Mkurugenzi TBC: Uzushi huwachota watu wajinga, wakiambiwa mvuvi amepiga mlango wa ndege hadi ukafunguka wanaamini

BARD AI

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2018
Posts
3,591
Reaction score
8,826
Mkurugenzi wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC), Dkt. Ayoub Rioba amesema Habari za kizushi mara nyingi zinawachota watu wajinga ambapo amefafania kuwa ujinga si tusi lakini watu wajinga maana yake ni watu wasiokuwa na maarifa ya kutosha.

Akizungumza kutoka katika kongamano la kwanza la maendeleo ya sekta ya habari linalofanyika jijini Dar es Salaam Rioba amesema watu wajinga hata wakiambiwa mvuvi amepiga mlango wa ndege, mlango ukafunguka wanaamini.

#KongamanoHabari2022
 
Ila huyu jamaa kaisha kweli,namaanisha afya yake imezorota Sana,dizaini sijui sukari..Mungu amasaidie!
 
We ndio mzushi mkubwa na mwongo. Dr Ryoba hawezi kusema hayo maneno. Sababu inajulikana.
 
Yeye na TBC yake kuna nini cha maana wanafanya zaidi ya ujinga ujinga tu...
Sijawahi ona mkurugenzi wa hovyo km Ryoba hana sifa na hawezi kazi ya ukurugenzi aliwekwa na Magu sababu ya ukanda. Anachoweza ni ulevi na kubwabwaja sijui kwanini hawajamwondea mpaka Leo. TBC hakuna kitu haina mvuto wowote wala taarifa ya maana bora Channel Ten baba lao ITV. Aondolewe.
 
Nilikuwa naangalia LIVE mbona sijasikia hayo maneno uliyoandika hapa yanayohusu mvuvi kupiga mlango wa ndege

Kwanini usilete video inayothibitisha hayo maneno uliyoandika.
 
Ajira yake kaiweka kwenye samadi kwa kauli hii
 
Nilikuwa naangalia LIVE mbona sijasikia hayo maneno uliyoandika hapa yanayohusu mvuvi kupiga mlango wa ndege

Kwanini usilete video inayothibitisha hayo maneno uliyoandika.
We ndio mzushi mkubwa na mwongo. Dr Ryoba hawezi kusema hayo maneno. Sababu inajulikana.

Haya, huyu ni nani ?

Your browser is not able to display this video.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…