Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mtanda: Ajibu shutma vurugu za Simba SC, CCM Kirumba, "Sikuingia Uwanjani"

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mtanda: Ajibu shutma vurugu za Simba SC, CCM Kirumba, "Sikuingia Uwanjani"

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Kufuatia sakata lililotokea Mwanza, na Uongozi wa klabu ya Simba kutoa taarifa ya kulaani vikali vitendo visivyo vya kiungwana vilivyodaiwa kufanywa na viongozi wa timu ya Pamba Jiji FC kwa kushirikiana na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Said Mtanda, pamoja na maafisa wa polisi.

Soma, Pia:

+
Vurugu kali zimezuka Uwanja wa CCM Kirumba wakati Simba SC ikifanya mazoezi kuelekea mechi na Pamba Jiji hapo kesho
+ Simba yalaani matumizi ya Polisi kuwazuia kufanya mazoezi katika uwanja wa CCM Kirumba kuelekea mchezo wa dhidi ya Pamba

Kupitia Crown FM, Said Mtanda, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza amesema:

"Mimi ninaamini mpira utachezwa leo, na mkuu wa mkoa akitembelea sehemu ya mkoa wake iwe uwanjani au amekwenda hospitali haina maana kwamba ameenda kuwahujumu wagonjwa au wachezaji"

"Mimi nikiwa ofisini kwangu jana nilipata taarifa kuna dalili za uvunjifu wa amani, baadhi ya makomandoo wa Simba Sc wamewahold viongozi wa Pamba Jiji Fc ambao walikuwa uwanjani wakifanya mazoezi kabla ya kuondoka, sasa wamefunga milango yote, wale vijana walipoona watashambuliwa wakaenda juu VIP wakafunga milango...."

"Makomandoo wa Simba sc wakaanza kuvunja vioo vya VIP ya CCM Kirumba, lakini baadae wakaanza kuvunja milango, kwa hiyo wakanipigia mimi, nikampigia Mkurugenzi wa jiji, lakini nikawapigia jeshi la polisi, na nikafikiri ni busara kusogea eneo hilo ili baadae mambo yasije kutangazwa ambayo sio sahihi.... lakini pia kuhakikisha jeshi la polisi linafanya kazi yake kwa weledi"

"Sikuingia uwanjani na wala sikuwa na nia ya kuona mazoezi ya Simba Sc, kwa sababu mimi ndio mgeni rasmi, nina haraka gani ya kuwaona Simba Sc wakati leo nilikuwa na uwezo wa kuiona Simba Sc kwa utulivu kwa dakika 90?"
1732264043872.png
 
Simba wanajiona wako juu ya mamlaka
Hao makomando wa Simba wa Nini?
Simba wanamiliki jeshi?
Hao walileta michezo yao ya kusambaza ngada.
Piga kazi RC mtanda
 
Simba wanajiona wako juu ya mamlaka
Hao makomando wa Simba wa Nini?
Simba wanamiliki jeshi?
Hao walileta michezo yao ya kusambaza ngada.
Piga kazi RC mtanda
Usijibu hoja kwa kusikiliza/kuangalia upande mmoja tu. Jitahidi kusikiliza pia upande wa pili halafu uje utoe maoni yako kwa utulivu kabisa, huku ukiweka ushabiki pembeni, angalau kwa muda.
 
Usijibu hoja kwa kusikiliza/kuangalia upande mmoja tu. Jitahidi kusikiliza pia upande wa pili halafu uje utoe maoni yako kwa utulivu kabisa, huku ukiweka ushabiki pembeni, angalau kwa muda.
Mazoezi ya Simba Yana u special Gani hadi yazuie viongozi wa serikali kutimiza majukumu Yao ya kikatiba
Umeambiwa kuwa makomando wa Simba walikuwa wanavunja vioo na milango kushambulia viongozi wa Pamba.

We ulitaka watu wafe muanze kulaumu uongozi wa mkoa?
 
Simba wanajiona wako juu ya mamlaka
Hao makomando wa Simba wa Nini?
Simba wanamiliki jeshi?
Hao walileta michezo yao ya kusambaza ngada.
Piga kazi RC mtanda
Inakuwaje usikie upande mmoja na kuanza kutolea hukumu? Yaani tukio la fujo uwanjani ni kubwa kiasi gani hadi Mkuu wa Mkoa afike? Wakuu wa mikoa tunawaona kwenye matukio makubwa kama migomo ya wafanyabiashara, moto kuteketeza majengo mengi (sio nyumba moja) kama soko, majanga ya asili na ya kutengenezwa kama majengo yenye watu wengi kuporomoka au mafuriko kutokea nk. Lakini eti mlinzi ametofautiana na uongozi wa timu RC anawasha gari kwenda kufuatilia, utafuatilia vingapi?
 
Inakuwaje usikie upande mmoja na kuanza kutolea hukumu? Yaani tukio la fujo uwanjani ni kubwa kiasi gani hadi Mkuu wa Mkoa afike? Wakuu wa mikoa tunawaona kwenye matukio makubwa kama migomo ya wafanyabiashara, moto kuteketeza majengo mengi (sio nyumba moja) kama soko, majanga ya asili na ya kutengenezwa kama majengo yenye watu wengi kuporomoka au mafuriko kutokea nk. Lakini eti mlinzi ametofautiana na uongozi wa timu RC anawasha gari kwenda kufuatilia, utafuatilia vingapi?
Umeambiwa kuwa makomando wa Simba walivamia jengo walimokuwa viongozi wa Pamba na kuvunja vioo na milango
Kwa uhalifu huu ulitaka hao makomando wa Simba wawauwe hao viongozi wa Pamba ndo muanze kumlaumu Mkuu wa mkoa
 
mpira wa tz ushaingia siasa tff mpo tu!
 
Mazoezi ya Simba Yana u special Gani hadi yazuie viongozi wa serikali kutimiza majukumu Yao ya kikatiba
Umeambiwa kuwa makomando wa Simba walikuwa wanavunja vioo na milango kushambulia viongozi wa Pamba.

We ulitaka watu wafe muanze kulaumu uongozi wa mkoa?
Bado hujajibu hoja ipasavyo. Umesikikiza upande wa pili? Mbona unang'ang'ana tu na maelezo ya upande mmoja?
 
Hakika kwa mbali naona makada wa chama na wakuu wa wilaya na mkoa w mwanza.wa fisiem TU.
 

Attachments

  • FB_IMG_1732272315669.jpg
    FB_IMG_1732272315669.jpg
    30.8 KB · Views: 5
Kufuatia sakata lililotokea Mwanza, na Uongozi wa klabu ya Simba kutoa taarifa ya kulaani vikali vitendo visivyo vya kiungwana vilivyodaiwa kufanywa na viongozi wa timu ya Pamba Jiji FC kwa kushirikiana na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Said Mtanda, pamoja na maafisa wa polisi.

Soma, Pia:

+
Vurugu kali zimezuka Uwanja wa CCM Kirumba wakati Simba SC ikifanya mazoezi kuelekea mechi na Pamba Jiji hapo kesho
+ Simba yalaani matumizi ya Polisi kuwazuia kufanya mazoezi katika uwanja wa CCM Kirumba kuelekea mchezo wa dhidi ya Pamba

Kupitia Crown FM, Said Mtanda, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza amesema:

"Mimi ninaamini mpira utachezwa leo, na mkuu wa mkoa akitembelea sehemu ya mkoa wake iwe uwanjani au amekwenda hospitali haina maana kwamba ameenda kuwahujumu wagonjwa au wachezaji"

"Mimi nikiwa ofisini kwangu jana nilipata taarifa kuna dalili za uvunjifu wa amani, baadhi ya makomandoo wa Simba Sc wamewahold viongozi wa Pamba Jiji Fc ambao walikuwa uwanjani wakifanya mazoezi kabla ya kuondoka, sasa wamefunga milango yote, wale vijana walipoona watashambuliwa wakaenda juu VIP wakafunga milango...."

"Makomandoo wa Simba sc wakaanza kuvunja vioo vya VIP ya CCM Kirumba, lakini baadae wakaanza kuvunja milango, kwa hiyo wakanipigia mimi, nikampigia Mkurugenzi wa jiji, lakini nikawapigia jeshi la polisi, na nikafikiri ni busara kusogea eneo hilo ili baadae mambo yasije kutangazwa ambayo sio sahihi.... lakini pia kuhakikisha jeshi la polisi linafanya kazi yake kwa weledi"

"Sikuingia uwanjani na wala sikuwa na nia ya kuona mazoezi ya Simba Sc, kwa sababu mimi ndio mgeni rasmi, nina haraka gani ya kuwaona Simba Sc wakati leo nilikuwa na uwezo wa kuiona Simba Sc kwa utulivu kwa dakika 90?"
Kweli makonda ni mkuu wa mkoa Bora kabisa sio kama wajinga kama Hawa kina mtanda
 
Tehetehe, Simba ameacha majeruhi wa kimichezo na kisiasa
 
Mtanda alitumwa na GSM abalansi point za ligi
 
Back
Top Bottom