Mkurugenzi TEMEKE naye akamatwe na ahojiwe

Mkurugenzi TEMEKE naye akamatwe na ahojiwe

Joined
Mar 3, 2018
Posts
75
Reaction score
800
Mwananchi wangu wa Kakonko ambae,alikua ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Nyang'wale Ndugu yangu Carlos Gwamagobe ameswekwa Rumande kwa Wizi na wenzake 5.

Carlos namfahamu vizuri maana niliwahi kufanya nae Kazi Halmashauri ya Kakonko akiwa ni afsa Ustawi wa Jamii. Niliwahi kumwambia aache kula pesa za vikundi lakini sikuwahi kueleweka kwake. Labda kwasababu Mimi ni mpinzani. Sasa amepatikana.

ALIYEKUWA DED KAKONKO (Lusubilo Mwakabibi) NAE AKAMATWE.
Huyu Bwana nimekutana nae kwa Mara ya kwanza UDSM,akiwa anasoma PSPA mwaka wa pili wakati huohuo akiwa ana masters.

Baadae tuliagana akisema Rais wa awamu ya NNE amemtuma nje ya Nchi, na kweli aliondoka,aliniachia sabuni alizokua anatumia na ndoo zake pale mlimani.

Baada ya uchaguzi akachaguliwa kuwa Mkurugenzi Kakonko. Baada ya miezi 9 alikamatwa na kuletwa Rumande kwenye Gereza la Nyamisivya Kibondo kwa kosa la kuharibu Mali wakati huo huo Mimi pia nilikuwa gereza hilohilo kwa kesi za uchochezi. Nilimpa wembe zangu wakamnyoa kipara huku akiniambia kuwa Mkuu wa Wilaya ya Kakonko ndie amemzunguka jambo ambalo ni uongo.

Ameiba sana,lakini baada ya kujua ataingia hatiani wamemhamisha chini ya mwamvuli wa uchaguzi mdogo wa Buyungu! Sasa huyu mwizi mzoefu yupo Temeke. Ila hajahama kijinga,narudia tena hajahama kijinga!

Alishauliwa na wakubwa kwamba awatawanye watu anaodhani watamuumbua ama kwa ushiriki wao katika ulaji ama kwa kuwajibika kwao.

Alianza na Mwanasheria wetu wa Halmashauri,huyu alihama,akafuata Mkaguzi wa hesabu akahama,Akafuata Afsa utumishi,na baadae Mhasibu wa Halmashauri,Afsa Mipango na Mkurugenzi hawa wote wamehama ndani ya wiki mbili isipokuwa Mhasibu,Afsa Mipango na DED wao wameondoka siku moja.

Sasa hapa Kakonko tuna hoja za ukaguzi ambazo hazina majibu maana waliotakiwa kujibu wamehama.
Matokeo yake sisi tumekuwa Halmashauri ya kwanza kwa kukusanya mapato Kidogo . Tumekusanya Mil 347 chini ya lengo la Kukusanya Mil 700.

Moja ya wizi wa wazi wa huyu Mkurugenzi ni fedha za OC ya Desemba 2017 Tsh Mil 36 na mapointi kidogo hivi ambazo alizinywa waziwazi.

Sasa nimtakie kila la heri na wizi wake pale TEMEKE,sina shaka pale wajanja ni wengi.

Elia F Michael.
DED%2020181009_094847.jpg
 
Ccm bana wana watu wao wa kuwashughulikia kuna yule ngeleja alikubali kupokea pesa za wizi lakin hamna alichofanywa

Bila kumsahau mchonga dili mkubwa kuliko wote hapa Tanzania yule nyoka mwenye makengeza anakula bata bila wasiwasi wowote..
 
Mwananchi wangu wa Kakonko ambae,alikua ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Nyang'wale Ndugu yangu Carlos Gwamagobe ameswekwa Rumande kwa Wizi na wenzake 5.

Carlos namfahamu vizuri maana niliwahi kufanya nae Kazi Halmashauri ya Kakonko akiwa ni afsa Ustawi wa Jamii. Niliwahi kumwambia aache kula pesa za vikundi lakini sikuwahi kueleweka kwake. Labda kwasababu Mimi ni mpinzani. Sasa amepatikana.

ALIYEKUWA DED KAKONKO (Lusubilo Mwakabibi) NAE AKAMATWE.
Huyu Bwana nimekutana nae kwa Mara ya kwanza UDSM,akiwa anasoma PSPA mwaka wa pili wakati huohuo akiwa ana masters.

Baadae tuliagana akisema Rais wa awamu ya NNE amemtuma nje ya Nchi, na kweli aliondoka,aliniachia sabuni alizokua anatumia na ndoo zake pale mlimani.

Baada ya uchaguzi akachaguliwa kuwa Mkurugenzi Kakonko. Baada ya miezi 9 alikamatwa na kuletwa Rumande kwenye Gereza la Nyamisivya Kibondo kwa kosa la kuharibu Mali wakati huo huo Mimi pia nilikuwa gereza hilohilo kwa kesi za uchochezi. Nilimpa wembe zangu wakamnyoa kipara huku akiniambia kuwa Mkuu wa Wilaya ya Kakonko ndie amemzunguka jambo ambalo ni uongo.

Ameiba sana,lakini baada ya kujua ataingia hatiani wamemhamisha chini ya mwamvuli wa uchaguzi mdogo wa Buyungu! Sasa huyu mwizi mzoefu yupo Temeke. Ila hajahama kijinga,narudia tena hajahama kijinga!

Alishauliwa na wakubwa kwamba awatawanye watu anaodhani watamuumbua ama kwa ushiriki wao katika ulaji ama kwa kuwajibika kwao.

Alianza na Mwanasheria wetu wa Halmashauri,huyu alihama,akafuata Mkaguzi wa hesabu akahama,Akafuata Afsa utumishi,na baadae Mhasibu wa Halmashauri,Afsa Mipango na Mkurugenzi hawa wote wamehama ndani ya wiki mbili isipokuwa Mhasibu,Afsa Mipango na DED wao wameondoka siku moja.

Sasa hapa Kakonko tuna hoja za ukaguzi ambazo hazina majibu maana waliotakiwa kujibu wamehama.
Matokeo yake sisi tumekuwa Halmashauri ya kwanza kwa kukusanya mapato Kidogo . Tumekusanya Mil 347 chini ya lengo la Kukusanya Mil 700.

Moja ya wizi wa wazi wa huyu Mkurugenzi ni fedha za OC ya Desemba 2017 Tsh Mil 36 na mapointi kidogo hivi ambazo alizinywa waziwazi.

Sasa nimtakie kila la heri na wizi wake pale TEMEKE,sina shaka pale wajanja ni wengi.

Elia F Michael.View attachment 891474
Kuna hesabu ndefu hapo. Kisaikolojia mtumishi kama huyo yupo si kutumikia watu. Watu anawaibia. Anakwamisha maendeleo yao Yupo kumtumikia aliyemteua. Yupo kwa hisani. Madudu hayaangaliwi. Ana mission maalum anatekeleza au atatakiwa kuitekeleza baadaye. Chochote atakachoamriwa kufanya atafanya tu. Kila mtu atabaki kujiuliza anawezaje kufanya hayo kwa usomi wake na cheo chake! Anakumbuka alivyotakiwa lupango lakini yupo mtaani anakula bata. Mfadhili wake kwake ni mungu. Lazima atalipa fadhila jua kali au mvua ya eli ninyo. Wengi tuwaonao kujitoa fahamu ni sampuli hiyo. Ana godfather.
 
Daaahh hii inaitwa nilipue Bahati mbaya"... ......... by the way mkuu Jiandae kufuatwa na Nissan nyeupe
Kama dogo hajamjua huyu bwana vizuri, anyamaze tu.
Hawa kengele ni wale wanaotumwa kuharibu na ghafla anahamishwa au kutoweka na kuibukia idara ingine.

Kama amesoma nae na akaondoka kabla hajamaliza na akaibuki kiwa Ukurugenzi unashindwa nini kujiongeza.
 
Back
Top Bottom