Mkutano wa 13 wa Mwaka wa Jukwaa la Wahariri Tanzania, TEF, Mgeni Rasmi ni Dotto Biteko, Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati

Tasnia ya habari Kwa Sasa mmekuwa mkipangiwa habari za kutangaza Kwa umma, hakuna uhuru wa vyombo vya habari kama ilivyokuwa kipindi Cha Kikwete.
 
Aisee doto jana tu alikua na washika dau kasimama sana pale mbele , leo yupo huko tena. Mwana anapambana
 
Hili jukwaa la wahariri ni kusanyiko la wahuni tupu, badala ya kumwalika Tido Mhando ambaye aje awape mbinu na uzoefu unamleta Doto ambaye ni Mwl hajui hata tasnia ya habari ikoje na hana mchango wowote ni kutafuta kujipendekeza kwa watawala, namna hii kuna mhariri ataruhusu habari ya kukosoa hii serikali dhalimu na fisadi? shame on you
 
Nchi ya ovyo sana hii,mtu anapewa madaraka ambayo kimsingi hata hayapo matokeo yake kazi yake inabaki kuzurura kwenda kufungua mikutano tu! Sasa kulikuwa kuna haja gani ya kuanzisha cheo kama hicho wakati kuna mawaziri wa kila sekta si waziri husika angefungua tu huo mkutano.
Huku mitaani watu wanateseka kwa kukosa huduma muhimu wao kazi yao kugawana vyeo na kutapanya fedha ovyo tu kwa sababu ya tamaa ya madaraka ya mtu mmoja ambaye anafikiri akigawa vyeo kwa kila kundi itamfanya aungwe mkono na kila mtu kutoka kila pembe ya nchi!
 
Acha kuwapangia watu. Sheria za kwenye familia zako usitake kuleta hata kwenye mambo ya muhimu na ya msingi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…