JanguKamaJangu
JF-Expert Member
- Feb 7, 2022
- 2,780
- 6,607
Wilaya ya Kinondoni imeanzisha utaratibu wa kuweka Matron katika gari za kubeba wanafunzi, kutokana na kuibuka kwa vitendo vya ubakaji kwa watoto vinavyodaiwa kufanywa na madereva.
Mkuu wa Wilaya hiyo, Godwin Gondwe amesema amepokea malalamiko mengi kutoka kwa wazazi na walezi, wakidai watoto wao kufanyiwa vitendo vya ubakaji katika magari ya shule.
Akizungumza leo Septemba 6, 2022, Dar es Salaam katika Mkutano wa Maofisa Ustawi wa Jamii nchini, Gondwe aliwataka wazazi na walezi kuwa makini kufuatilia taarifa za watoto na kujenga ukaribu, ili wanapokumbana na changamoto waseme haraka.
“School Bus mtoto anapanda wa kwanza anashuka wa mwisho na bahati mbaya wazazi hawafuatilii watoto, hivi karibuni kuna mama alikuja kulalamika mwanaye alifanyiwa ukatili. Dereva alipaki gari akaenda kumfanyia mtoto shambulio la kikatili na mtoto alivyofika nyumbani alikuwa huru kuzungumza na mama,” ameeleza.
Chanzo: Habari Leo
===
Hukumu kwa watuhumiwa soma: Wafungwa maisha kwa ukatili wa mtoto kwenye school bus
Mkuu wa Wilaya hiyo, Godwin Gondwe amesema amepokea malalamiko mengi kutoka kwa wazazi na walezi, wakidai watoto wao kufanyiwa vitendo vya ubakaji katika magari ya shule.
Akizungumza leo Septemba 6, 2022, Dar es Salaam katika Mkutano wa Maofisa Ustawi wa Jamii nchini, Gondwe aliwataka wazazi na walezi kuwa makini kufuatilia taarifa za watoto na kujenga ukaribu, ili wanapokumbana na changamoto waseme haraka.
“School Bus mtoto anapanda wa kwanza anashuka wa mwisho na bahati mbaya wazazi hawafuatilii watoto, hivi karibuni kuna mama alikuja kulalamika mwanaye alifanyiwa ukatili. Dereva alipaki gari akaenda kumfanyia mtoto shambulio la kikatili na mtoto alivyofika nyumbani alikuwa huru kuzungumza na mama,” ameeleza.
Chanzo: Habari Leo
===
Hukumu kwa watuhumiwa soma: Wafungwa maisha kwa ukatili wa mtoto kwenye school bus