mkuu wa it baraza la mitihani asimamishwa kazi.


rais - muislamu
makamu wa rais - muislamu
rais wa zanzibar - muislam
makamu wake wa kwanza - muislam
makamu wake wa pili - muislamu
waziri mkuu mkristu


sasa sijui which is which

Unataka tanzania tuanze kusema haya?? "kama sio hawa waislamu, tungekua mbali sana......."

we kaa kimya faidi hizo bakshishi za kupiga scrub na kubeba begi la dark child

mengine acha kabisa kwenye dini huna hoja

wakati watu wansoma uchumi (na wewe ulisoma uchumi) wengine walikua bize na alif laam miim) haiwezekani kutegemea mahindi kwenye mizeytuni
 
Alieanzisha Algebra ni nani? katoliki au?
haha wewe unaweza kuanza kitu kikakushinda kumaliza na wenye akili wakamalizia , utakaa unajisifu, mimi mtu wa kwanza kuweka kibanda kawe, wakati huo ushapigwa danadana uko mkuranga

wakuja wanakupiga tanji tu

ujanja kupata
 
wapendwa,

kusema ukweli ndalichako alitakiwa nae kusimamishwa kama si kujiuzulu mwenyewe!! amedhihirisha kuwa ni mzembe wa hali ya juu kabisa!

mbarikiwe sana

Glory to God!
 
Nitaomba IT awekwa Muislamu ila kuondoa visingizio..
 
Safi hii. Ni lazina tujijengee utamaduni wa kuwajibika/kuwajibishana.
 

Angalia gazeti la Mwananchi la Juni 8 utaona matokeo mapya. Sijaona chochote cha maana kwa sababu, asilimia 80 wamepata F. Mie nashangaa watu wanaolalmikia matokeo hata darasa la 7 hawajafika. Hata hawajui mitihani huwa inakuwa vipi wanalialia ovyo tu. Kwa taarifa wanafunzi wengi huwa wanaweka effort ndogo sana kwenye mitihani hiyo ndiyo maana wanafeli sana.
 
Asilimia kama 60-70 ni F. Niliona A kama mbili hivi, B na C nazo chache mno. D ni nyingi za kutosha...Hivi hilo somo ni gumu kiasi hicho au watahiniwa nao ni wagumu.
Kama sio kosa, naomba kwenda pembeni kidogo ya mada, zaidi ya Uislamu na udini na "Ndalichako," kwa sababu mustakabali wa elimu ya nchi yetu nadhani ni suala kubwa kuliko "Ndalichako."

Sijui siku hizi lakini wakati mimi nasoma mtihani wa Kiswahili ulikuwa unarindima D na F. In fact miaka sita niliyokuwa sekondari sikuwahi kusikia A ya kiswahili. Ma genius wote ninaowajua wa Dar-es-Salaam (in fact nchi nzima, manake mtu alikuwa akimwaga radhi kwenye nationals hata kama ni wa mikoani mnasikia) miaka hiyo mid nineties kwenda nyuma hakuna aliyepata A ya Kiswahili, sikuwahi kusikia. Mbona hili halikuwa tatizo? Tukaaminishwa kwamba eti hatujui Kiswahili, tumekuwa raised tunaongea broken Swahili.

Which could be very true, kwamba tunaelewana kwa maongezi lakini lugha rasmi ya kujibia mitihani ya Kiswahili hatuijui. Ok, swali linakuja, mbona Kiingereza watu kibao wanapata A halafu Kiswahili F's zimetandaa? Umezaliwa Tandahimba Kijiji cha Ujamaa, umesomea Tandale Kwa Mfuga Mbwa, halafu leo eti unajua Kiingereza kuliko Kiswahili!

Basi nadhani kama kuna tatizo baraza la mitihani inawezekana halijaanza na, na ni kubwa kuliko, "Ndalichako."
 
JF inayokuja itakuwa ni jamvi la uhakika kidogo maana itakuwa unapewa access baada kuchangia kiasi fulani kuanzia 50,000 kwa mwaka!pumba zitapungua sana
 
Pamoja na yoote hayo jamaa wa kwa mama mdogo wanapenda sana kulalamika,mm nimekulia pwani nawajua sana,hii ni kawaida yao!hata kama limefanyika kosa la kawaida wao watalalamika tu,hembu fikiria zanzibar wamechoma makanisa sisi tumewaangalia tu,lakini wao matokeo yamekosewa wamesahfika barabarani,aibu kubwa sana!
 
Waziri je?

mpendwa,

waziri si mtendaji wa baraza la mitihani, yeye angeweza tu kutakiwa kujiuzulu kama yangekuwa makosa ya kibajeti, kisera ama kimkakati nk. ambayo anawajibika nayo moja kwa moja

sema tu hao wanaojiita waislamu ndio wanahisi kuwa kufelishwa wanafunzi waliofanya somo la maarifa ya kiislam ulikuwa ni "mkakati" wa kuididimiza jumuia ya kiislam kielimu! halafu wakati huohuo wanammtaka mutu anaueitwa "joyce" ajiuzulu bila kumtaka na na waziri wake wa elimu ajiuzulu, hapo ndipo wanapodhihirisha "wehu' wao. inaonekana wengi wanasukumwa na hisia za udini tu katika kuweka mashinikizo yao lakini masikini, hawajui masuala ya public administration!

ubarikiwe sana

Glory to God!
 
Wala suala la matatizo ya Baraza la mitihani si hilo lililogunduliwa na Waislam. Angalia kauli hizi za ajabu. Kwaza Dr Ndalichako alikataa kuwa hakuna makosa yoyote kwa maana ati wanasahihisha kwa umakini mkubwa. Pili, amekiri ni makosa tu ya kibinadamu, je, ni wanatahiniwa wangapi hukumbwa na makosa ya kibinadamu na hukaa kimya? Baraza la mitihani lina matatizo makubwa. Ni watahiniwa wangapi huvurugiwa matokeo yao kwa mtindo huu? Linahitaji kufumliwa na kuundwa upya.
 

wapendwa,

ndo maana nasema huyo ndalichako ndiye hasa aliyetakiwa kujiuzulu akajifunze upya maana ya 'mtihani'

mbarikiwe sana wapendwa,

glory to God!
 
Huko kuna madudu mengi sana wanaofanyiwa Waislaam, tume huru tu ikachunguze kwa undani madai ya miaka mingi ya Waislaam, yaunganishwe na yale waliolalamika Zanzibar juzi kuhusu NECTA.

Ukweli ukidhihiri uongo hujitenga.

Mkuu si kwa waislamu tu. Kwa ujumla ni kuwa hawa jamaa huwa wanafanya makosa sana tu. Kuna watu wengi tu ambao huwa wanapewa matokeo ambayo si ya kwao kila mwaka. Umakini unahitajika sana kwa hawa watu maana inaonekana wako careless sana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…