LGE2024 Mkurugenzi Kigoma akiri uwepo wa kura 'feki'

LGE2024 Mkurugenzi Kigoma akiri uwepo wa kura 'feki'

Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024

Suley2019

JF-Expert Member
Joined
Oct 7, 2019
Posts
2,203
Reaction score
5,610

Wakati Novemba 27, 2024 ikiwa ni zoezi la kupiga kura kwa ajili ya kuchagua viongozi wa serikali za mitaa, mkoani Kigoma tangu asubuhi kumeshuhudiwa malalamiko ya uwepo wa kura feki licha ya wimbi la wananchi kuonekana kujitokeza kupiga kura.

Hali hii imeshuhudiwa katika maeneo ya Mwandiga, ya Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma ambako mgombea wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) amekamatwa na kura feki 800. Katika Manispaa ya Kigoma Ujiji mkoani humo, kituo cha Masanga Stendi, baadhi ya wanawake wamekamatwa na kura feki wakiwa wanaingia nazo kituoni. Halikadhalika malalamiko yameshuhudiwa katika vituo vya Kamara, Bangwe, Kibirizi na maeneo mengine.

Kutokana na hayo, Jambo Tv tumemtafuta Mkurugenzi wa Manispaa ya Kigoma Ujiji ambaye pia ni Msimamizi wa Uchaguzi katika eneo hilo Kisena Mabuba ambapo amethibitisha kuwepo kwa kura hizo feki.

"Zoezi linakwenda vizuri. Kuna uwepo wa kura feki ambazo hazifanani na za kwetu, na tayari tumeshachukua hatua, tayari kuna mtu mmoja tunamshikilia", ameeleza.

PIA SOMA
- LGE2024 - Kigoma: Kura feki zakamatwa Mwandiga
 
Tunapofunga vituo vya kupiga kura kwenye uchaguzi wa Serikali za Mitaa, Taifa limeendelea kushuhudia tena ubaradhuli wa wazi na wa aibu toka kwa mamlaka zote za Serikali kushirikiana kuipatia CCM na wagombea wake ushindi wa aibu hata kwa gharama za maisha ya Watanzania.

Tunalaani mauaji na kujeruhiwa kwa wagombea, viongozi na wanachama wetu mbalimbali wakiwemo:

1) Steven Chalamila wa Jimbo la Tunduma aliyevamiwa na kukatwakatwa mapanga kikatili hadi umauti kumkuta.
2) Modestus Timbisimilwa, Mgombea nafasi ya Ujumbe wa Serikali ya Mtaa wa Ulongoni A, Kata ya Gongolamboto, Jimbo la Ukonga, Dar es Salaam aliyeuwawa na askari kwa kupigwa risasi wakati wa purukushani za kuzuia kura bandia na batili kuingizwa kituo cha kupiga kura.
3)George Juma Mohammed wa Kitongoji cha Stand Kata ya Mkwese Jimbo la Manyoni Mkoani Singida aliyevamiwa nyumbani kwake na watu waliofahamika kuwa askari na kumpiga risasi iliyomsababishia umauti.

Aidha, tuna taarifa kadhaa za kujeruhiwa na kukamatwa na Polisi viongozi, wagombea, wanachama na wapenzi wetu maeneo mbalimbali ya nchi walipokuwa wakijitahidi kukamata na kuzuia kuingizwa vituoni kura bandia na batili zilizopigwa tayari kuwabeba wagombea wa CCM.

Tunataka watu wetu hawa waachiwe haraka na bila masharti yeyote.

Tunaendelea kuwasiliana na Chama kitatoa tamko rasmi zoezi hili likikamilika.

Tunaamini kinachofanyika kina maagizo na baraka zote za @SuluhuSamia na Serikali yake na au nchi iko kwenye "autopilot" na yeyote katika eneo lake ana mamlaka ya kunajisi uchaguzi anavyotaka kwani tayari wamepewa kinga na Kanuni ya 49 ya Kanuni za Uchaguzi wa Viongozi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa, Ngazi ya Vijiji, Vitongoji na Mitaa inayosema, nanukuu:

"Msimamizi wa Uchaguzi, Msimamizi Msaidizi wa Uchaguzi, Msimamizi wa Kituo, Wajumbe wa Kamati ya Rufani au mtumishi yeyote wa Umma aliyehusika na usimamizi wa uchaguzi hatowajibika kwa Jinai au Madai au kuchukuliwa kwa hatua za kinidhamu au za kiutawala kwa jambo lolote alilolifanya au kuacha kulifanya kwa nia njema wakati wa kutekeleza majukumu yake chini ya Kanuni hizi". Mwisho wa kunukuu.

Hakika Taifa lina Msiba mwingine!!
 
Samia na mkwe wake wameamua kunajisi uchaguzi licha ya kujitia uchamungu fake kumbe ni ushetani mtupu
 
Kama uchaguzi wa serikali za mitaa mambo yapo hivi.. mwakani itakuwaje?
Fisiem ni wazi na walafi, kwakua tayari walishafanya udhalimu wakaengua wapinzani wanabakia wao kwa 100% na wapinzani walibakia kitu kama 20% wanao shindana na 100% ya fisiem kwakua wao hakuna aliye enguliwa. Kwahiyo wana uhakika wa ushindi wa kuanzia 80% kwakua hizo hawana mshindani, lakini kwa kuwa ni walafi na wariho wa madaraka, hata hizo 20% wanazo gombea pamoja na upinzani bado wanaiba kura, kwa mtindo huu usitarajiemaendeleo kwakua viongozi wetu wanatokana na wizi kwahiyo wataendelea na kuiba kwakua ndio mfumo ulio waweka madarakani
 

Wakati Novemba 27, 2024 ikiwa ni zoezi la kupiga kura kwa ajili ya kuchagua viongozi wa serikali za mitaa, mkoani Kigoma tangu asubuhi kumeshuhudiwa malalamiko ya uwepo wa kura feki licha ya wimbi la wananchi kuonekana kujitokeza kupiga kura.

Hali hii imeshuhudiwa katika maeneo ya Mwandiga, ya Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma ambako mgombea wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) amekamatwa na kura feki 800. Katika Manispaa ya Kigoma Ujiji mkoani humo, kituo cha Masanga Stendi, baadhi ya wanawake wamekamatwa na kura feki wakiwa wanaingia nazo kituoni. Halikadhalika malalamiko yameshuhudiwa katika vituo vya Kamara, Bangwe, Kibirizi na maeneo mengine.

Kutokana na hayo, Jambo Tv tumemtafuta Mkurugenzi wa Manispaa ya Kigoma Ujiji ambaye pia ni Msimamizi wa Uchaguzi katika eneo hilo Kisena Mabuba ambapo amethibitisha kuwepo kwa kura hizo feki.

"Zoezi linakwenda vizuri. Kuna uwepo wa kura feki ambazo hazifanani na za kwetu, na tayari tumeshachukua hatua, tayari kuna mtu mmoja tunamshikilia", ameeleza.

PIA SOMA
- LGE2024 - Kigoma: Kura feki zakamatwa Mwandiga
Ndugu zangu nchi hii sasa tumebakia na kete mbili zilizo kuu ili tuondokane na vitisho na uongozi wa kidhalimu wa CCM chini ya SAMIA Suluhu Hassan ,kete ya kwanza ni ss wananchi kuamua kuandamana nchi nzima non stop kujitetea wenyewe dhidi ya mateso ya kutekwa na kuuawa kwa ndugu zetu mbalimbali.Kete ya pili ni JESHI la WANANCHI wa TANZANIA kama linavyofahamika kuchukua mamlaka kwa niaba ya wananchi kama kweli jeshi hili ni lao na liko kwa ajili ya wananchi.Mauaji yanayoendelea sasa naamin ni zaidi ya awamu zote zilizowahi kupita kuongoza Taifa hili.Kete hz mbili yoyote inaweza kuanza bila kusubiri nyingine kwa lengo la kuponya Taifa.Anayeshabikia watu kutekwa ,kuteswa na kuuawa ni kwa sababu hana upendo na uzalendo kwa watanzania wenzake.Majeshi ya wananchi kama ya Burkina faso,Mali na kwingineko yalipoona siasa chafu zinazonuka kama mavi zikiendeshwa ndani ya nchi zao majeshi hayo yaliingilia Kati ya kuwafurusha wanasiasa washenzi na wapumbavu wasio na Akili wanaohujumu nchi zao.JESHI letu linasemwa na kusifiwa kuwa lina weledi,nidhamu na maadili ya hali ya juu kabisa,Sasa SWALI la msingi linawezaje kuwa na sifa zote hizo Alafu linavumilia wananchi wake wakiteseka,je sifa hizi kea jeshi letu ni za kweli?.Kama nchi ni lazm tuache usanii na tujitafakari kwa kina na mapana.
 
Fisiem ni wazi na walafi, kwakua tayari walishafanya udhalimu wakaengua wapinzani wanabakia wao kwa 100% na wapinzani walibakia kitu kama 20% wanao shindana na 100% ya fisiem kwakua wao hakuna aliye enguliwa. Kwahiyo wana uhakika wa ushindi wa kuanzia 80% kwakua hizo hawana mshindani, lakini kwa kuwa ni walafi na wariho wa madaraka, hata hizo 20% wanazo gombea pamoja na upinzani bado wanaiba kura, kwa mtindo huu usitarajiemaendeleo kwakua viongozi wetu wanatokana na wizi kwahiyo wataendelea na kuiba kwakua ndio mfumo ulio waweka madarakani
 
Back
Top Bottom