Mkutano wa Dharura wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa SADC walaani mashambulizi ya M23 na RDF, waunga Mkono juhudi za Kidiplomasia kutatua mgogoro huu

Mkutano wa Dharura wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa SADC walaani mashambulizi ya M23 na RDF, waunga Mkono juhudi za Kidiplomasia kutatua mgogoro huu

Heparin

JF-Expert Member
Joined
Sep 24, 2021
Posts
242
Reaction score
1,141
Mkutano wa Dharura wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) ulifanyika tarehe 31 Januari 2025, Harare, Zimbabwe, chini ya uenyekiti wa Rais wa Zimbabwe, Emmerson Mnangagwa. Mkutano huu ulijadili hali ya usalama Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC).

Pamoja na mambo mengine, Mkutano ulilaani mashambulizi yanayofanywa na kundi la waasi la M23 na Jeshi la Rwanda (RDF) dhidi ya vikosi vya serikali ya DRC, ujumbe wa kijeshi wa SADC (SAMIDRC), na raia wa Kivu Kaskazini. SADC ilitoa rambirambi kwa familia za wanajeshi waliopoteza maisha na kusisitiza urejeshaji wa huduma muhimu kama maji, umeme, na usafirishaji wa chakula.

Viongozi wa SADC walikubaliana kuendelea kuunga mkono juhudi za kidiplomasia kupitia Mchakato wa Luanda na Nairobi ili kurejesha amani. Pia, waliagiza kupelekwa kwa mawaziri wa ulinzi na wakuu wa majeshi ili kuhakikisha usalama wa vikosi vya SAMIDRC na kurejesha majeruhi na waliopoteza maisha.

SADC ilirejea dhamira yake ya kuilinda DRC dhidi ya uvamizi wa nje na kuhimiza pande zinazozozana kushiriki mazungumzo ya amani. Mkutano ulimalizika kwa kuthamini mchango wa viongozi wa SADC na wanajeshi waliopo DRC kwa ajili ya kulinda amani.
 

Attachments

Hapo Ndiyo Wamemaliza Kufanya Maamuzi, Yaani Watu Wanauwawa Kama Hakuna Wenye Nguvu Kuzuia Hayo
 
Kila siku kulaani, kulaani, kulaani!
Wanatakiwa wafanye maamuzi magumu, tayari adui anajulikana ila wao wanadhani kwa kulaani adui atanywea
 
Yani wanatiwa kidole alafu wanasema wakae chini na magaidi wajadiliane 😊

Kwa style hii naona m23 wakienda hadi mji mkuu
 
Kulaani! Kwamba laana w23 wawevichaa??😁
nchi kama zote zinapatikana congo kulikoni??
Kiongozi wa nchi aibu yake, nchi imefia mikononi mwake!!
 
Mkutano wa Dharura wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) ulifanyika tarehe 31 Januari 2025, Harare, Zimbabwe, chini ya uenyekiti wa Rais wa Zimbabwe, Emmerson Mnangagwa. Mkutano huu ulijadili hali ya usalama Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC).

Pamoja na mambo mengine, Mkutano ulilaani mashambulizi yanayofanywa na kundi la waasi la M23 na Jeshi la Rwanda (RDF) dhidi ya vikosi vya serikali ya DRC, ujumbe wa kijeshi wa SADC (SAMIDRC), na raia wa Kivu Kaskazini. SADC ilitoa rambirambi kwa familia za wanajeshi waliopoteza maisha na kusisitiza urejeshaji wa huduma muhimu kama maji, umeme, na usafirishaji wa chakula.

Viongozi wa SADC walikubaliana kuendelea kuunga mkono juhudi za kidiplomasia kupitia Mchakato wa Luanda na Nairobi ili kurejesha amani. Pia, waliagiza kupelekwa kwa mawaziri wa ulinzi na wakuu wa majeshi ili kuhakikisha usalama wa vikosi vya SAMIDRC na kurejesha majeruhi na waliopoteza maisha.

SADC ilirejea dhamira yake ya kuilinda DRC dhidi ya uvamizi wa nje na kuhimiza pande zinazozozana kushiriki mazungumzo ya amani. Mkutano ulimalizika kwa kuthamini mchango wa viongozi wa SADC na wanajeshi waliopo DRC kwa ajili ya kulinda amani.
Maamuzi legevu hiviii...
 
... mpaka Kigali ya Habyarimana inaanguka, mpaka Habyarimana anauawa, mpaka mauaji ya kimbari yanaanza Rwanda juhudi za kidiplomasia zilikuwa zinaendelea!
:AweeWoo: :AweeWoo: :AweeWoo: 🤣
 
Maamuzi yaliyostahili ni kumpiga yule kimbaumbau tu kijitu chenye roho mbaya kinaona kuua mtu ni kama kuua sisimizi
 
Back
Top Bottom