Mke wangu anapata maumivu kwenye mshono wa oparesheni ya uzazi

Mke wangu anapata maumivu kwenye mshono wa oparesheni ya uzazi

AbuuMaryam

JF-Expert Member
Joined
Dec 26, 2015
Posts
2,577
Reaction score
4,637
Jamani naombeni msaada wa mke wangu kusumbuliwa na maumivu makali ya mshono, yanayokuja na kuondoka leo yamezidi alijifungua kwa operation miezi minne iliyopita anaumia sana mpaka namuonea huruma.

Yaani kwenye sehemu ya mwanzo ya mshono kama pamebonyea sio sawa kama nyingine zilizoinuka as for example mtu aliyewahi kuchwanjwa na kitu akiwa amepona lile kovu lake..naombeni msaada...

Akikohoa ndo panauma...

Sasa sijui ni vile aliambiwa asikanyage maji maji ya baridi au sakafu ya baridi awe anavaa soksi au ndo kumbeba mtoto mara kwa mara labda yaani sielewi naombeni msaada wa mawazo nifanye nini?

Sina hela kwa kweli usiku huu wa kwenda hosp ndio maana nikaja hapa ila sijaomba mnisaidie hela inshaa allah amlaze salama mke wangu kesho nitatafuta nitapata na inshaa allah ushauri wenu nitaufanyia kazi nikijaaliwa...

Naamini allah amejaalia wataalamu humu

IMG-20190223-WA0006.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu Hii ni emergency case nendeni hospitali. Anapata homa?
 
Pole mkuu,Mungu mwema wanakuja wataalam,daa kwa kuangalia tu kisu kilivo pita hapo nimeumia sana....

Mungu awalinde usiku huu kesho mtafute tiba!Mpe pole shem!
 
Mkuu huu si muda wa kumtaja mungu mungu peleka huyo kiumbe hospital madaktari ni watu wanaweza kukuelewa
 
Fanya maarifa ndugu yangu ukope hata huu usiku kwa ndugu au kwa marafiki wa karibu usiku ni mkubwa. Suala la afya(uzima) hilo ubavu wako una umia fanya maarifa usiku huu huu muende hospital.
 
Hii kitu ndio inayonifanya nimuonee mwanamke uruma,akuna kitu kinachoniumizaga kama kumuona mwanamke akitolewa chumba cha upasuaji akiwa hajitambui daah!

Mkuu MUNGU ampe shemeji yetu nguvu na afya ya uponyaji wa haraka pia jaribu kumuona daktari wa mama na mtoto kuna vidonge wanapewaga ili kuimarisha huo mshono maana huo unachukua mda kupona kwa ndani japo kwa nje unaonekana umepona

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom