iamwangdamin
JF-Expert Member
- Feb 25, 2015
- 864
- 1,798
Tarehe 31 Julai 2024 kuanzia saa 5 asubuhi utafanyika mkutano baina ya Taasisi zinazoshughulika na tafiti za afya nchini Tanzania na Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Afya ya nchini Uingereza (National Institute for Health and Care Research (NIHR).
Mkutano huo umeandaliwa na Ubalozi wa Tanzania nchini Uingereza kwa madhumuni ya kuwezesha taasisi za Tanzania kupata ufahamu juu ya fursa za ushirikiano na ufadhili wa shughuli za utafiti katika sekta ya afya.
Mkutano huo unatarajiwa kuhudhuriwa na taasisi mbalimbali nchini ikiwemo taasisi ya @NIMR_Tanzania; @ifakarahealth, @muhimbiliuniver, @kcmucotz, @cuhas_bugando, @hkmuniversity, @MuhimbiliOrtho1, @TaasisiMoyoJKCI, @MuhimbiliTaifa, UDOM, Hospitali ya Benjamin Mkapa na Hospitali ya Rufaa ya Mbeya.
Mkutano huo utafanyika chini ya wenyeviti wenza Balozi wa Tanzania Nchini Uingereza Ndugu @MbelwaK na Mkurugenzi wa Afya wa NHRI Profesa Kara Hanson. Mganga Mkuu wa Serikali Prof. Tumaini Nagu atahudhuria Mkutano huo.
iamwangdamin
Mkutano huo umeandaliwa na Ubalozi wa Tanzania nchini Uingereza kwa madhumuni ya kuwezesha taasisi za Tanzania kupata ufahamu juu ya fursa za ushirikiano na ufadhili wa shughuli za utafiti katika sekta ya afya.
Mkutano huo unatarajiwa kuhudhuriwa na taasisi mbalimbali nchini ikiwemo taasisi ya @NIMR_Tanzania; @ifakarahealth, @muhimbiliuniver, @kcmucotz, @cuhas_bugando, @hkmuniversity, @MuhimbiliOrtho1, @TaasisiMoyoJKCI, @MuhimbiliTaifa, UDOM, Hospitali ya Benjamin Mkapa na Hospitali ya Rufaa ya Mbeya.
Mkutano huo utafanyika chini ya wenyeviti wenza Balozi wa Tanzania Nchini Uingereza Ndugu @MbelwaK na Mkurugenzi wa Afya wa NHRI Profesa Kara Hanson. Mganga Mkuu wa Serikali Prof. Tumaini Nagu atahudhuria Mkutano huo.
iamwangdamin