Mkopo milioni 35 wewe unachukua milion 5.

Mkopo milioni 35 wewe unachukua milion 5.

Majaribu2013

JF-Expert Member
Joined
Jul 3, 2013
Posts
952
Reaction score
1,049
Mimi ni mbeba box wa kawaida ambaye kipato changu ni chakawaida, ninahitaji mkopo wa milion 35 halafu hizo milion 5 nampa aliyenifanikisha kupata hiyo loan. Kwa kazi yangu ya box naweza kuulipa ndani ya miaka 4 hadi 8, nikijumlisha na zali la biashara nitakayokuwa naifanya naweza kulilipa mapema zaidi.

Ukweli sina sifa kama wanazotaka bank, dhamana ya nyumba sijui biashara mimi sina. ila nina uhakika wa kulipa huo mkopo kama nilivyoeleza hapo juu.

Nani mtalaamu aniunganishie pande??? Tukipewa tu hata saivi hiyo milion 35 nakuhesabia hapohapo milion 5 zako unakwenda zako.

Nisaidieni.

#Majanga
 
Kwa kifupi unahitaji mkopo wa shilingi milioni 35 bila kuweka dhamana ya mali inayoendana na milioni35 right? ila maneno yako tu kuwa una 'uwezo wa kulipa' ndio yawe dhamana tosha si ndio mkuu?
 
Kwa kifupi unahitaji mkopo wa shilingi milioni 35 bila kuweka dhamana ya mali inayoendana na milioni35 right? ila maneno yako tu kuwa una 'uwezo wa kulipa' ndio yawe dhamana tosha si ndio mkuu?

Mkuu siyo maneno tu, nitaweka pia mambo mengine kama mikataba ya kampuni ninayobebea box, sehemu ninakoishi, bplan ya biashara ninayoombea mkopo n.k
 
Una wazo zuri lakini kwa nchi yetu hii labda ukopeshwe na ndugu na sio tahasisi hizi za kibenki.kumbka milioni 35 kulipa kwa miaka 8 unaweza tozwa riba ya 25% kwenja juu.Ukijumlisha utakuta unahitajika kulipa kama 43milions.Kama box unapiga serikalini hapo sawa ila kama ni kwa muhindi ni ngumu mtu kukudhamini.
 
Una wazo zuri lakini kwa nchi yetu hii labda ukopeshwe na ndugu na sio tahasisi hizi za kibenki.kumbka milioni 35 kulipa kwa miaka 8 unaweza tozwa riba ya 25% kwenja juu.Ukijumlisha utakuta unahitajika kulipa kama 43milions.Kama box unapiga serikalini hapo sawa ila kama ni kwa muhindi ni ngumu mtu kukudhamini.

Duh hapa ndo namaliza nguvu kabisa, yaani business yangu ningepata hiyo pesa hatan hizi zingerudi mapema kwelikweli. Mungu nisaidie
 
Miaka 4 mingi sana huwezi kupata huo Mkopo kwneye taasisi na kupewa na mtu ndio kabisaaa maana huwa watu binafsi wanategemea pesa zao zirudi mapema mapema.
 
una wazo zuri lakini kwa nchi yetu hii labda ukopeshwe na ndugu na sio tahasisi hizi za kibenki.kumbka milioni 35 kulipa kwa miaka 8 unaweza tozwa riba ya 25% kwenja juu.ukijumlisha utakuta unahitajika kulipa kama 43milions.kama box unapiga serikalini hapo sawa ila kama ni kwa muhindi ni ngumu mtu kukudhamini.
kwa serikali inawezekana vipi wa bukoba?
 
kwa nn hiyo 5 umwachie huyo atakaekusaidia? hii sio dalili nzuri
 
kwa nn hiyo 5 umwachie huyo atakaekusaidia? hii sio dalili nzuri

Kaka hii ndiyo bongo ni jasho la aliyeshughulika mpaka akakufanikishia vya bure viliisha enzi za nyerere
 
User name yako.. inaogopesha ukizingatia na hilo ombi
 
kwa nn hiyo 5 umwachie huyo atakaekusaidia? hii sio dalili nzuri

wasi wasi na hili pia... sio ndo kutokomea na 30 mils za watu ukizingatia hakuna fixed asset yeyote ilowekwa rehani...mh!! You're drunk go home. ..
 
wasi wasi na hili pia... sio ndo kutokomea na 30 mils za watu ukizingatia hakuna fixed asset yeyote ilowekwa rehani...mh!! You're drunk go home. ..

sidhani kama ungeniona ungesema hayo au ungefika ofisini kwangu, usifikiri kila mtu anakuwa vile unavyomtizama
 
sidhani kama ungeniona ungesema hayo au ungefika ofisini kwangu, usifikiri kila mtu anakuwa vile unavyomtizama

Mkuu ni msaada tu tunapeana hapa , kwa jinsi ulivyoeleza hapa ni ngumu sana kwa financial institutions nyingi kukupa huo mkopo...
 
Mi ningekupa lakini sio bank na niko far, sa ukishindwa kulipa au ukifa je?
 
Mi ningekupa lakini sio bank na niko far, sa ukishindwa kulipa au ukifa je?

hapo ngumu kwakweli, maana inahitaji uniamini kwelikweli, nikifa nina familia watakulipa kutokana na biashara au unaweza kuiza biahsra yote ukachukua pesa yako
 
Mkuu risk ya kutoa milioni 35 kwa mtu asiye na dhamana wala haeleweki ni kubwa sana. Na pia hujaeleza riba itakuwa kiasi gani, yaani unaona kama hiyo milioni 5 ndio riba yenyewe au ni mlungula kwa banker atakayepindisha taratibu za benki kukuwezesha kukopesheka??

Kwa kifupi maelezo yako hayatoshelezi kabisa kumridhisha mkopeshaji. Na ile mikopo yetu ya uswahilini ya kulipana ndani ya muda mfupi riba yake huwa ni zaidi ya 20% kwa mwezi, which means ka_milioni tano kako hakafikii hata riba ya mwezi mmoja kwa ile mikopo ya benki binafsi za uswazi. Mkuu nakuhakikishia kwa hapa duniani hutopata huo mkopo, labda ahera.
 
Mkuu risk ya kutoa milioni 35 kwa mtu asiye na dhamana wala haeleweki ni kubwa sana. Na pia hujaeleza riba itakuwa kiasi gani, yaani unaona kama hiyo milioni 5 ndio riba yenyewe au ni mlungula kwa banker atakayepindisha taratibu za benki kukuwezesha kukopesheka??

Kwa kifupi maelezo yako hayatoshelezi kabisa kumridhisha mkopeshaji. Na ile mikopo yetu ya uswahilini ya kulipana ndani ya muda mfupi riba yake huwa ni zaidi ya 20% kwa mwezi, which means ka_milioni tano kako hakafikii hata riba ya mwezi mmoja kwa ile mikopo ya benki binafsi za uswazi. Mkuu nakuhakikishia kwa hapa duniani hutopata huo mkopo, labda ahera.
mh, maelezo zaidi naweza kutoa kwa mtu atayekuwa tayari siwezi kumwaga kila kitu hapa.
 
Back
Top Bottom