Mkiona mgonjwa wenu hawezi kupona, mrudisheni akafie nyumbani. Akipelekwa tu Mortuary mtadaiwa mamilioni msiyoyaweza

KING MIDAS

JF-Expert Member
Joined
Dec 1, 2010
Posts
8,589
Reaction score
16,936
Nchi hii imekuwa ya hovyo sana, huduma za afya na matibabu zimekuwa mbovu na duni kabisa.

Kila siku tunasikia sehemu mbalimbali watu wakifa kwa uzembe wa madaktari na manesi.

Mbaya zaidi mgonjwa akifa haraka haraka anakimbizwa mortuary ambako kama hamna mamilioni kadhaa, ndugu yenu atazìkwa na halmashauri, mazishi yasiyo na heshima wala staha wala stara.

Wito wangu kwa Watanzania wenzangu, mkiona mgonjwa wenu hana dalili za kupona hospitali, mrudisheni nyumbani kuepuka kadhia ya kudaiwa mamilioni mengi wakati wa kuchukua mwili wake.
 
Waambie CHAWA wanaoanzisha nyuzi za kusifia humu JF kila siku kina CHOICE VARIABLE,LUCAS MWASHAMBWA, JIDULABAMBASI,KABENDE MSAKILA nk wachangishane wakakomboe maiti ya Mtoto wa miaka 5 iliyozuiliwa Muhimbili kisa inadaiwa 2,400,000
 
Kuna Siku Nilikuwa Muhimbili pale wodi ya Mwaisela napiga michango nakuta Familia ya Kiarabu ya watu kama watatu wanalia,nikamdodosa mmoja akaniambia Shangazi Yao kafariki wanafanya process za kuchukua mwili,nikamuuliza amefariki lini?akajibu Leo wakati tunamleta kufika hapa kumbe alikuwa amefariki kwenye gari,wamefika pale Dr anawaambia mbona alishafarki!Wanataka kugeuka na Mwili wa Shangazi wanaambiwa hapana upelekwe Mochwari.Jamaa waling'ang'aniwa mpaka maiti ikapelekwa Mochwari Sasa msala kuitoa.
 
Hayo mamilioni yanayodaiwa ni bill ya kuifadhi mwili mochwari? Au kunakingine
 
Huu ni upuuzi, hospitali mtamdai nini mtu aliyefiwa na mgonjwa wake, si aruhusiwe tu achukue maiti yake akaizike? Kuna jamii mtu wao akifa fisi wanaachiwa wale mzoga huo, sasa kama kafia hospitalini wakianza kudai gharama kubwa mbona wanaachiwa tu wawape wanafunzi wa udaktari wakajifunzie kupasua viungo kama spacemen
 
Kulaza mwili mochwari ni kiasi gani kwa siku?
 
Ukiona mambo kama haya elewa unaishi in a shithole country, kila family ilitakuwa iwe na uchaguzi na uamuzi wa wapi maiti yao ikahifadhiwe, kama nchi tulitakiwa tuwe na private undertakers, means unapeleka mwili wa mpendwa wako kwa undertaker unayemtaka,pia ni wajibu wa undertaker wako kukuandalia death certificate kutoka home affairs, sio uchafu uliopo hapa nchini, Ile idara ya vifo na mirathi ilitakiwa futilia mbali uchafu ule, sawa na msajili wa vyama futilia mbali, vyama vikajisajili NEC.
 
CCM ni Chanzo Cha Matatizo yote nchini
 
Duuuh!! Mbaya sana hii
 
Ipo siku watu watakuja kususia miili ya waliofariki ikae huko huko mortuary ijazane sijui wataila nyama!!
 
 
Ipo siku watu watakuja kususia miili ya waliofariki ikae huko huko mortuary ijazane sijui wataila nyama!!
Mmoja toka Lindi alisusa,kamleta mkewe alipewa referral kuja pale mkewe kajifungua bahati Mbaya kaondoka,huku na huku Wanataka Mil 3 hiyo nauli ya kuja tu ndugu walimchangia kazunguka wiki mzima Kila ofisi wapi.Karudi temeke alikofikia kaweka Msiba siku tatu, baada ya hapo watu wakatawanyika arobaini Lindi.Ninyi na hiyo Mochwari yenu mtajijua.
 
Akili kubwa hiyo[emoji1787]maisha magumu bado ukamuliwe na Kodi ya Maiti kweli!!!hapana
 
Tena huko Lindi ndio wanachagua MATAGA sana ataenda kuwasimulia wenzake kilichomkuta hospitali DAR.
 
Hii kero ya miili kuzuiwa iliyoletwa na serikali ya CCM ipelekeni kwa waziri kiongozi mwenezi makonda itatuliwe on the spot.
Sasa hivi tunayo hii fursa ya kupeleka kero zetu. Tuitumie otherwise mwakani huyu akipewa ubalozi itakua business as usual.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…