Pre GE2025 Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga: Wanasiasa msiandae futari zenye asili ya rushwa kwa ajili ya Uchaguzi

Pre GE2025 Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga: Wanasiasa msiandae futari zenye asili ya rushwa kwa ajili ya Uchaguzi

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Mindyou

JF-Expert Member
Joined
Sep 2, 2024
Posts
1,869
Reaction score
4,877
Wakuu,

Wakati taifa linaeleka kenye Uchaguzi, Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Anamringi Macha amewaomba wanasiasa wasitumie fursa ya kuwafuturisha wananchi kama rushwa ya kwenye uchaguzi

Soma pia: Rais Samia awafuturisha watoto yatima, wenye mahitaji maalumu Ikulu

"Niwaombe sana viongozi wa kisiasa wasitumie visivyo mwezi huu. Tunajua kuna kuandaa futari kwa waumini wa dini zetu zote hususani kwa kweli lazima tukiri futari inayohusu waumini wa dini ya kiislamu ambayo mara nyingi ndio huonekana dhahiri kabisa.

Niwaombe viongozi wa kisiasa kama kweli wana imani ya kuandaa futari, waandae futari kwa ajili ya kukidhi imani za waumini wetu wawe wa kikristo wawe wa kislamu lakini ningewaomba wasiandae futari ili futari hizo wapitishe ushawishi wao wa kisiasa kwa sababu mifungo hii lengo lake sio hilo"

"Na sisi tunawaomba wasiandae futari zenye asili ya rushwa kawa ajili ya uchaguzi"

 
Huu mwaka wa uchaguzi si jambo la ajabu kumkuta mwanasiasa mashuhuri akiosha vyombo Kwa mama ntilie
 
Yeye hawapi watu chakula, wanapewa na wengine analalamika, hii kama sio roho mbaya ni nini?

Huu kwa waislamu ni mwezi wa kupendana na kupeana na kuhurumiana na kusaidiana, nadhani asiingilie masuala ya dini au ataharibikiwa
 
Back
Top Bottom