Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania(TRA) ana mtihani mkubwa sana akifanikisha hili anastahili tuzo

Leverage

JF-Expert Member
Joined
Jan 25, 2021
Posts
2,125
Reaction score
3,150
Upande mmoja anatakiwa atumie akili na hekima kukusanya kukusanya kodi kwa maelekezo ya Rais.

Upande wa pili ni lengo la trilioni 2 kwa mwezi kwa maelekezo ya Makamu wa Rais.

My take:
Siku zote mfanyabiashara lengo lake ni kutengeneza faida kubwa hapa naongelea "Big potatoes" au wafanyabiashara wakubwa ambao kila kitu wakichuma Tanzania wanapeleka kwenye account zao Canada/Ulaya.

Wafanyabiashara wa jamii ya Asia ni wajanja sana na wengi wao hawana uchungu na nchi yetu maana sio RAIA hawana hata kiwanja cha 20*20 hapa kwetu. Bado kuna makampuni makubwa yanayodai kila mwaka yanaingiza hasara ila hayafungi biashara au kuacha kuchimba madini.

Bado kuna ujanja wa kubadili majina ya kampuni baada ya grace period ya kodi kuisha. Wafanya biashara ni wajanja mno. Muhindi anaingiza mzigo kutoka China anausambaza kwenye store zaidi ya tano kisha dukani anaweka kamzigo kadogo ukienda kumkadiria kodi anajikuta analipa laki 1 kwa mwezi sawa na mtumishi kwenye salary ya laki 7.

Ukiweza kutimiza malengo haya yote mawili kwa ukamilifu, kwangu mimi wewe utakuwa mkurugenzi bora Tanzania.

"KAZI IENDELEE"
 
Hujui ulisemalo, ksbb hufanyi biashara. Kwa sisi tuliopo kwenye hiyo sekta kipindi hiki imepitia kigumu sana. Elewa T.R.A hakuishia kwa wa Asia tu. Biashara za wazawa wengi tena wadogo zimefungwa. Ona kariakoo ilivyo sasa na miaka 10 nyuma. Hivi sasa unapata chumba cha biashara maeneo tu mazuri bila kutumia dalalali. Unajua maana yake?. Vyumba vingi viko tupu pale,watu wamefunga biashara. Wapo waliofirisiwa. Ndio unayataka hayo?.
Kibaya zaidi ile kariakoo ilitakiwa iwe kitivo cha biashara kwa nchi za DRC,Rwanda,Burundi,Malawi,Zambia,Mozambique. Lakini kinachofanyika sasa?. Nchi zote hizo wanafuata bidhaa zao Kampala Uganda,nchi ambayo haina bandari.
Unajua tatizo liko wapi hapo?. Bidhaa nzuri kariakoo hamna,eidha watu waliokuwa wanafuata hiyo bidhaa wamefunga biashara au wamefirisiwa. Pili bidhaa za kariakoo wenye bandari ni ghari kuliko Kampala wenye bidhaa zinazopitia bandarini kwetu.
Siku hizi ni kawaida kwa kariakoo kukosa baadhi ya bidhaa kabisa,tofauti kabisa na kipindi cha nyuma.
Walikuwa wanaingia kwenye account za watu. Hata kama una biashara yako umeamua kuhifadhi pesa bank labda kwa kidogo kidogo mpaka kufikia milioni 20,siku wakikuibukia unajua nini walikuwa wanafanya? Mosi ilikuwa lazima uingie kwenye makubariano nao,ukijifanya unajua taratibu ndio hapo unafunguliwa kesi za uhujumu uchumi. Na account inafungiwa kwanza.
Nenda pale tunduma mpaka wa Zambia na Tz. Wafanyabiashara wamehamia upande wa zambia. Unajua ipoje? Mamlaka za Zambia baada ya kunusa wafanyabiashara kunyanyasika na mamlaka za mapato Tz wakawakaribisha kufanyia biashara upande wa Zambia. Tumekimbiza wengi pale,tumekosa mapato mengi sana.
Mwisho ujue wapo walipata strock ksbb ya hawa jamaa,wapo walio maisha kabisa. Ndio unayataka hayo?
 
Shida nyie wafanya biashara mna ujanja mwingi sana,huwa hampendi kulipa kodi,mnapenda mpate faida tu,ndo maana hata zile mashine za EFD zilipokuja mlilalamika sana kwa kisingizio eti zinauzwa bei ya juu,bado hamkuweza kutoa list ya EFD zaid ya kutuandikia kwenye makaratasi, asilimia kubwa ya wafanya biashara wa Tanzania janja janja ni nyingi mno na ujuaji ni mwingi mno,mnapenda mpate faida tu pasipo kutoa kodi,mkibanwa kidogo tu kelele kibao,acheni ujanja lipeni kodi,mbona sisi wafanyakazi serikalini tunalipa kodi kubwa tu tena zaid ya mfanya biashara mkubwa!
 
TRA na task force zake wameua biashara nyingi ambazo hazikuwa zinakwepa kodi.
Walikuwa wana wanatumia vigezo gani kufanya audit kwa mahesabu waliyofunga wenyewe, hata miaka kumi nyuma? Wanatakiwa nao au waliofunga mahesabu Yenye kasoro, nao wawajibishwe
 
Kila mwezi unalipa kodi ambayo mfanyabiashara angekadiriwa yeye angeandamana kuwa ni kodi kandamizi! Hapo ukipandishiwa mshahara mwaka huu ndo inapanda maradufu.
 
Kama mfanyabiashara mjanja ndo umuonee?
Ndo umnyanyase?
Ndo imakdirie kodi inayozidi hata mtaji wake?
Ndo umuundie task force?
Ndo umwendee na bunduki kudai mapato?

We jamaa najua una ham ule ukatili wa baba yenu uendelee ili umuenzi.
Hii ni awamu ya sita. 6
Maagizo yanayofanyiwa kazi ni ya rais. Mapango hana mamlaka ya kumtumbua mteuliwa na rais.

Sent from my SM-A207F using JamiiForums mobile app
 
Nizingue nikuzingue.
 

Kamishna wa TRA
 
Kumbe hata hujui utaratibu wa kulipa kodi?!!nani alikwambia kuwa kodi inakadiriwa kutokana na mzigo ulio nao dukani?!!hahaaa?yaani mfanyabiashara kama muhindi ambaye ni mkusanyaji kodi ya ongezeko la thamani(VAT)akakadiliwe kodi dukani!!!??kwani mbona kama vile mmeumia sana kwa mheshimiwa kusema kuwa kodi sasa ikusanywe kwa stahaa?!!mataga BWANA!!!
 
Cheo chenyewe hicho ulichotaja hakipo. Tumekuelewa lakini tumia vyeo sahihi kulingana na taasisi husika
 
Hakika umesema kweli tuliopo kwenye biasharala ndio tunalijua joto la jiwe.
 
Mfano negotiation ikishindikana nini kifanyike?
 
Wengine mashine waliziharibu kwa makusudi ili kukwepa kulipa kodi. Kuna ukweli mchungu wanaukwepa hapa wanasingizia kuonewa.
 
Kodi inakadiriwa kutokana na mauzo, ila nyinyi wafanyabiashara mmechezea mashine janja janja nyingi
 
Sawa ngoja tuone
 
Mfano negotiation ikishindikana nini kifanyike?
Hapo ndio unakutana na zile kesi zilikuwa nyingi nyingi msimu huu. Money laundering. Na hapo unakuta kwenye account wameikuta milioni hata 16 tu,na kesi inaisha kwa wewe kunyang'anywa hiyo hela yote.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…