3 Angels message
JF-Expert Member
- Aug 3, 2017
- 5,350
- 15,426
Kutokana na athari za mvua zile za mwanzo za mwezi Desemba mwaka jana daraja lililopo eneo la Mwanzo Kata ya kifuru-Kinyerezi lilikatika na kuharibiwa vibaya na hivyo kuleta changamoto kubwa kwa wakazi wa maeneo hayo.
Mkuu wa wilaya ya Ilala alifika kwenye Desemba 17 kujionea athari na kuahidi kuwaleta Tarura waje kutathmini na kujenga daraja la kudumu lakini mpaka leo zaidi ya mwezi hatuoni utimiaji wa ahadi hiyo huku wananchi wakiendelea kuathirika.
Kwa kuona uchelewaji huo waliamua kujenga kivuko cha muda ili kurahisisha angalau uvukaji wa watu ili shughuli za maendeleo zisikwame ila nalo siyo imara sana na lina hatari nyingi hasa kwa watoto.
Tunakukumbusha Mkuu wa Wilaya Ilala ahadi yako itimie ili kuepusha madhara yanayoweza kutokea hasa kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha lakini pia shughuli za maendeleo ziendelee bila kikwazo.
Mkuu wa wilaya ya Ilala alifika kwenye Desemba 17 kujionea athari na kuahidi kuwaleta Tarura waje kutathmini na kujenga daraja la kudumu lakini mpaka leo zaidi ya mwezi hatuoni utimiaji wa ahadi hiyo huku wananchi wakiendelea kuathirika.
Kwa kuona uchelewaji huo waliamua kujenga kivuko cha muda ili kurahisisha angalau uvukaji wa watu ili shughuli za maendeleo zisikwame ila nalo siyo imara sana na lina hatari nyingi hasa kwa watoto.
Tunakukumbusha Mkuu wa Wilaya Ilala ahadi yako itimie ili kuepusha madhara yanayoweza kutokea hasa kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha lakini pia shughuli za maendeleo ziendelee bila kikwazo.