mkurugenzi kilosa,unatarifa hii?

kajaga88

JF-Expert Member
Joined
Jul 7, 2013
Posts
228
Reaction score
31
ndugu wana jamvi,mimi ni mwalimu,idara ya sekondari wilaya kilosa.nina miaka minne kazini,na tayari nahesabu mwaka wa tano.kitu cha ajabu,wote tulioanza kazi mwaka 2009,hakuna mwalimu hata mmoja alopandishwa daraja.wakati wilaya nyingine,wote wamepanda madaraja.mfano.kilombero,mvomero,kongwa dodoma.kwann kilosa tu! katibu tsd ukimwendea,atakavokujibu,utajuta kwanini ulimwendea.mkurugenzi,na watendaji wako,fuatilianeni suala hili,zaidi ya hapo,wambie ukaguzi wilaya wasilete magari yao kuulizia scheme,lesson plan na mengineyo.nawakilisha
 

mpe muda huyo mkurugenzi ni mpya hapo Kilosa na pia mpya kwenye cheo cha ukurugenzi,alikuwa mtunza hazina Mufindi.
 
....kwa malalamiko na masononeko haya ya walimu,karibu wilaya nyingi huku Tanganyika(isomeke Tanzania bara) hiyo BIG RESULTS NOW kwenye sekta ya ELIMU,itatoka wapi?
 
Pole sana Mwalimu...niseme kwanza hauwakilishi bali unawasilisha. Mbili kwenye madai yako una haki ya kupandishwa daraja na haki siku zote haiombwi bali hudaiwa. Cha kufanya mjioganize walimu wote mlioanza kazi mwaka huo wa idara ya Msingi mpeleke madai yenu kwa mkurugenzi kwa maandishi na kama hamtapata ufumbuzi ndani ya miezi 3 andikeni barua kwa Katibu mkuu Wizara . Na kama bado kimya nendeni Mahakamani kwa kushirikisha chama cha walimu. Kugomea kukaguliwa maandalio, schemes, na zana za kufundishia hakutawasaidia kwa sababu zenyewe ni zana za upimaji. Kumbuka 'wajibu na haki'.
 
na wao wanahaki ya kutenda wajibu bila shuruti.pia jiografia ya kilosa,kwenda wilayani,kuna wa2 inatugarim zaid ya 22 elfu,oneway trip,hujala,hujalala.katibu tsd ndo hafai kabisa.na ikumbukwe,matokeo ya mwaka juz kdato cha nne,kilosa ilishika mkia ktk mkoa,badala ya kuangalia wiknes,wanaongeza matatzo.
 
Mkurugenzi na afisaelimu hasa sekondari huyu mpya hili linawagusa. Ebu pelekeni taarifa walimu wapandishwe na kuanza kupata stahiki zao maana hizo pesa hamtoi mifukoni mwenu, msikubali kupewa taarifa mbovu, kilosa sio mbaya wabayat ni viongozi wake hebu msiingie kwenye sifa hiyo. Tunataka kuona makucha yenu au na nyinyi ni walewale?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…