Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 3,984
- 13,760
Ameeleza hayo leo tarehe 18 Juni 2024, wakati akizungumza kwenye Mashindano hayo ya Umoja wa Shule za Sekondari Tanzania, yanayofanyika Mkoani Tabora kwa mara ya tatu mfulululizo.
Kuhusu maazimio ambayo yametolewa na viongozi mbalimbali juu ya kukuza michezo, amesema kuwa Mkoa utayasimamia yote yaliyoazimiwa kwa ajili ya maendeleo ya michezo nchini.
Akitoa salam za Mkoa kwa Mgeni rasmi Waziri wa Sanaa Utamaduni na Michezo Dkt. Damas Ndumbaro, Mkuu huyo wa Mkoa amemhakikishia kuwa wamejipanga kahakikisha kuwa michezo inapewa kipaumbele katika shule mbalimbali.
"Viongozi wetu wa kitaifa akiwepo Waziri Mkuu wakati wa uzinduzi rasmi wa mashindano ya UMITASHUMTA & UMISSETA 2024 alisisitiza juu ya kukuza na kuendeleza vipaji vitakavyoibuliwa katika mashindano haya, na sisi kama mkoa tumejipanga kutekeleza hilo," amesema Mkuu wa Mkoa wa Tabora.