Mkude akaribia kutua Yanga

Ila umesikia au kusoma mchezaji katika nchi hizo anazima simu ili viongozi wasimpate?Kama mchezaji una haki ya kukataa kusaini ili kupata maslahi zaidi au kuondoka hiyo ni haki yako ya kimsingi. Ila huwezi kusikia mchezaji mkataba haujaisha anasema naenda timu fulani. Kwa sababu Tanzania sheria zinazotawala mpira hazifuatwi ndio unaona viongozi na wachezaji wanafanya wanavyotaka .Mchezaji yupo kwenye mkataba haheshimu mkataba .Anajua wazi kwamba uamuzi wa suala lake utapigwa danadana. Mfano suala la Kessy,Simba waliambiwa walete risiti za mshahara wake wa miezi 3 ya mwisho wa mkataba.Wamepeleka hakuna uamuzi.Utasikia kutaneni muamuwe wenyewe.Mohamed Mkopi amesign Mbeya Stars huyu akiwa na mkataba na Prisons kafungiwa mwaka 1.Hamna cha kutaneni mpate muafaka. Sheria zifuatwe viongozi na wachezaji itabidi nao wafuate sheria watakapoona hamna longolongo.
 
Ndiyo ujinga wa kukuza vitimu vya watoto klabuni,, unahangaika kuvihudumia kwa muda mrefu na kurisk ktk mechi muhimu kwa kuvipa nafasi ili vicheze na kupata uzoefu baadaye wakisha pata uzoefu wanaanza maneno Mbofu mbofu.

Aende tu Yanga akacheze huko pale atakuja mwingine Simba haijahi kufanya makosa ktk usajili wa kiungo toka Enzi za Nico Njohole,, Gaga,, Renny ,, Michael Paul nk.
 
Ndio viongozi wa soka wa kibongo hao

Ila wachezaji nao wana shida kidogo
 
Sio mbaya akienda, yanga naona inakuwa simba B sasa kuanzia kwa Barthez, kessy, mkude na tambwe, hapo tayari idara zote covered. Kipa, beki, kiungo na straika.
Simba imeishakuwa feeder club!
Inazalisha wachezaji ili timu kubwa ziwachukue!
 
Hans pope anazungumza kama sio kiongozi mkubwa wa klabu na mdau wa soka letu.Ni kama vile anasema mkude hatakiwi kudaihaki kwakuwa ni mchezaji wa kitanzania.Hii ni kasumba mbaya sana isiyoheshimu mchango wa mchezaji kwenye timu.

Hakuna ubishi wowote juu ya mchango wa Mkude simba.Kuna magarasa kama Blagnon utakuta yanalipwa mapesa mengi eti kisa ni wa kutoka nje.Ujinga kabisa

Hata kama hawataki kulipa pesa zaidi basi kuna lugha za kuongea ukiwa kama kiongozi wa klabu.Sema tu mkude ni mchezaji mzuri na anastahili kupatiwa maslahi bora na klabu lakini kwa sasa tutaendelea kufanya nae mazungumzo tukiafikiana tutakuwa nae tukishindwana yupo huru kwenda sehemu atakayoona inamfaa zaidi...mchango wake tunauthamini sana kwa kupindi ambacho anekuwa nasi.Huu ndo weledi wenyewe

By the way shafii dauda ni reporter ea goal.com hapa bongo?
 
Viongozi wa mpira bongo bwana-'Eti kwa vile Mkude ni mchezaji ambaye tumemkuza wenyewe na tumekabidhi majuku, lakini anajifanya amekuwa na wakati hata asipokuwepo kwenye timu hatupati madhara yoyote,”amesema Hans Poppe.
Hivi hastahili hicho anachotaka? kama mchango wake kwenye time ni kawaida , jee wamefungwa mabao mangapi kutokana na uzembe wake? Kwa mbali naona yale ya tambwe yanajirudia. Kwa mwendo huu, naona yale ya kesi yanajirudia na simba isitarajie mengi kwani kama mnaona hao wachezaji wa nje ndiyo wazuri basi mfahamu kuwa mnatengenze matatizo ndani ya time na kwa mwendo huu, ubingwa itakuwa vigumu sana.
 
Jibu muafaka kabisa. Simba sasa ni feeder club. Inatengeneza wachezaji ili waende club kubwa. Hilo sasa halina mjadala.
 
Misaada itapungua akianza kulipa deni la bilioni 13 au mali ziuzwe. Isije ikawa deni analowadai la bilioni 11 likafufuka. Mtaanza kupitisha bakuli kama enzi za Mzee Matunda. Mlichanga mpaka maharage leo mmesahau. Pesa za sponsor zitakatika soon.
 
Unajua Mkude amefanya ujinga sana kuexpose mambo ya klub nje.Ukweli mchango wake umepungua sana,nafikiri ushawishi mwingi unamponza.Anapenda kuridisha mipira langoni mwake sijui kwanini.Mwacheni aende akazeekee huko maana atakua amezika nafasi yake.
 
Sio mbaya akienda, yanga naona inakuwa simba B sasa kuanzia kwa Barthez, kessy, mkude na tambwe, hapo tayari idara zote covered. Kipa, beki, kiungo na straika.
Mkude anataka walau passport yake igongwe muhuri. Toka aipate haijawahi gongwa muhuri!
 
Mkodisho fc.. kila mchezaji mzuri wa Simba wanamtaka

Safari hii kwa mkude hamuwezi nyinyi Simba B



Endeleeni kuamini kuwa Yanga SC ni simba B wakati klabu yako hiyo hiyo imetoka ubavuni mwa Dar es Salaam Young Africans SC..
 
Endeleeni kujisifia kuwa makini kusajili viungo ikiwa Safu ya Ushambulizi na Ulinzi iko hoi...

Wakati wenzenu wanaimarisha safu yao ya Kiungo..


 
Yanga iachane na huyo mamluki wa Simba


Usimuite Mamluki....


Tungemuita Tambwe kuwa ni mamluki ingekuwaje hivi sasa...?


Tungemuita Yondani ni mamluki ingekuwaje sasa....?

Wachezaji wengi wa simba wana ndoto za kuitumikia Yanga SC kwa sababu ni klabu pekee hapa TZ inayoweza kuwapa Mafanikio.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…