Pre GE2025 Mkuu wa Mkoa kutoa chai na mkate kupunguza wafanyakazi kuzurula muda wa kazi

Pre GE2025 Mkuu wa Mkoa kutoa chai na mkate kupunguza wafanyakazi kuzurula muda wa kazi

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Replica

JF-Expert Member
Joined
Aug 28, 2017
Posts
1,681
Reaction score
8,887
Mkuu wa Mkoa wa kusini Unguja Visiwani Zanzibar, Ayoub Mohammed Mahamoud, ametangaza uamuzi mpya wa kuwapatia Wafanyakazi wa Ofisi yake chai ya asubuhi ikiwa na kitafunwa cha mikate wenye siagi kuanzia kesho Jumatatu May 6 2024 ili kupunguza Wafanyakazi kuzurura saa za kazi, kuongea na simu mara kwa mara pamoja na kutoka nje kwenda kununua urojo.

RC Ayoubu ameyasema hayo leo wakati akifungua kampeni ya ‘amshaamsha Kusini’ ikiwa ni mahususi kwa Watumishi wa Serikali lengo likiwa ni kutokomeza uchelewaji makazini, kuzurura muda wa kazi na matumizi ya simu vitu ambavyo amesema haridhishwi navyo kwani vinachelewesha maendeleo ya Wananchi ambapo amesisitiza kuwa gharama zote za chai na vitafunwa zitakuwa zikitoka kwenye mshahara wake yeye Mkuu wa Mkoa.

#Tanzania2025
 
Zanzibar mkate wao mkubwa ni boflo zinauzwa 250 na 500 tzsh ni mkate flani hivi haina lafha upo upo tu sema wenyewe washauzoea.
 
Shule walikuwa na menu wanaita 'special diet' kwa changamoto kama hizo..😁
Hiyo Special diet imenikumbusha mbali, siku ya nyama nilikuwa najifanya situmii nyama tunapikiwa mchanganyiko mmoja mzuri wa mboga za majani halafu nikirudi bwenini tunakula pamoja na mshkaji wangu tunachanganya na nyama aliyochukua yeye, ugali utaliwa hapo mpaka basi.
 
Back
Top Bottom