wamogori
JF-Expert Member
- Mar 20, 2013
- 888
- 339
Nakubaliana na wewe kabisa, hila unaweza shauri nini kuhusu kiswahili? Labda TBC1 redio kidogo wanapiga kiswahili mwanzo mwisho, kuhusu FM redio zingine ni kuchanganya lugha. Unategemea tutakuwa na kiswahili kizuri? Viongozi wakisimama wanakandamiza kingereza na kiswahili hapohapo, unategemea nini kwenye taifa? Kijana hacha kukosoa toa suluhisho la nini kifanyike.
Hacha ilipaswa iwe acha.
Naona na wewe umeingia kwenye kundi la kulaumu bila kutoa suluhisho.
Suluhisho la kukifanya kiswahili kipendwe na kikubalike zaidi ni pamoja na kuzingatia mambo yafuatayo:-
1. Viongozi wa kitaifa watumie kiswahili katika hotuba zao zote bila kuchanganya na lugha nyingine.
2. Katika vituo vya redio na luninga waajiriwe watangazaji wanaokifahamu vizuri kiswahili na waepuke kuchanganya na lugha nyingine wakati wa matangazo.
3. Kuwe na mashindano ya uandishi wa insha za kiswahili na pia kuwe na mashindano ya midahalo ya kiswahili.
4. Serikali na hasa kupitia baraza la sanaa Tanzania iwatumie watu mashuhuri na watu maarufu kukitangaza kiswahili ndani na nje ya nchi.