Uchaguzi 2020 Mkuu wa Mkoa wa Mtwara awaombea kura wagombea wa CCM kwa watumishi wa sekta binafsi

Uchaguzi 2020 Mkuu wa Mkoa wa Mtwara awaombea kura wagombea wa CCM kwa watumishi wa sekta binafsi

Lazia Sultan

Senior Member
Joined
Jun 4, 2020
Posts
120
Reaction score
328
Tarehe 5 September 2020 ndugu Gelasius Byakanwa aliwaita watumishi wanaofanyia kazi kwenye taasisi zinazomilikiwa na watawa wa shirika la kikatoliki la Mt. Benedicto Ndanda kwenye kikao kifupi Cha kuzungumza nao.

Watawa hawa wana watumishi wengi kwani ndiyo wanaomiliki Ndanda Refferal Hospital, Abbey sec School, Abbey pure drinking water, printing press and bookshop, nursing school, trade school na workshop nyingi Kama plumbing, welding, garage, carpentry na takataka nyingine nyingi.

Hivyo watawa hawa wameajiri watu wengi sana ambao mh mkuu wa Mkoa amecheza karata zake kwenda kuwaombea kura wagombea wa CCM katika uchaguzi mkuu hapo October 28 mwaka huu.

Mmoja wa waliohudhuria kanambia walipewa taarifa ya kikao hicho cha mkuu wa Mkoa ila hawakujua agenda ni nini, walizikuta huko huko, ambazo kwa asilimia kubwa ni kuwataka washiriki uchaguzi mkuu kwa kuwachagua ccm kwani wamekuwa bega kwa bega na taasisi hiyo tangu zamani, hivyo waendeleze mshikamano huo.

Kwa mtazamo wangu sasa naanza kuona jinsi CCM walivyopoteza matumaini kutoka kwa watumishi wa umma hadi kuamua kucheza karata zao kwa private sectors. Wameanza kuukimbia na kuuogopa mzimu wao wenyewe hadi wanaenda kwa jirani.
 
Ccm walijisahau walijua kwa kununua wabunge wa upinzani basi kazi yao imeisha.

Kadri Lisu anavyozidi kutema cheche mpk John mzee wa kuhubiri makanisani amegoma kusali leo ili apige kampeni.
 
Hayo ni mawazo yako finyu, ila ukweli ni kuwa CCM ni chama nyenyekevu kwa watu wake kuomba na kujishusha kwa watu haimaanishi wewe ninmasikini.
 
Hali imekuwa tete, wameamua kuzigeukia tasisi za dini kuomba kura. Leo kule Arusha waziri mkuu alienda kwenye kongamano lililo andaliwa na safina redio.
 
Alikuwapo mkuu wa mkoa wa Mwanza ailiitwa Magesa mlongo, nakumbuka mwaka 2010 alituita kwa vitisho kwenye kikao na kutuambia ni lazima tuchague CCM, tulijiuliza kwani wakati wa kupiga kura kuwa siri? Mungu si Rajabu baada ya uchaguzi kumalizika tu, hakuteuliwa na ikawa ndio mwisho wake. Hata huyu Byakanywa subili tu, time will tell.
 
Alikuwapo mkuu wa mkoa wa Mwanza ailiitwa Magesa mlongo, nakumbuka mwaka 2010 alituita kwa vitisho kwenye kikao na kutuambia ni lazima tuchague CCM, tulijiuliza kwani wakati wa kupiga kura kuwa siri? Mungu si Rajabu baada ya uchaguzi kumalizika tu, hakuteuliwa na ikawa ndio mwisho wake. Hata huyu Byakanywa subili tu, time will tell.
Magesa alikuwa anapenda Sana Media, sijui yupo wapi yule mbaba.
 
Back
Top Bottom