Mkutano wa Modi na Abe waahirishwa kutokana na machafuko India

Mkutano wa Modi na Abe waahirishwa kutokana na machafuko India

Nyendo

JF-Expert Member
Joined
Jun 4, 2017
Posts
1,336
Reaction score
4,731
Mkutano wa kilele uliotarajiwa kuwakutanisha Waziri Mkuu wa India Narendra Modi na mwenzake wa Japan Shinzo Abe umeahirishwa.

Kulingana na wizara ya mambo ya kigeni ya India hatua hiyo inatokea wakati kukiwa na maandamano yaliyosababisha machafuko kwenye eneo lililoandaliwa kwa ajili ya mazungumzo.

Msemaji wa wizara hiyo Raveesh Kumar amesema kwenye taarifa yake kwamba pande zote zimeamua kuahirisha ziara hiyo hadi tarehe itakayokubalika katika siku za usoni.

Abe alitarajiwa kuwasili India Desemba 15 na kufanya mazungumzo na Modi katika mji wa Guwahati kaskazini mwa jimbo la Assam ambao hata hivyo umezingirwa na waandamanaji wiki hii wakipinga sheria mpya yenye utata kuhusu uraia.


MODIABE.jpg

Chanzo: DW Kiswahili
 
Hao waandamanaji wajitafakari, Marais wa siku hizi hawaki mchezo...
 
Hao waandamanaji wajitafakari, Marais wa siku hizi hawaki mchezo...
Ila wabongo kwa unafiki hamjambo sio wewe kila siku unalalamika jiwe kuzuia maandamano na mikutano?
Sasa mbona unajisikia vibaya watu wa India wakiandamana kudai haki zao?
 
Ila wabongo kwa unafiki hamjambo sio wewe kila siku unalalamika jiwe kuzuia maandamano na mikutano?
Sasa mbona unajisikia vibaya watu wa India wakiandamana kudai haki zao?
Mimi uliishaniwahi kuniona naandamana
 
Back
Top Bottom