Mkubwa Fella:Juma Nature amekosa kampani yangu ndio maana ‘anafeli’

kirerenya

JF-Expert Member
Joined
Aug 27, 2013
Posts
1,696
Reaction score
2,253

Mkurugenzi wa Yamoto Band na TMK Wanaume Family, Mkubwa Fella amedai Juma Nature anashindwa kufanya vizuri kwenye muziki kutokana na kukosa huduma yake.

Meneja huyo amedai yeye alikuwa anajua njia za kupita kumpromote muimbaji huyo na kuhakikisha kazi zake zinafika kwa wananchi.

“Juma Nature muziki wake haujapungukiwa chochote, yule kapungukiwa kampani yangu. Kwa sababu alichokuwa anafanya ni kile kile, ila kwa sasa amekosa kampani yangu,” alisema Mkubwa Fella. “Mimi naweza kuongea na mwenye redio vizuri, mimi naweza kuongeza na Dj vizuri. Juma Nature anaimba vizuri pia ni mtunzi mzuri kwahiyo mimi nachoweza kusema kwa Nature ni hilo,”

Fella alisema yupo tayari kufanya tena kazi na Juma Nature lakini Nature ameonekana kutokuwa tayari kufanya tena kazi na meneja wake huyo wa zamani.

Nyimbo nyingi za Juma Nature za hivi karibuni zimeshindwa kufanya vizuri.


Chanzo: Bongo5
 

Nature ndio kamuingiza fela kwenye mziki ..fela kama añaona anaweza kufanya kitu na nature ni bora wakayazungumza kiutu uzima kuliko kupayuka payuka ..huko ni kumkosea adabu mtu aliyemuonyesha njia
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…