Mkenya pekee anayejua mziki

Ni kweli wanafuata pesa lakini utafuataje pesa bila ya kuwana soko?

Wanaoleta bidhaa zao huko inamaana wanajua soko lipo.

Unafikiri Kenya ndiyo penye pesa tu Afrika au duniani? Ila kwasababu wakenya wanaipenda bidhaa ya Solomoni mkubwa ndiyo maana wanaigharamia na kuinunua.

Kenya mnajitahidi kuimba ila Watanzania kwa hili tunawazidi.
 
hapa tuseme tu kuwa 'starehe ya kuku sio ya bata'
kwangu, bongo nawatambua tu Kiba na Diamond. wengine wote hawafiki bei.
Nikikwambia kuwa ni wabongo wachache sana wanawajua wasanii wa kenya utashangaa! Ila ndiyo ukweli!
 
katika music industry ya sasa bongo fleva inashindana na Nigeria only hawa wakenya wanaujua ukweli ila wanajifanyaga wabishi tuuu
 
Eeh bhn eh
wanamziki wa kibongo wanakuja kuponda mali na kuishi Kenya. Jana usiku nimempata matonya kwa roadblock ya polisi pale parklands akiwa ametiwa mbaroni kwa kosa la kuendesha gari akiwa mlevi.
 
katika music industry ya sasa bongo fleva inashindana na Nigeria only hawa wakenya wanaujua ukweli ila wanajifanyaga wabishi tuuu
Hatujafika level ya Nigeria ila wakenya hawatukuti.

-South Africa
-Nigeria
-Ghana

wapo mbele...

Nigeria wao wana diamond zaidi ya 5. kina Alikiba nao ni wengi... South nao vile vile.

Mziki wa Tanzania unasikilizwa saana Kenya zaidi ya mziki wa kenya unavyosikilizwa Tanzania.
 

hujanielewa! mziki wa bongo uko targeted kwa the Kenyan Market kwa kiwango kikubwa, watu kama Solomon mkubwa wanaishi Kenya na wameanzia mziki pale na vipaji vyao vinakubalika.

Nikikwambia kuwa ni wabongo wachache sana wanawajua wasanii wa kenya utashangaa! Ila ndiyo ukweli!
siwezi kushangaa sababu ni ukweli.
 
Khaligraph kwa East afrika kwa lipi kana?

Khali ni Rapper tu kama alivyo Octopii..

Nshiski sawa...ila anabore hachange mazee ni yule yule.

BTW;music ni feelings ni vyenye unakutouch.
Inapendeza San ,comments Zak ziko poa
 
Kumlinganisha caligraph na Fid Q ni sawa na kulinganisha titi na kalio. Fid ni level nyingine kabisa.
 
Mzee .hayo yapo mfano ni ajali za ki MV nyerere na MV bukoba.ni matambiko hayo
waAfrica tuwache hizi akili za kijinga! ajali ni ajali na tukishakubali hilo, tutaweza kufanya jitihada za kuzuia ajali nyingine kama hiyo.
 
hujanielewa! mziki wa bongo uko targeted kwa the Kenyan Market kwa kiwango kikubwa, watu kama Solomon mkubwa wanaishi Kenya na wameanzia mziki pale na vipaji vyao vinakubalika.


siwezi kushangaa sababu ni ukweli.
Mzee baba hatuelewani...

Ninasema Watanzania wanaimba kitanzania na kwa Utanzania kabisa.

Ila wakienda kenya bidhaa yao ilishafika na inakubalika. Lugha rahisi wakenya wanapenda Mziki wa Tanzania.

Hawa wote unaowaona wamehamia kenya Huku kwetu ni wasanii wa ziada...

Leo Diamond akija kufanya show Nairobi Show itakuwa kubwa kuliko msanii yeyote akija Tanzania akitokea kenya.
 
Ni kwel kabisa.ila wenzetu wana upcoming wa nguvu San yan
 
Nilpenda km vile Alikiba angemsainisha otile kweny label ya rockstar.Otile anajua san,.ni level za kina mavoko
 
Ipo vizuri hii nyimbo, Anakuja vizuri dogo. Lugha pia anaijua tofauti na waKenya wengi
 
Wakenya mna kiswahili gani bhana na nyie mnapenda kubisha hata yasiyobishika.

Msanii gani anaweza kuimba kiswahili kilichonyooka kenya kama wanavyoimba vijana wetu karibu wote. Kenya kiswahili No. japo mnajitahidi
Kuja mombasa wewe upewe vitu na waswahili wenyewe...wacha porojo...we wajuwa kingozi kwel..au unfanya kukiskia tu...kiswahili si cha watanzania..kiswahili ni cha waswahili...hv nikuulize dar kuna kabila la waswahili...
 
Kuja mombasa wewe upewe vitu na waswahili wenyewe...wacha porojo...we wajuwa kingozi kwel..au unfanya kukiskia tu...kiswahili si cha watanzania..kiswahili ni cha waswahili...hv nikuulize dar kuna kabila la waswahili...
Sasa hadi uende Mombasa ? Tanzania popote pale ukienda kiswahili kinazungumzwa.

Cha kufanya sema kuna kiswahili cha Kenya na cha Tanzania. Ila hata mtu wa kakamega huwezi mfananisha na wa Mombasa. Mtaanza kukataana wenyewe kwa wenyewe.
 
South Africa na Ghana?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…