Mkopo kutoka Benki

Kukopa ktk ma benki ya tanzania labda uwe unafanya biashara ya bangi,riba zake kubwa sana!maneno ya nyerere hayo
BOT wangekuwa makini huu wizi usingeendelea lakini sasa wapo pamoja, Xmasi wakipelekewa zawadi wanawaachia. Katika Banking kuna kitu kinaitwa SPREAD ama kitu kama hicho ambacho ni Tofauti kati ya RIBA kwenye mkopo na riba unayowapa watu wanaoweka pesa ktk benki yako. Inatakiwa iwe ndogo yaani iwe single digit. Hapa BONGO ni BALAA waweza kukuta RIBA kwenye Mkopo ni zaidi ya mara kumi ya riba wanayotoa ukiweka pesa zako kwa ujumla ni balaa. Halafu mwisho wa mwaka wanatangaza faida asilimia 34% wananunua mikate miwili na unga kilo 100 wanaendakutoa msaada katika kituo cha watoto yatima eti wanarejesha kwa jamii
 
Kwa expiriance yangu ni atlest saccos wanakua open zaidi ya benki na hesabu zao hata kama huna ujuzi sana unazielewa maana ni deni +interest kisha total inadividiwa na tym ya marejesho.hamna longolongo nyingine, tatizo tu ni lazma uwe na hela ndo upate hela tofauti na mabenki
 
Duu hii mikopo ya kwenda kufungia ndoa hii inatuumiza
 
Mkopo? ni hatari sana kama hukupata elimu vizuri juu ya wakopeshaji,wengi ni matapeli.
siku hizi wizi umehamia kwenye kalamu
 

Kaka bongo hii mbona tutakufa na mikopo maana haikwepeki mishahara ya CCM nayo midogo. Usione majumba yanasimama pembezoni mwa mji. Mi pia ni mteja mzuri wa NMB naweza kusema ndo wamenilea hapa mjini. Swali langu inakuwaje pale unapotop-up? Kwa mfano unamkopo wa miaka 4 kisha umelipa miezi 12 na unataka kutop-up wanachukua kiasi kile ulichokopa ama wanafanyaje?
 
Wakuu, biashara ni ngumu hapa Bongo kama ukikopa benki kichwakichwa. Kuna vijimicrofinance viiiingi vimeanzishwa na former loan sharks navyo ni balaa tupu. Mtu anakuambia bila aibu njoo nikupe mkopo lakini utanirudishia 10% ya ulichokopa kila mwezi. Eti nae anataka umpe collaterals kama hati ya nyumba, gari nk. Yaani tunaumizana vibaya mtaani siku hizi. Ushauri: Ogopa sana mikopo hasa yenye riba zisizoeleweka!! n hatari zaidi ya ukoma
 

Wewe tunashare the same experience, mimi ninamobilize wanasheria wangu kufungulia bank mbili mashtaka ya bank hizo kuvunja sheria ya mabenk inayokataza mabank kubadirisha terms za mikopo bila makubaliano na wateja, inaonekana ni mchezo wa kawaida kwa mabank kuwacharge wateja interests rates za juu, penalty charges na mafee mengi kinyume na sheria.

Nadhani yanafanyia kazi ukweli kwamba watanzania hatujari kabisa kuangalia matumizi yetu na kisingizio kwamba banking ni special profession, hakuna profession kwenye hela, hela ni hela.
 
Dah!ss cjui tukakope wapi?
Mikopo imesaidia watu wengi. la muhimu ni kujua na kutafuta washauri wataalam wa maswala ya Financing iwapo huna utaalamu wa kutambua jinsi ya mkopo unavyochukuliwa na kurejeshwa kwa riba bila kuleta hatari ya kupoteza mali zako.
Mkopo wowote na riba yake inategemea jinsi ulivyokuwa structured.

Mkopo wote umeshakuwa dscounted to present value kwa kutumia rate mnayokubaliana. na si kweli interest rate iongezeke wa kati wa kuservice hiyo loan huko kutakuwa ni kuvunja makubaliano ya mkopo unless kamakuna kifungu ktk mkataba wa kuongeza hiyo interest rate.
Kama huelewi mambo haya vizuri yanaleta shida na pengine kupelekea kufirisiwa au usiweze fanikisha lengo lako.
Ni vyema kwa mtoa mada arudi kule kwenye Benki yake na kuona jinsi gani ataweza kurekebisha structure ya hiyo loan.

Kwa siku hizi ziko Benki zingine zinaweza kununua mkopo huo( yaani wanairejeshea Benki iliyokupa mkopo na kukupa mkopo mwingine kwa masharti na makubaliano mapya.

Financial management consultants wakusaidie.
 
long term loan ni majanga kwa walala hoi jamani...kopeni kwa muda mfupi isizidi mwaka
 

Asante ndugu yangu itabidi niwatafuta hao watu hapo kwenye red ili wanifafanulie. Si mnajua kila mtu na fani yake! mie fani yangu biashara.
 
Inategemea kama ni 'policy' gani ya mkopo wanatumia. Kuna 'interest based on reducing balance' na 'interest based on original balance'.Hivyo ni muhimu kuusoma na kuuelewa mkataba wa mkopo.Kwa saccos, mkopo wa mwaka mmoja wanachukua interest ya 13%, miaka miwili 25%, miaka mitatu 37% na miaka minne 49% n.k Uzuri wa saccos ni kwamba 'at least' 30% au 50% ya mkopo inakuwa hela yako mwenyewe..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…