Mkutano Mkuu Chadema Kesho Kujibu Mapigo Dhidi ya CCM kwa Kusimka Lissu Mwenyekiti Taifa, Kumtangaza Mgombea Urais 2025 na Kumpatia Mgombea Mwenza?

Mkutano Mkuu Chadema Kesho Kujibu Mapigo Dhidi ya CCM kwa Kusimka Lissu Mwenyekiti Taifa, Kumtangaza Mgombea Urais 2025 na Kumpatia Mgombea Mwenza?

Doctor Mama Amon

JF-Expert Member
Joined
Mar 30, 2018
Posts
2,089
Reaction score
2,725
1737378693966.png

Mhe. Tundu Antipas Mughway Lissu, Mwenyekiti Mtarajiwa wa Chadema na Mgombea Urais Mtarajiwa Katika Uchaguzi wa 2025

Kutokana na mikutano mikuu ya Chadema na CCM inayofanyika kwa kufuatana ndani ya Januari 2025 sasa ni wazi kwamba busara kongwe za wanazuoni zitaanza kutimia.

Wanazuoni wengi husema kwamba ukweli uliochujwa hupatikana kutokana na mchakato wa mnyukano wenye hatua tatu zinazojumuisha mapendekezo, mapingamizi, mikingamo na majumuisho.

Katika hatua ya kwanza kuna mnyukano kati ya mapendekezo yenye kusindikizwa na ushahidi wa daraja la kwanza, daraja la pili, na daraja la tatu, na mapingamizi dhidi ya yote haya (claims vs objections)

Katika hatua ya pili kuna mchakato wa mnyukano kati ya mapingamizi na mikingamo dhidi ya mapingamizi (objections vs rebuttals)

Na katika hatua ya tatu mchakato huu huzalisha hitimisho la ukweli uliochujwa ambao ni zao la upatanisho wa kimaarifa lenye kusuluhisha mnyukano kati ya mapendekezo, mapingamizi na mikingamo (qualified conclusion)

Busara hizi zitaaanza kutimia machoni mwa wapiga kura wa Tanzania kuanzia kesho baada ya uchaguzi mkuu wa Chadema.

Uchaguzi huu wa Chadema utaweza kutoa mapingamizi dhidi ya mapendekezo ya CCM.

Kisha CCM wataleta mikingamo dhidi ya mapingamizi ya Chadema.

Sisi wapiga kura tutakuwa watazamaji katika mnyukano huu.

Hatimaye tutatoa suluhisho kupitia sanduku la kura.

Ni katika muktadha huu, taarifa zimelifikia dawati la utafiti la Dkt Mama Amon zikionyesha kuwa kesho huenda Mkutano Mkuu Chadema ukajibu Mapigo dhidi ya mkutano wa CCM uliofanyika jana.

Jana huko Dodoma, wajumbe wa CCM walitumia kanuni ya "early timer politics" kumteua Makamu Mwenyekiti wa CCM, Mgombea Urais wa CCM, na Mgombea Mwenza wa CCM katika nafasi ya Urais, ifikapo Oktoba mwaka 2025.

Kwa kufuata mantiki ile ile ya "kunywa supu ikiwa bado ya moto," inaelekea kwamba, sasa Chadema nao watajibu mapigo ili kuimarisha midahalo ya kusiasa kuelekea 2025.

Na uwezekano mkubwa ni mwamba Tundu Antipa Mughwai Lissu atasimikwa rasmi kuwa Mwenyekiti wa Chadema Taifa kwa kura zaidi ya 50%, atatangazwa Mgombea Urais 2025, na pia Mgombea Mwenza wake atatajwa.

Wote hawa watathibitishwa na Mkutano Mkuu wa Chadema.

Ni mtindo wa bandika bandua, piga nikupige, kunywa chai kabla haijapoa.

Kwa kuzingatia ukuu wa haki ya kikatiba ya kila raia anayetaka kugombea na kuchaguliwa katika nafasi yoyote ya uongozi, kama isemavyo ibara ya 21 ya Katiba ya Tanzania (1977), mpaka sasa watu wafuatao wanatajwa kuwa na nafasi kubwa ya kusimikwa katika nafasi ya Mgombea Mwenza wa Lissu:

Wakili Fatuma Karume, Prof. Assad, Mohammed Gassany, Wakili Mwabukusi, Wakili KIbatala, Dkt Bagonza, Dkt Slaa na watu eengine kadhaa

1737377396927.png

Fatuma karume

1737377470209.png

Professa Assad

1737377555166.png


Mohamed Ghassany

1737379218493.png

Wakili Mwabukusi

1737381933477.png

Peter KIbatala

images.jpeg

Ask. Dkt. Benson Bagonza

download (1).jpeg

Balozi Dkt. Wilbrod Slaa

Hebu tujiulize maswali machache:

Unadhani mgombea urais kwa tiketi ya Chadema atakuwa nani?

Kama ni Lissu Unajua Mgombea mwenza wa Lissu atakuwa nani?

Unafikiri kujulikana kwa Mgombea Urais wa Chadema na Mgombea mwenza wake kutakuwa na mchango kiasi gani katika kuchangamsha pilika za siasa za Tanzania?

Unadhani kati ya Timu CCM na Timu Chadema ni timu gani yenye mikakati iliyo na zindiko kubwa dhidi ya mishale ya kambi hasimu?

Na je, kati ya Timu Chadema na Timu CCM, unadhani ni timu gani itakuwa na mguso wa karibu kwa wapiga kura wa Tanzania ya leo?

Uhakika ni kwamba yaliyotokea kwenye Mkutano wa CCM Dodoma jana yamefungua ukurasa mpya katika siasa za Tanzania, yakiwa yanatuonyesha ukweli-nusu.

Tayari tunajua "Kisigino gani chenye udhaifu wa zindiko katika mikakati ya CCM," yaani "CCM's Achilles' Heel"

Lakini, yajayo kutoka Dar Es Salaam kwenye Mkutano Mkuu wa Chadema yatatoa sura kamili ya siasa za Tanzania kuelekea uchaguzi mkuu wa 2025.

Yaani tutaweza kufahamu "Kisigino gani chenye Udhaifu wa zindiko katika mikakati ya Chadema," yaani "Chadema's Achilles' Heel."

Ni baada ya hapo, bila kupiga ramli tutaweza kuwatangazia Watanzania mshindi wa uchaguzi wa Urais ifikapo Oktoba 2025 atakuwa ni nani hasa!

Hao Watanganyika kina Wakili Mwabukusi, Wakili Kibatala, Aslofu Dkt Bagonza, Dkt. Slaa na watu baki kama wao, wanatajwa kwa sababu moja ya kikatiba.

Kwa mujibu wa ibara ya 21 ya Katiba ya Tanzania (1977) wao ni raia wenye haki ya kugombea na kuchaguliwa katika nafasi yoyote ya uongozi wa nchi.

Kwa sababu ya kifungu hiki l wigo wa kijiografia wa wagombea wa nafasi ya Umakamu Rais wa Tanzania unagusa kona zote za Tanzania ukiwemo upande wa Tanganyika na Zanzibar bila kujali mgombea urais wa Tanzania ametoka wapi.

Kwa mtazamo wa kisheria, hii maana yake ni kwamba, kifungu cha 47(3) cha Katiba ya Tanzania (1977) ni ubatili na utupu tangu mwanzo.

Yaani kifungu hiki cha 47(3) ni ubatili na utupu tangu mwanzo. Yaani, NULL AND VOID AB INITIO.

Ubatili wake unatokana na ukweli kuwa kinabagua kimakosa baadhi ya Watanzania, ambao kwa mujibu wa ibara ya 21 ya Katiba hiyo hiyo, wanayo haki, na wanataka kugombea nafasi ya Umakamu wa Rais wa Tanzania.

Kifungu hiki batili kinasomeka kama ifuatavyo:

"47(3) Mtu atateuliwa kugombea kiti cha Makamu wa Rais kwa kufuata kanuni kwamba endapo Rais wa Jamhuri ya Muungano atatoka sehemu moja ya Muungano, basi Makamu wa Rais atakuwa ni mtu anayetoka sehemu ya pili ya Muungano."

Inasemekana kuwa wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Chadema wameapa kutotanbua uhalali wa kifungu hiki cha kikatiba kwa sababu iliyotajwa hapo juu.

Sasa, baada ya kusema hayo, na kabla ya kumalizia niseme neno kuhusu dhana ya "Kisigino chenye udhaifu wa zindiko katika mikakati ya kina Achilles."

Kulingana na Ngano za kale za Wagriki, "Kisigino chenye udhaifu wa zindiko katika mikakati ya Achilles" ni maneno yanayomaanisha udhaifu wa mtu mwente maguvu ukiwa umefichika mwilini mwake, kiasi kwamba, adui yake akiufahamu na akajipanga kushambulia vizuri eneo la mwili wake lisilo na zindiko, basi adui anapata ushindi kamili.

Katika Ngano za kale za Wagriki, mama yake Achilless alimtosa mtoto wake kwenye mto ulioitwa "Styx" ili kumpa zindiko la kimwili litakalomlinda na mabaya ya dunia hii.

Wakati mama anamzamisha Achilles kwenye mto huo alikuwa ameshika kisigino cha mguu wa kulia cha mtoto huyo.

Hivyo, kisigino hicho cha kulia hakikuzamishwa kwenye maji ya mto na hivyo hakikupata zindiko kabisa.

Baadaye, Achilles alikua na kuwa askari hodari aliyefanikiwa kubutua mishale na risasi zote kwa sababu mwili wake wote ulikuwa na zindiko maalum likinfanya aonekane kama mtu aliyevakia jaketi la kuzyia risasi yaani bullet proof coat.

Lakini, siku moja akiwa katika vita ya "Trojan" maadui zake walipata kujua siri kuhusu kisigino gani cha Achilles hakina zindiko kabisa.

Hivyo walifyatua mishale yenye sumu kukilenga kisigino kile, cha kulia, na hatimaye mshale mmoja ukamchoma na kuondoa uhai wa jasiri Achilles.

Tangu wakati huo, maneno "Kisigino cha udhaifu wa zindiko katika mikakati ya Achilles" hutumika kumaanisha kipengele cha udhaifu wa mtu, mfumo, taasisi au mikakati.

Tayari tunajua kisigino cha udhaifu wa zindiko la mikakati ya Timu CCM ni kipi.

Kesho tutajua vema kisigino cha udhaifu wa zindiko la mikakati ya Timu Chadema ni kipi.

Stay tuned.

=========UPDATES=========

A. MATOKEO YA MWENYEKITI TAIFA
  • Odero Odero - Kura 01 Sawa na 0.1%
  • Freeman Mbowe - Kura 482 Sawa na 48.3%
  • Tundu Lissu - Kura 513 Sawa na 51.5%

B. MATOKEO YA MAKAMU MWENYEKITI BARA
  • Mathayo Gekul - Kura 49 Sawa na 5%
  • Ezekia Wenje -Kura 372 Sawa na 37%
  • John Heche - Kura 577 Sawa na 57%
C. MATOKEO YA MGOMBEA URAIS NA MGOMBEA MWENZA
  • Uamuzi wa chama ni kwamba watavuka mto baada ya kuufikia. Kwa sasa kipaumbele sio uchaguzi bali mageuzi ya kimfumo kwa ajili ya kuweka uwanja wa uchaguzu ulio tambarare kwa washirikibwote. Video ifuatayo inafafanua;

View attachment 3210255
 
Yaani Tundu Antipa Mughwai Lissu atasimikwa rasmi kuwa Mwenyekiti wa Chadema Taifa kwa kura zaidi ya 50%, atatangazwa Mgombea Urais 2025, na pia Mgombea Mwenza wake atatajwa, na wote kuthibitishwa na Mkutano Mkuu wa Chadema. Ni mtindo wa bandika bandua, piga nikupige.
Chadema wakifanya hivi , Samia atazimia na kupata heart-attack. Watawavuruga sana ccm.
 
Mnaacha kufanya mambo yenu mnajilinganisha na CCM. Sasa mnawajibu mapigo ina maana wasingefanya wao na ninyi msingefanya.
 
View attachment 3207445
Mhe. Tundu Antipas Mughway Lissu, Mwenyekiti Mtarajiwa wa Chadema na Mgombea Urais Mtarajiwa Katika Uchaguzi wa 2025

Sasa ni wazi kwamba yale maneno ya wanafilosofia wa kale wa Magharibi yasemayo kwamba ukweli hujulikana kutokana na mnyukano kati ya hoja, hoja-kinzani na hatimaye kuzaliwa kwa hoja-sanisi, yataaanza kutimia machoni mwa wapiga kura wa Tanzania kuanzia kesho.

Naongelea matumizi ya kanuni ya "thesis, anti-thesis, and synthesis" katika siasa za kitaifa, ambako kila kambi hujitahidi kufanya utafiti juu ya "Kisigino cha Udhaifu," yaani "Achilles' Heel," katika mwili wa kambi kinzani.

Ni hivi: Taarifa za uhakika zilizolifikia dawati la utafiti la Dkt Mama Amon zinaonyesha kuwa kesho huenda Mkutano Mkuu Chadema ukajibu Mapigo dhidi ya mkutano wa CCM uliofanyika jana.

Yaani Tundu Antipa Mughwai Lissu atasimikwa rasmi kuwa Mwenyekiti wa Chadema Taifa kwa kura zaidi ya 50%, atatangazwa Mgombea Urais 2025, na pia Mgombea Mwenza wake atatajwa, na wote kuthibitishwa na Mkutano Mkuu wa Chadema. Ni mtindo wa bandika bandua, piga nikupige.

Unadhani Mgombea mwenza wa Lissu atakuwa nani?

Unafikiri kujulikana kwa Mgombea Urais wa Chadema na Mgombea mwenza wake kutakuwa na mchango gani katika pilika za siasa za Tanzania?

Na je, kati ya Timu Lissu na Timu Samia, unadhani ni timu gani itakuwa na mguso wa karibu kwa wapiga kura wa Tanzania?

Yaliyotokea kwenye Mkutano wa CCM Dodoma jana yamefungua ukurasa mpya katika siasa za Tanzania, yakiwa yanatuonyesha ukweli-nusu.

Tayari tunajua "Kisigino cha Udhaifu," yaani "Achilles' Heel," katika kambi ya CCM kiko wapi.

Lakini, yajayo kutoka Dar Es Salaam kwenye Mkutano Mkuu wa Chadema yatatoa sura kamili ya siasa za Tanzania kuelekea uchaguzi mkuu wa 2025.

Yaani tutaweza kufahamu "Kisigino cha Udhaifu," yaani "Achilles' Heel," katika kambi ya Chadema kiko wapi.

Ni baada ya hapo, bila kupiga ramli tutawatangazia Watanzania mshindi wa uchaguzi wa Urais ifikapo Oktoba 2025 ni nani hasa!

Wafuatao wanatajwa tajwa kuhusu nafasi ya Mgombea Mwenza wa Lissu, japo inasemekana kuwa ikibidi kutaanzishwa mkakati wa kulazimisha mabadiliko ya Katiba ili kupanua wigo wa wagombea binafsi kwa kufuta kifungu cha 47(3) katika Katiba ya Tanzania (1977).

Kifungu hiki kinasema kuwa: "47(3) Mtu atateuliwa kugombea kiti cha Makamu wa Rais kwa kufuata kanuni kwamba endapo Rais wa Jamhuri ya Muungano atatoka sehemu moja ya Muungano, basi Makamu wa Rais atakuwa ni mtu anayetoka sehemu ya pili ya Muungano."


View attachment 3207408
Fatuma karume

View attachment 3207411
Professa Assad

View attachment 3207413

Mohamed Ghassany

View attachment 3207474
Wakili Mwabukusi
Kwa ujengaji hoja wako..wewe sio mama amon...kuanzia leo nakuita baba amon

Uchambuzi mzur Sanaa wapenda maendeleo/mageuzi/ upinzani tuna ungana na wapenda NURU ili kulishinda GIZA

Freeman mbowe ni GIZA na TUNDU LISU ni NURU.
 
CHADEMA hawapaswi kuchelewa kunywa supu ya moto, ikipoa haina ladha nzuri. Kama ACT tayari wamejipanga kwa uchaguzi mkuu why CHADEMA wasifanye hima kumtangaza mgombea wao mapema? waache makundi yao haraka warudi pamoja kujibu mapigo ya CCM haraka
 
Back
Top Bottom