Mkubwa Fella kustaafu, kumwachia Temba Yamoto Band

chinchilla coat

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2016
Posts
5,107
Reaction score
10,969
Mkurugenzi wa Mkubwa na Wanae Foundation pamoja na Yamoto Band, Mkubwa Fella amesema tayari ameshampata mtu sahihi ambaye atamwachia mikoba yake ya kusimamia wasanii pale atakapostaafu.
“Kusema kweli mtu ambaye nitamwachia kijiti ni Temba, tayari imeshamuandaa vya kutosha na bado naendelea, kwa hiyo Temba tayari anaelewa nini anatakiwa kufanya muda ukifika,” alisema Fella.

Kwa upande wa Temba amesema yupo tayari kupokea majukumu atayoachiwa na bossi wake huyo.

“Mimi nipo poa tu, tayari nimeshazungumza naye kuhusu ili swala na naamini kila kitu kitaenda sawa,” alisema Temba.

Pia Temba alisema hata kama akiwa kwenye jukumu la umeneja hataacha kufanya muziki kwa kuwa muziki ni sehemu ya maisha yake.
 
Kama kati ya wote waliomzunguka kaona Temba ndio afadhali basi, sasa atafanyeje?
 
Ila kwa Mondi alitemwa ka bigG
 
temba ulevi na bangi kwa sana mashushushu tunajua mengi[emoji17] [emoji17] [emoji17] [emoji17] [emoji18] [emoji18]
Kimoja ni tiba na kingine ni mapato..nikajua anapenda pia kufyatua..hii sio nzuri sana
 
HONGERENI SANA KWA KUWA NA SUCCESSION PLAN AMBAYO INAKUBALIKA. Mkubwa Fela simfahamu wala sijawahi kuonana naye ila ni kijana ambaye ana vision na discipiline. kwa watu wa aina hii hufanikiwa hata wakiuza mkaa
 
HONGERENI SANA KWA KUWA NA SUCCESSION PLAN AMBAYO INAKUBALIKA. Mkubwa Fela simfahamu wala sijawahi kuonana naye ila ni kijana ambaye ana vision na discipiline. kwa watu wa aina hii hufanikiwa hata wakiuza mkaa
Jamaa yuko poa sana, anasemwa vibaya lakini hajibu shombo, ndio maturity hiyo, amabayo hata jamaa yetu hana
 
Roma mkatoliki anajua kuona mbali .. boss kaikacha TpTop kamganda Dangote..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…