Mindyou
JF-Expert Member
- Sep 2, 2024
- 1,869
- 4,877
Wakuu,
Jeshi la Polisi Mkoa wa Songwe limepiga marufuku wananchi kulipua vilipuzi (fataki) bila kuwa na kibali cha Jeshi la Polisi katika Sikukuu Za Krismasi na Mwaka Mpya.
Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Songwe Kamshina Mwandamizi Msaidizi wa Polisi Augustino Senga amesema Jeshi la Polisi limejikita katika kuhakikisha ulinzi na usalama unakuwepo muda wote na maeneo katika Mkoa wa Songwe hasa kipindi hili cha sherehe za Mwisho wa Mwaka.
Aidha Kamanda Senga amewataka watumiaji wa vyombo vya moto Nà watumiaji wa barabara kuhakikisha wanazingatia Sheria na taratibu za barabarani ili kuepusha ajali na madhara mengine barabarani.
Source: Wasafi FM
Jeshi la Polisi Mkoa wa Songwe limepiga marufuku wananchi kulipua vilipuzi (fataki) bila kuwa na kibali cha Jeshi la Polisi katika Sikukuu Za Krismasi na Mwaka Mpya.
Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Songwe Kamshina Mwandamizi Msaidizi wa Polisi Augustino Senga amesema Jeshi la Polisi limejikita katika kuhakikisha ulinzi na usalama unakuwepo muda wote na maeneo katika Mkoa wa Songwe hasa kipindi hili cha sherehe za Mwisho wa Mwaka.
Aidha Kamanda Senga amewataka watumiaji wa vyombo vya moto Nà watumiaji wa barabara kuhakikisha wanazingatia Sheria na taratibu za barabarani ili kuepusha ajali na madhara mengine barabarani.
Source: Wasafi FM