Mkurugenzi mkuu LATRA Habibu Suluo hizi namba zenu 0800 11 0019 na 0800 11 0020 hazina msaada, toa namba zako mwenyewe

Mkuu hoja yako ya kuzungumza na CPA kama unachangamoto au maoni ni wazo zuri lakini tambua kuna watenda kazi wengi chini yake ambao wanaweza kutatua changamoto yako kabla ya kufika kwa CPA Habibu suluo,
Kuhusu watoa huduma wa LATRA kukupa namba ya afisa wa mkoa husika ni kwaajiri ya kupata huduma kwa haraka na kwa wakati,
Mbona kwa changamoto hiyo ya nauli hao watoa huduma wametusaidia sana kurudishiwa nauli zetu hasa kwenye daladala na mabasi kwa kuzungumza na konda au suka wa gari husika, na wasipoonesha ushirikiano ndipo huduma kwa wateja hutoa namba ya afisa wa mkoa ili akusaidie changamoto yako
NB: kubeza utendaji kazi wa kiongozi kulingana na asili yake au wap anatokea wapi sio sawa
 
Pole sana kwa hiyo changamoto
Ila binafsi kuna nyakati mbili tofauti nimekutana na changamoto ya usafiri, nilipiga simu nikapokelewa vizuri, nikahudumiwa kwa ufasaha, na nikapewa backup ya msaada wa Namba za afsa wa LATRA aliyeko katika mkoa niliokuwa (Mwanza)

Na ilikuwa ni usiku, lakini tulisaidiwa kupata usafiri mwingine.
Inawezekana kwako hawakukidhi Mahitaji ila kwangu walihudumia na nikahisi umuhimu wa Namba zao kutolewa
 
Tanzania ni nchi moja yenye muunganiko wa bara na visiwani .
Na pande zote mbili zinawakilishwa na Taifa moja ambalo ni Tanzania
Tuweke hoja mezani ikiwa ni kutokutatuliwa kwa matatizo yako au ya Watanzania na sio kuleta ubaguzi wa kikanda.

Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania anafanya teuzi kwa kuzingatia utendaji kazi wa mtu husika na wala sio kwa kuzingatia kanda anayotokea

Nakushauri kwa masilahi mapana ya taifa letu, usijenge hoja ukihusianisha na ubaguzi wa kikanda, jenga hoja ukihusianisha na utekelezwaji pamoja na utatuzi wa changamoto zako binafsi au na wahusika unaowawakilisha
Sisi sote ni Watanzania tujenge hoja na sio kujenga ubaguzi kama hoja.
 
Kuna taboa

Mimi naona bora tuseme tu ukweli, hawa latra naona wanajitahidi sana ukilinganisha na kero zilizopo katika sekta, nimeshapiga simu mara kadhaa na kupokelewa na hatua zikachukuliwa, nimeona wameweka hadi namba zao za mikoani na za viongozi katika intagram story yao ya latra_tz na wanajibu hadi baadhi ya comments
 

Attachments

  • tempFileForShare_20240310-154345.jpg
    1.1 MB · Views: 2
Taboa Ni chama.cha wamiliki wa vyombo vya usafiri........sijaona chombo cha kutetea wasafiri
Ni Baraza la Ushauri la Watumiaji wa Huduma za usafiri Ardhini (LATRA CCC, ndo watetezi wa watumia huduma
 
Mimi binafsi nimepiga simu mara kadhaa na nimepata msaada mzuri sana, Kwa mara ya kwanza nilipiga kuuliza nauli ya kwenda dodoma nilijibiwa vizuri sana pia juzi nilimsafirisha mdogo wangu kwenda Tanga katika vitu nilivyompa ni pamoja na namba ya Latra japo kuwa hakupata shida yoyote njiani...kwa huduma nzuri kwa wateja Latra na Tanesco wanajitahidi sana,
Tuendelee kubishana mambo ya pacome na chama [emoji1]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…