Mindyou
JF-Expert Member
- Sep 2, 2024
- 1,869
- 4,877
Wakuu,
Kumbe viongozi wa CCM upande wa serikali za mitaa walikuwa wanauza kiholela viwanja vya wananchi na mlikuwa hamsemi?
Naona CCM sasa wameanza kujiumbua wenyewe hadharani kwa kusema mambo ya hovyo ambayo walikuwa wanayafanya kipindi wako kwenye uongozi.
===========================
Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Jabir Shekimweri, ametoa rai kwa viongozi wa serikali za mitaa kuzingatia weledi katika utendaji wao, kuepuka vitendo vya rushwa, na kujiepusha na uuzaji wa viwanja vya wananchi kwa njia isiyostahili.
Aidha, alibainisha kuwa serikali imepanga kutoa mafunzo maalum kwa viongozi hao ili kuboresha ufanisi wao kazini.
Mhe. Shekimweri alitoa tamko hilo JANA, Desemba 4, 2024, katika viwanja vya Shule ya Msingi Dodoma Makulu, jijini Dodoma, wakati akizindua kampeni ya "Nipendezeshe Nisome," ambayo inalenga kusaidia wanafunzi wenye mahitaji maalum kwa kuwapatia sare za shule.
Source: Jambo TV
Kumbe viongozi wa CCM upande wa serikali za mitaa walikuwa wanauza kiholela viwanja vya wananchi na mlikuwa hamsemi?
Naona CCM sasa wameanza kujiumbua wenyewe hadharani kwa kusema mambo ya hovyo ambayo walikuwa wanayafanya kipindi wako kwenye uongozi.
===========================
Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Jabir Shekimweri, ametoa rai kwa viongozi wa serikali za mitaa kuzingatia weledi katika utendaji wao, kuepuka vitendo vya rushwa, na kujiepusha na uuzaji wa viwanja vya wananchi kwa njia isiyostahili.
Aidha, alibainisha kuwa serikali imepanga kutoa mafunzo maalum kwa viongozi hao ili kuboresha ufanisi wao kazini.
Mhe. Shekimweri alitoa tamko hilo JANA, Desemba 4, 2024, katika viwanja vya Shule ya Msingi Dodoma Makulu, jijini Dodoma, wakati akizindua kampeni ya "Nipendezeshe Nisome," ambayo inalenga kusaidia wanafunzi wenye mahitaji maalum kwa kuwapatia sare za shule.
Source: Jambo TV