Mindyou
JF-Expert Member
- Sep 2, 2024
- 1,869
- 4,877
Wakuu,
Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), Dkt. Irene Isaka, amesema mfuko huo unaendelea na mazungumzo na Hospitali ya Aga Khan ili kurejesha huduma za bima kwa wanachama wa NHIF katika kituo hicho jijini Dar es Salaam.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma kuhusu mafanikio ya NHIF katika miaka minne ya Serikali ya Awamu ya Sita, Dkt. Isaka alisema mazungumzo hayo yamefikia hatua nzuri.
Alifafanua kuwa sababu iliyosababisha Aga Khan kusitisha huduma za NHIF ni hospitali hiyo kujiona kuwa inatoa huduma za viwango vya juu ("high class"), hivyo haikuridhishwa na kiwango cha malipo kilichotolewa na NHIF kwa vifurushi vya bima.
"Kilichotokea ni kwamba wao wanasema huduma zao ni za viwango vya juu, na bei tunazowalipa ni ndogo, hivyo hawawezi kuendesha biashara," alisema Dkt. Isaka.
Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), Dkt. Irene Isaka, amesema mfuko huo unaendelea na mazungumzo na Hospitali ya Aga Khan ili kurejesha huduma za bima kwa wanachama wa NHIF katika kituo hicho jijini Dar es Salaam.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma kuhusu mafanikio ya NHIF katika miaka minne ya Serikali ya Awamu ya Sita, Dkt. Isaka alisema mazungumzo hayo yamefikia hatua nzuri.
Alifafanua kuwa sababu iliyosababisha Aga Khan kusitisha huduma za NHIF ni hospitali hiyo kujiona kuwa inatoa huduma za viwango vya juu ("high class"), hivyo haikuridhishwa na kiwango cha malipo kilichotolewa na NHIF kwa vifurushi vya bima.
"Kilichotokea ni kwamba wao wanasema huduma zao ni za viwango vya juu, na bei tunazowalipa ni ndogo, hivyo hawawezi kuendesha biashara," alisema Dkt. Isaka.