiriki ktk mambo hayo. Mambo yalikuja kuharibika pale mumewe alipomtegea vitu vya kunasa sauti katika maeneo ya nyumbani na maeneo ambayo mkewe anafanyia kazi zake na kushitushwa na mawasiliano ya kulipana pesa baina yake na mganga wake huyo.
Baada ya mumewe kugundua hivyo na kupata ushahidi wa sauti, mkewe alijitetea kuwa anajilinda mwenyewe na anashughulikia afya yake na kuwa eti hana mpango wa kumdhuru yeye.
Anasema mkewe baada ya kuona ishu imevuja kaomba msamaha na kuahidi kuwa hatafanya tena upuuzi huo. Mume anasema haamini maneno hayo, anadai labda mkewe anasema hivyo ili kujipanga zaidi na kuhakikisha kuwa nyendo zake hazivuji tena.
Sasa jana rafiki yangu huyo kaja povu likiwa linamtoka akisema kesha mzaba mkewe vibao kadhaa na anafikiria kuachana naye. Kaniomba ushauri afanye nini maana keshachanganyikiwa baada ya kugundua kuwa mkewe amekuwa akifanya mambo hayo behind the door!
Kaja kuniomba ushauri na mimi nikaona sio vibaya nikaliweka hapa jamvini ili watu waweze kunisaidia kumshauri rafiki yangu katika kipindi hiki kigumu!
Mh! Lazima utakua nawe ni Fundi (mtaalam) wa hayo mamboz.mwambie ambane atupatie historia yake ni lini ameanza kufanya mambo hayo, tangu akiwa mtoto au hivi karibuni.
je ameridhishwa mikoba au amejifunzia katika saloon za kike mnakowaruhus wake zenu kushiriki umbea na baiashara ya ngono bila ninyi kujua. saloon kuna mambo waulizeni wanawake watawaeleza
unalosema ni kweli kabisa. siwezi kuacha kutumia third part kama ishu inamhusu third part, ingekuwa inanihusu nisingehangaika kuweka third part...hii ni kwa sababu humu jf hatutumii majina halisi kwa hiyo hata kama nikisema ni ishu yangu huwezi kunfahamu/kunitambua.
Lakini heading ya thread yenyewe inaonesha ni mkeo. Kuwa mpole tu rafiki maana hukujipanga vizuri.
Superstitious goat.
With wives like these, who needs marriage?
Kiranga, huyo mke anahitaji sana elimu, na huwezi jua; uwezekano mkubwa amekulia kwenye familia ya kishirikina.
Tukirudi nyuma, wafanyabiashara wakubwa wangapi washirikina, mafisi wangapi wa serikali ni washirikina, wanasiasa wangapi ni washirikina?
Can you say, 'with leaders like ours; who
needs leadership?'
Kwa nini mnapenda kutumia neno rafiki yangu, badala ya ninyi wenyewe? hao rafiki zenu ni kwa nini msiwashauri wawe member wa JF? nahisi udanganyifu mtupu kuwatumia third part kwa karibu kila thread.