Mkurugenzi wa Jamvi la Habari, Habibu Mchange, adaiwa kushikiliwa na TAKUKURU Kigamboni

Mkurugenzi wa Jamvi la Habari, Habibu Mchange, adaiwa kushikiliwa na TAKUKURU Kigamboni

upupu255

Senior Member
Joined
Sep 4, 2024
Posts
119
Reaction score
144
Habibu Mchange, Mkurugenzi Mtendaji wa magazeti Jamvi la Habari, Times Observer, Tanzania Bora na mengineyo amedaiwa kushikiliwa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Kigamboni kwa saa kadhaa.

Inadaiwa kuwa Mchange aliitwa TAKUKURU Ijumaa saa tatu asubuhi baada ya siku ya Alhamisi kukaa ofisini hapo hadi saa saba usiku.

1741957388948.jpeg

Tukio hili limejiri muda mfupi baada ya magazeti yake kuandika habari za taasisi hiyo kuwafungia ofisini viongozi wa CCM kata ya Tungi iliyopo wilaya ya Kigamboni.

Soma, Pia: Mambo yafichuka ndani ya Equity Bank, mmiliki wa gazeti la Jamvi la Habari alipewa tender na swahiba wake Zenda

Inaelezwa kuwa baada ya viongozi hao kufungiwa ofisini, Mchange na wanahabari wenzake walikimbilia eneo hilo na kusimamisha gari lao mita chache mbele ya ofisi na liliposimama gari la TAKUKURU, wakifuatilia kinachoendelea. Baada ya hapo maafisa hao waliwaamuru waongozane nao hadi ofisini kwao.

Jambo TV imepata kuwasiliana na afisa fulani ndani ya TAKUKURU Kigamboni ambaye ameeleza kutokuwa na mamlaka ya kulisemea jambo hilo, bali mwenye mamlaka hayo ni Mkuu wa TAKUKURU wilayani humo ambapo jitihada za kuwasiliana naye bado zinaendelea.

Chanzo: Jambo TV
 
Haya magazeti ni ya kichawa kama ya musiba au haya ya mchange yana muelekeo mwingine?
 
Habibu Mchange, Mkurugenzi Mtendaji wa magazeti Jamvi la Habari, Times Observer, Tanzania Bora na mengineyo amedaiwa kushikiliwa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Kigamboni kwa saa kadhaa.

Inadaiwa kuwa Mchange aliitwa TAKUKURU Ijumaa saa tatu asubuhi baada ya siku ya Alhamisi kukaa ofisini hapo hadi saa saba usiku.


Tukio hili limejiri muda mfupi baada ya magazeti yake kuandika habari za taasisi hiyo kuwafungia ofisini viongozi wa CCM kata ya Tungi iliyopo wilaya ya Kigamboni.

Soma, Pia: Mambo yafichuka ndani ya Equity Bank, mmiliki wa gazeti la Jamvi la Habari alipewa tender na swahiba wake Zenda

Inaelezwa kuwa baada ya viongozi hao kufungiwa ofisini, Mchange na wanahabari wenzake walikimbilia eneo hilo na kusimamisha gari lao mita chache mbele ya ofisi na liliposimama gari la TAKUKURU, wakifuatilia kinachoendelea. Baada ya hapo maafisa hao waliwaamuru waongozane nao hadi ofisini kwao.

Jambo TV imepata kuwasiliana na afisa fulani ndani ya TAKUKURU Kigamboni ambaye ameeleza kutokuwa na mamlaka ya kulisemea jambo hilo, bali mwenye mamlaka hayo ni Mkuu wa TAKUKURU wilayani humo ambapo jitihada za kuwasiliana naye bado zinaendelea.

Chanzo: Jambo TV
Habibu mchange nakukumbuka.
Ulipomaliza degree yako pale UDOM hukuwa na kitu kabisa. Chadema na wana kibaha wakakupokea. Ukapewa kugombea ubunge jimbo la kibaha mjini. Ukashinda kwa michango ya walala hoi.
Kaka aka KUHONGA . Ukauza jimbo
Yatakukuta mengi
 
Back
Top Bottom