Mlenge
R I P
- Oct 31, 2006
- 2,125
- 2,306
Nianze na kusema, nina shitariki ya mawazo ya udogo wa serikali (small Government), na, haki na wajibu kwa mtu binafsi (individual rights and responsibility); mawazo yanayoweza kujumuishwa kwa dhana ya Ruksa (Liberty).
Tuje kwenye mada.
Suala la mikopo ya elimu ya juu ni suala tete na mtambuka. Kwa baadhi ya waombaji, kukubaliwa kupata mkopo au kutokubaliwa kunamaanisha kupata elimu ya juu au kukosa. Hivyo basi, jitihada zimekuwa zikifanyika kuhakikisha kila mwombaji mkopo elimu ya juu anapata mkopo huo. Dhumuni la mada hii ni kuainisha njia mbadala za kufikia lengo hilohilo la mkopo wa elimu ya juu kwa kila mwombaji.
Mbadala wa Kwanza
Serikali ndio mwenye wajibu wa kuhakikisha kila anayetaka kwenda elimu ya juu anawezeshwa kifedha kwenda kusoma. Vyombo vya serikali ndivyo vyenye dhamana ya kukopesha. Navyo vinaweka masharti ya nani astahili kupata mkopo au kukosa. Wale wanaokosa, baadhi hutoa lawama kwa serikali. Rasilmali fedha zisingekuwa changamoto, kila mwombaji angepata kadiri anavyotaka. Huu mbadala ndio kwa kiasi kikubwa hali halisi ilivyo sasa. Mbadala huu unaegemea shitariki ya mawazo ya Ujamaa (socialism) kwa kuchukua hela kwa watu wengine (walipakodi) na kuzigawa, ngaa kwa mkopo, kwa watu wengine (waomba mkopo).
Mbadala wa Pili
Mbadala huu ni wa kubadili kidogo Mbadala wa kwanza. Waombaji mkopo wanawekwa kwenye mafungu, tuseme, manne.
(a) Fungu la kwanza la wasiohitaji mkopo kabisa. Vyuo vingekaribishwa kudahili wanafunzi walio na uwezo wa kujilipia kwa 100%. Nafasi, tuseme, asilimia 60 ya nafasi ziliopo zinatengwa kwa ajili hii.
(b) Fungu la pili la wanaohitaji mkopo kiasi, tuseme, kuanzia 0.1% mpaka 49% ya gharama za elimu ya juu. Hawa, tuseme wanatengewa asilimia 20 ya nafasi zilizopo. Awamu yao ya udahili inafuata baada ya ile ya kwanza.
(c) Fungu la tatu la wanaohitaji mkopo mwingi, kuanzia 50% ya gharama mpaka 75%. Hawa tuseme wanatengewa asilimia 10 ya nafasi zilizopo, na wanapewa fursa ya tatu ya udahili.
(d) Fungu la nne ni la wanaotaka mkopo 100% ya gharama au pungufu kidogo. Hawa wanapewa fursa ya mwisho kudahiliwa, na wanagombea nafasi zilizobaki.
Kila mwombaji kwenye awamu moja, hapati fursa ya kuomba mkopo awamu nyingine.
Mbadala wa Tatu
Katika mbadala huu, serikali inajitoa kwenye biashara ya kutoa mikopo ya elimu ya juu. Kila mwananchi anapewa wajibu wa kujigharamia elimu ya juu, na haki ya kuchagua mkopeshaji mwenye masharti anayoyaweza.
Serikali inatunga tu sera kuhusu masharti yanayoweza kutolewa, mathalan, mintarafu:
1. Muda wa mkopo
2. Kiwango cha riba
3. Masharti ya makato
4. Ukomo wa mkopo (e.g., nini kitatokea iwapo mkopaji atafariki au atatangaza kufilisika)
5. Mahitaji ya dhamana ya mkopo
6. Utaratibu wa kuzisarifu pesa za mkopo.
7. n.k.
Kwa njia hiyo, kila mhitaji wa mkopo wa elimu ya juu atajichagulia mkopeshaji, na kiwango cha kukopa, kadiri atakavyoona vema. Serikali itakuwa na jukumu la kutunga sheria za mchezo, huku refarii akiwa ni soko huria.
Serikali inaweza kuzihamasisha taasisi za kukopesha kwa kuziongezea mtaji au isifanye hivyo.
Katika mibadala hii mitatu, mbadala huu utakuwa ndio maridhawa zaidi kwani utakuwa unaiacha serikali ifanye kile inachofanya vizuri zaidi: kutunga sera, na kuachia sekta binafsi ifanye kile inachofanya vizuri zaidi: kufanya biashara; na mwisho wa yote kumwachia mwananchi fursa ya kufanya maamuzi binafsi.
Nawasilisha.
Tuje kwenye mada.
Suala la mikopo ya elimu ya juu ni suala tete na mtambuka. Kwa baadhi ya waombaji, kukubaliwa kupata mkopo au kutokubaliwa kunamaanisha kupata elimu ya juu au kukosa. Hivyo basi, jitihada zimekuwa zikifanyika kuhakikisha kila mwombaji mkopo elimu ya juu anapata mkopo huo. Dhumuni la mada hii ni kuainisha njia mbadala za kufikia lengo hilohilo la mkopo wa elimu ya juu kwa kila mwombaji.
Mbadala wa Kwanza
Serikali ndio mwenye wajibu wa kuhakikisha kila anayetaka kwenda elimu ya juu anawezeshwa kifedha kwenda kusoma. Vyombo vya serikali ndivyo vyenye dhamana ya kukopesha. Navyo vinaweka masharti ya nani astahili kupata mkopo au kukosa. Wale wanaokosa, baadhi hutoa lawama kwa serikali. Rasilmali fedha zisingekuwa changamoto, kila mwombaji angepata kadiri anavyotaka. Huu mbadala ndio kwa kiasi kikubwa hali halisi ilivyo sasa. Mbadala huu unaegemea shitariki ya mawazo ya Ujamaa (socialism) kwa kuchukua hela kwa watu wengine (walipakodi) na kuzigawa, ngaa kwa mkopo, kwa watu wengine (waomba mkopo).
Mbadala wa Pili
Mbadala huu ni wa kubadili kidogo Mbadala wa kwanza. Waombaji mkopo wanawekwa kwenye mafungu, tuseme, manne.
(a) Fungu la kwanza la wasiohitaji mkopo kabisa. Vyuo vingekaribishwa kudahili wanafunzi walio na uwezo wa kujilipia kwa 100%. Nafasi, tuseme, asilimia 60 ya nafasi ziliopo zinatengwa kwa ajili hii.
(b) Fungu la pili la wanaohitaji mkopo kiasi, tuseme, kuanzia 0.1% mpaka 49% ya gharama za elimu ya juu. Hawa, tuseme wanatengewa asilimia 20 ya nafasi zilizopo. Awamu yao ya udahili inafuata baada ya ile ya kwanza.
(c) Fungu la tatu la wanaohitaji mkopo mwingi, kuanzia 50% ya gharama mpaka 75%. Hawa tuseme wanatengewa asilimia 10 ya nafasi zilizopo, na wanapewa fursa ya tatu ya udahili.
(d) Fungu la nne ni la wanaotaka mkopo 100% ya gharama au pungufu kidogo. Hawa wanapewa fursa ya mwisho kudahiliwa, na wanagombea nafasi zilizobaki.
Kila mwombaji kwenye awamu moja, hapati fursa ya kuomba mkopo awamu nyingine.
Mbadala wa Tatu
Katika mbadala huu, serikali inajitoa kwenye biashara ya kutoa mikopo ya elimu ya juu. Kila mwananchi anapewa wajibu wa kujigharamia elimu ya juu, na haki ya kuchagua mkopeshaji mwenye masharti anayoyaweza.
Serikali inatunga tu sera kuhusu masharti yanayoweza kutolewa, mathalan, mintarafu:
1. Muda wa mkopo
2. Kiwango cha riba
3. Masharti ya makato
4. Ukomo wa mkopo (e.g., nini kitatokea iwapo mkopaji atafariki au atatangaza kufilisika)
5. Mahitaji ya dhamana ya mkopo
6. Utaratibu wa kuzisarifu pesa za mkopo.
7. n.k.
Kwa njia hiyo, kila mhitaji wa mkopo wa elimu ya juu atajichagulia mkopeshaji, na kiwango cha kukopa, kadiri atakavyoona vema. Serikali itakuwa na jukumu la kutunga sheria za mchezo, huku refarii akiwa ni soko huria.
Serikali inaweza kuzihamasisha taasisi za kukopesha kwa kuziongezea mtaji au isifanye hivyo.
Katika mibadala hii mitatu, mbadala huu utakuwa ndio maridhawa zaidi kwani utakuwa unaiacha serikali ifanye kile inachofanya vizuri zaidi: kutunga sera, na kuachia sekta binafsi ifanye kile inachofanya vizuri zaidi: kufanya biashara; na mwisho wa yote kumwachia mwananchi fursa ya kufanya maamuzi binafsi.
Nawasilisha.