Mkurugenzi wa JATU PLC aendelea kusota Gerezani kwa zaidi ya siku 690

Mkurugenzi wa JATU PLC aendelea kusota Gerezani kwa zaidi ya siku 690

Mtoa Taarifa

JF-Expert Member
Joined
Sep 21, 2024
Posts
213
Reaction score
671
Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Jatu PLC, Peter Gasaya (33), anayekabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi yenye mashitaka mawili likiwamo la kujipatia Sh5.1 bilioni kwa njia ya udanganyifu, amefikisha siku 690 akiwa gerezani kutokana na upelelezi wa shauri hilo kutokamilika.

Mbali na upelelezi kutokamilika, mshtakiwa huyo kupitia wakili wake, Nafikile Mwamboma ameiomba Mahakama hiyo imfutie kesi mteja wake na imuachie huru.

Gasaya anadaiwa kujipatia fedha hizo kutoka katika Saccos ya Jatu kwa madai kuwa fedha hizo atazipanda kwenye kilimo cha mazao ili kuzalisha faida zaidi, wakati akijua kuwa ni uongo.

Kwa mara ya kwanza, Gasaya alifikishwa mahakamani hapo Desemba 29, 2022 na kusomewa mashitaka yanayomkabili.

Hata hivyo, tangu afikishwe mahakamani hapo hadi leo Jumatatu Novemba 18, 2024 amefikishwa siku 690, sawa na mwaka mmoja, miezi 10 na siku 20 akiwa gerezani kutokana na upelelezi wa shauri hilo kutokukamilika.

Wakati mshtakiwa akifikisha siku hizo bila upelelezi kukamilika, upande wa mashitaka umedai kuwa bado unaendelea na upelelezi wa shauri hilo.
 
Atemeee hela hizo ndy wamuachiee lasivyoo akaeee tu huko,maana mnawapiga sana wajinga huku uraiani

Ova
Wabongo wanaona kukopa na kutokulipa, wizi wa kuaminiwa, kufilisi biashara za watu kama jambo la kawaida. Unakuta jitu linachezesha upatu kumbe majina yote ya kwake anawapata mahamuma anawaingiza chaka.
 
Hawa washenzi wanakula kweli hela za watanzania wajinga,ngoja abanwe mapumbu na ateme mkwanja wote pumbavu.
 
Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Jatu PLC, Peter Gasaya (33), anayekabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi yenye mashitaka mawili likiwamo la kujipatia Sh5.1 bilioni kwa njia ya udanganyifu, amefikisha siku 690 akiwa gerezani kutokana na upelelezi wa shauri hilo kutokamilika.

Mbali na upelelezi kutokamilika, mshtakiwa huyo kupitia wakili wake, Nafikile Mwamboma ameiomba Mahakama hiyo imfutie kesi mteja wake na imuachie huru.

Gasaya anadaiwa kujipatia fedha hizo kutoka katika Saccos ya Jatu kwa madai kuwa fedha hizo atazipanda kwenye kilimo cha mazao ili kuzalisha faida zaidi, wakati akijua kuwa ni uongo.

Kwa mara ya kwanza, Gasaya alifikishwa mahakamani hapo Desemba 29, 2022 na kusomewa mashitaka yanayomkabili.

Hata hivyo, tangu afikishwe mahakamani hapo hadi leo Jumatatu Novemba 18, 2024 amefikishwa siku 690, sawa na mwaka mmoja, miezi 10 na siku 20 akiwa gerezani kutokana na upelelezi wa shauri hilo kutokukamilika.

Wakati mshtakiwa akifikisha siku hizo bila upelelezi kukamilika, upande wa mashitaka umedai kuwa bado unaendelea na upelelezi wa shauri hilo.
Uwezo mdogo na ufinyu wa elimu unalikwaza jeshi katika upelelezi. Nchi ingesimamia sheria, angeshaachiwa, maana hamna ushahidi!
 
Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Jatu PLC, Peter Gasaya (33), anayekabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi yenye mashitaka mawili likiwamo la kujipatia Sh5.1 bilioni kwa njia ya udanganyifu, amefikisha siku 690 akiwa gerezani kutokana na upelelezi wa shauri hilo kutokamilika.

Mbali na upelelezi kutokamilika, mshtakiwa huyo kupitia wakili wake, Nafikile Mwamboma ameiomba Mahakama hiyo imfutie kesi mteja wake na imuachie huru.

Gasaya anadaiwa kujipatia fedha hizo kutoka katika Saccos ya Jatu kwa madai kuwa fedha hizo atazipanda kwenye kilimo cha mazao ili kuzalisha faida zaidi, wakati akijua kuwa ni uongo.

Kwa mara ya kwanza, Gasaya alifikishwa mahakamani hapo Desemba 29, 2022 na kusomewa mashitaka yanayomkabili.

Hata hivyo, tangu afikishwe mahakamani hapo hadi leo Jumatatu Novemba 18, 2024 amefikishwa siku 690, sawa na mwaka mmoja, miezi 10 na siku 20 akiwa gerezani kutokana na upelelezi wa shauri hilo kutokukamilika.

Wakati mshtakiwa akifikisha siku hizo bila upelelezi kukamilika, upande wa mashitaka umedai kuwa bado unaendelea na upelelezi wa shauri hilo.
atemee pesa ya watu hawa jamaa wamewatapeli wapenda mseleleko sana hadi eti wakaanza uza hisa DSE ama kweli tanzania kuna maajabu.
 
Nilikuwa kwenye group moja la whatsapp na vongozi fulani.. mambo ya jatu yalikuwa moto humo uzuri sikujiunga
Ile kitu ilikuwa imebaki kidogo nijiunge nao maana product zao zilikuwa sokoni, na kuingia DSE ndio ikawa inaonekana ni legitimate business.

1000016168.jpg
 
Ile kitu ilikuwa imebaki kidogo nijiunge nao maana product zao zilikuwa sokoni, na kuingia DSE ndio ikawa inaonekana ni legitimate business.

View attachment 3155454
Binafsi nimeanza kuingia na wasiwasi hata na UTT maana watu tunavyojazana huko ni balaa ..hata kama ni ya serikali, mara ngapi mifuko kama nssf, pspf n k hudidimizwa na serkali.
Nachoona huko utt badae pes yako lkn ukitaka uitoe masharti yatakuja kuwa kama ya kikokotoo
 
Kuna;
WACHEZESHA UPATU,
WACHANGISHA WATU HELA KWA MGONGO WA FOUNDATION MITANDAONI,
AGIZA CHINA,
WATU WA MADAWA ASILI/TIBA MBADALA,
.

Ni watu wa kuwachunga sana,vilio ni vingi sana mtaani.Serikali ichukue hatua protocols zifate ili jasho la mtu lisiondoke kizembe
 
Binafsi nimeanza kuingia na wasiwasi hata na UTT maana watu tunavyojazana huko ni balaa ..hata kama ni ya serikali, mara ngapi mifuko kama nssf, pspf n k hudidimizwa na serkali.
Nachoona huko utt badae pes yako lkn ukitaka uitoe masharti yatakuja kuwa kama ya kikokotoo
utt ni ngumu. serikali haiwezi kuchota hata sumni kule, na zaidi vigogo wamezika mabilioni kule.
 
Back
Top Bottom