Habari wanajamvi?
Katika ziàra zake akiwa Kanda ya Ziwa Mukulu alitoa agizo kwamba katika kipindi chake tufyatue tuwezavyo. Agizo hilo mimi nililipokea kwa furaha kwa mikono miwili, na nilipanga kuanzia leo hadi 2025 niwe nimemfyatulisha watoto 5, wanaume 3 na wakike 2. Ila mke wangu amepinga agizo hilo la ufyatuaji na kwamba anendelea na zoezi lake la uzazi wa mpango. Sasa kwa ukaidi huu wa agizo la mkulu umenifanya nifikirie mara mbili aidha nimtumbue au nimfanyeje? Unajua agizo la mkulu ni sheria? Maoni yenu tafadhari