Mkuu wa Wilaya kutoa amri ya kumkamata Hakimu, sheria ipi inayompa mamlaka

Mkuu wa Wilaya kutoa amri ya kumkamata Hakimu, sheria ipi inayompa mamlaka

ahamwiga

Member
Joined
Jul 22, 2013
Posts
6
Reaction score
0
Ninavyo jua mimi Nchi hii inaongozwa kwa Sheria,Kanuni, na Taratibu, nimesikia katika vyombo vya habari kuwa Mkuu wa Wilaya alitoa Amri ya kukatwa kwa Hakimu wa Mahakama ya Mwanzo kwa madai kuwa alitumia vibaya kalamu yake kutoa maamuzi yaliyo sababisha shamba la mkulima mmoja kuuzwa, Ninajua kuwa Mkuu wa Wilaya husika ndiye Mwenyekiti wa Bodi ya Mahakama ya kushughulikia maswala ya nidhamu kwa Mahakimu wa Mahakama ya Mwanzo. Ina maana Mkuu wa Wilaya huyo hajui kuwa Sheria hiyo ipo na hajui wajibu wake mpaka atoe Amri hiyo ya kumkamata hakimu huyo, au Sheria hiyo imefutwa? na kama haijafutwa yeye amefuata sheria au ametumia mdaraka yake vibaya kwa kujipendekeza ili hapo baadaye ateuliwe tena kuwa Mkuu wa Wilaya.

Ninafikiri kuwa Kauli mbiu ya "Hapa Kazi" haina maana ya kukiuka taratibu,kanuni na Sheria zilizo wekwa. Ninaomba kujua ni hatua zipi ambazo zinaweza kuchukuliwa dhidi ya watu kama ambao wanaoona makosa ya watu wengine wakati nao wakikiuka taratibu na sheria za nchi.
 
Hawa watu wanaojiita wakuu wa wilaya sijui wanafikiri kwa kutumia nini
 
Amuulize Mhe. Mrisho Gambo kilichompata akiwa Korogwe ajue kuwa kuna maadili ya utumishi wa umma na sio kumuweka mtumishi ndani. Watu wa Korogwe wanajua.
 
Amuulize Mhe. Mrisho Gambo kilichompata akiwa Korogwe ajue kuwa kuna maadili ya utumishi wa umma na sio kumuweka mtumishi ndani. Watu wa Korogwe wanajua.

Tuambie basi sisi hicho kitu nasi tukijue maana sisi siyo watu wa korogwe!
 
Mkuu wa wilaya hana mamlaka ya kumwajibisha hakimu bali anachoweza kufanya ni kumwomba Hakimu mkaazi umwajıbishe kwa niaba ya CJ.
 
Nnavojua mtumishi wa umma ana utaratibu wake maalum wa kuwajibishwa kinidhamu na sio matamko na amri
 
sijawahi sikia hichi kitu, mleta mada embu kuwa specific, mahakama ni muhimili tofauti kabisa na administators, na sina uhakika kama unachokisema ni kweli
 
Back
Top Bottom