Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Said Mtanda huwa anatembelea Wilaya za Mkoa wake?

chiembe

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2015
Posts
16,859
Reaction score
28,112
Mkoa wa Mwanza ni Mkoa wa Kimkakati, ila naona kama Mtanda "anaupoza" sana, anafanya ukuu wa mkoa wa kimangimeza, nilitarajia awe anakula "Misele" Ukerewe, Kwimba, Misungwi, Magu, nilimuona mara moja tu Sengerema akisema yule mama aliyedhulumiwa ardhi na Halmashauri wakaweka makaburi sijui viwanda aangaliwe.

Simuoni Kiseke, Igoma, Fela,Nyakato, Kirumba, Pansiansi, Buswelu, chocho za Mwanza.

Ni mkoa ambao anatakiwa auchachushe ili uwe senta ya operation ya siasa za 2025, siasa za Mwanza, zinaamua siasa za Kanda ya Ziwa kwa kiasi kikubwa. Ni sawa na timu ya mpira 'ife' sehemu ya kiungo. Wabunge ni kama wanajipambania tu, kamisaa wa mkoa hana msaada yule mama katepeta, bora yule Mabula wa Nyamagana ana nguvu kisiasa.

Hana mkakati wa kimaendeleo na kisiasa katika mkoa?

N.B: nimepitia instagram page ya mkoa kabla ya kupost, kwa mimi inatosha kumpima
 
Cheo cha mkuu wa mkoa ni useless,vyeo vya waingereza
 
Makonda anawaonyesha jinsi mkuu wa mkoa anavyo takiwa kuwa lakini bado wamelala, hawajui maana ya kumsaidia rais.
 
Acha kukuza mambo ilo swala sijuwi la mwz kuwa mwamuzi wa siasa ni kwa utafiti upi? Au umeshiba ujii ukaamua kutaka kiongozi azungunge kama utakavyo wewe?
 
Wakuu wengi wa mikoa wapo kula bata...sana sana wanategemea Kamati za Usalama.
 
Acha kukuza mambo ilo swala sijuwi la mwz kuwa mwamuzi wa siasa ni kwa utafiti upi? Au umeshiba ujii ukaamua kutaka kiongozi azungunge kama utakavyo wewe?
Umevimbiwa togwa na vimoro?
 
Makonda anawaonyesha jinsi mkuu wa mkoa anavyo takiwa kuwa lakini bado wamelala, hawajui maana ya kumsaidia rais.
Makonda na Kenani Kihongos ni mifano kwa Rc wa Tanzania...kwa upande wa maDc Kuna yule Petro Magoti wa Kisarawe
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…