Mkuu wa shule mpya Dunda sekondari Bagamoyo una kazi kubwa ya kurekebisha nidhamu ya wanafunzi.

Mkuu wa shule mpya Dunda sekondari Bagamoyo una kazi kubwa ya kurekebisha nidhamu ya wanafunzi.

mbeyaman

Member
Joined
Sep 28, 2013
Posts
97
Reaction score
28
Kwanza nichukue fursa hii kukupongeza kwa kuteuliwa kuwa mkuu wa shule wa shule ya sekondari Dunda iliyopo mjini Bagamoyo.Ila changamoto kubwa uliyonayo mbeleni katika uongozi wa shule ya sekondari Dunda ni utovu wa nidhamu wa hali ya juu wa wanafunzi.Utoro sugu ni mojawapo ya utovu wa nidhamu wa wanafunzi wa hiyo shule.Ajabu kuna baadhi ya wanafunzi wa kike wanadiriki kuishi na wanaume huku wakikacha shule,baadhi yao wamekuwa wanafanya biashara ya kuuza miili katika Night Club iitwayo Rusona iliyopo Millenium Hotel,cha kustaajabisha hivi huyu mkurugenzi wa Bagamoyo mh.Samwel Sakanga anafanya kazi gani?

Serikali iko wapi?sheria gani inaruhusu wanafunzi kuingia katika Night Club wakivaa nusu uchi wakiuza miili yao?Utafiti wangu umeonesha wanafunzi hawa wanatoka shule mbalimbali za sekondari za Bagamoyo,ila wengi wao wa Dunda.Mkuu mpya kuna baadhi ya wanafunzi wa kiume wamekuwa wanajishughulisha na kazi ya kuendesha bodaboda baada ya kwenda shule,kuna huyu mwanafunzi anaitwa Clay Matumbo wa kidato cha tatu amekacha shule anaendesha bodaboda.Hivi DEO anafanya kazi gani?Mkuu wa Trafiki wa Wilaya ya Bagamoyo anafanya kazi gani?Wanafunzi wengi hawaendi shule wanaendesha bodaboda,hasa wa shule ya sekondari Dunda je serikali imelala?...au mpaka mh.Rais aingilie kati?.

Mkuu mpya wa Dunda sekondari ndugu Deodata Mkwera umejipanga vipi kukabiliana na changamoto ya utovu wa nidhamu wa wanafunzi?...Usikamie walimu wasiowajibika wakati kutowajibika kwao kunachangiwa na nidhamu mbovu na iliyooza ya baadhi ya wanafunzi wa Dunda sekondari. Kwani nidhamu mbovu ya wanafunzi wa Dunda kumechangia kwa kiasi kikubwa kwa walimu kupunguza molari ya kazi.
 
Taja na jamii Kama wazazi na walezi je wao wanafanya nini katika kuhakikisha watoto wanasoma pia ujue kupotea kwa thamani ya elim yetu na kuongezeka kwa fursa Kama Boda na biashara nyingine kumeshusha kiwango na morali ya wanafunzi kusoma kwa ujumla kuinua elim yetu Sio swala la mwalm mkuu tu ni swala kubwa na Pana sna.
 
dah! kazi tunayo aisee wengne ndo yunajianda kuripoti ndani ya hiyo wilaya ila watanzania tushirikiane kwa pamoja kuanzia ngazi zote turudishe ile dhana ya mtoto ni mali ya jamii na kla ngaz iwajibike ipasavyo kama vile familia,walimu mashuleni na viongoz wote wa dini na serikali mbali na hivi jamii itaendelea itapotea
 
Back
Top Bottom