Mkoa au Wilaya gani naweza kwenda kuanza maisha kutoka chini kabisa (from zero)?

Karibu mbeya....kabla hujakaribia nipe hatua nawezaje pata kazi Vodacom customer naanza wapi
 
Karibu Iringa ukamate heka zako tatu ulime mahindi ya kuchoma, kila heka utapiga milioni mbili na itachukua miezi 4 mchakato wote kukamilika
mkuu mi napenda kuzalisha, shughuli km kilimo na ufugaji ndo napenda. target yangu nianzie from zero lakini naangalia uwezekano wa kutanuka zaidi kuelekea kwenye shughuli kubwa za kuzalisha

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Siku nyingine jaribu kuwa muwazi usaidiwe. Kuna information kadhaa ni muhimu kwa mfano una ujuzi gani/elimu yako/umri wako na mengineyo however, maeneo kama Babati/Magugu, Mafinga, katoro/Buselesele ni maeneo unayoweza kuanza upambanaji bila mtaji. All the best


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Nenda mitaa ya bukundi uko meatu, kuna bwawa wanavua samaki, wavuvi wanauza samaki mmoja shilingi 15 mpaka 20. Na sasa hivi ndo msimu wake mpaka mwezi wa kumi.


Imagine hio laki mmoja yako utabeba samaki wangapi, mchawi ni kutafuta soko pakwenda wauzia ni wale samaki aina ya perege.

Kule maisha ni cheap sana utatoboa ukiwa mvumilivu.
 
Write your reply...Nenda morogoro fanya biashara ya mazao
 
Nenda Singida mkuu unaweza ukakosa pesa lkn ukafanikiwa kuoa toto la kiarabu lkn waarabu koko


Sent using IPhone X
Hapo Singida waarabu wanakaa wapi?,nimeenda kama mara mbili town pale hao sijawaona uliowaita "koko".Maeneo niliyoenda ni "ubungo" stand ile mpya, mitaa ilipo nmb bank na kule nbc,uwanja wa namfua kwa haraka
 
Nenda mbeya au Sumbawanga kakusanyanye mazao kama mpunga mahindi au ngano kwa msimuu tayari mavuno zama pori kabisa intilia uko tafuta dalali apo mjin anae jua kucheza na soko vizur unapeleka mzigo unachukua chako unalud poli kuchukua mzigo usitake faida ya juu kama huna mtaji wa maana Tembea mdogo mdogo kabla ujaanza kukimbia within 2 years utakuwa mbal lakn pia ujue biashara inapande mbili wazee wa forex humu wana experience ya kutosha
 
Swali lako liko kiujumla sana, kuna mtu kauliza umri wako,uzoefu wako,una familia inakutegemea n.k sasa hatujajua hata unapenda ungependa kufanya shughuli gani na malengo yako katika hiyo shughuli.
Kila sehemu mambo ni magumu kwa "aina yake" kote wanakokwambia kuna masikini kibao pia,hivyo story za "ukija baada ya miezi michache unatoboa" sio kweli,unless uwe na mtaji kweli kweli,mwongozo na kushikwa mkono.
Kikubwa watu wakupe tathmini ya gharama ya maisha ya maeneo hayo,ili ujipime na nguvu yako ya kipesa kwa sasa.
 
Nenda Ifakara kalime mpunga , kwa hali ya hewa ilivyo mvua zinanyesha mwaka mzima. Na maisha yapo chini kuna watu waliondoka wakiwa zeo wakaenda huko kwa sasa wana maisha yanayoeleweka na wanaendelea na kilimo. Kama unataka connection karibu PM.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…