monjozee
Senior Member
- Sep 19, 2016
- 115
- 297
Taarifa za kiintelijensia (siyo ya polisi) zilizinifikia usiku huu ni kwamba Mkuu wa wilaya ya Tarime Glorious Luoga ameandaa kikundi cha wanaccm toka Tarime Mjini wanaojulikana kwa jina la Naybigena Cooperative ili kuandamana kesho huko Nyamongo kwa lengo la kujikomba kwa rais JPM. Hadi usiku huu DC Luoga bado yupo Nyamongo katika bar moja inayoitwa Wansa akiandaa risala ambayo atasomewa hapo kesho na waandamanaji aliowaandaa mwenyewe.
Maandamano hayo ya wanaccm ambayo wanatarajia kuyafanya hapo kesho katika eneo la *Nyamongo* ulipo mgodi wa dhahabu wa North Mara unaomilikiwa na kampuni ya Acacia yana lengo la kumpongeza Mwenyekiti wa ccm, rais JPM kwa kile Luoga anachodai kuwa ni hatua muhimu za kulinda rasilimali za madini.
Wananchi wanaoishi Nyamongo ambao wamekuwa wakikumbana na madhila ya mgodi wa North Mara wamekataa kushiriki maandamano hayo ya kipuuzi yenye lengo la kumjrnga kisiasa Mkuu wa wilaya mpenda kick.
Wananchi wa Nyamongo na Tarime kwa ujumla hatukubaliani na upuuzi unaopangwa kufanywa na Mkuu wa wilaya hapo kesho kwakuwa bado tuna malalamiko na madai ya msingi ambayo kwa muda mrefu serikali imeshindwa kuyapatia majibu.
Ukiacha hicho kikundi cha kihuni cha ccm, watu wa Tarime hawawezi kumpongeza rais kwasababu wana madai mengi ambayo hayajawahi kupatiwa ufumbuzi ambayo ni pamoja na;
1. Mauaji ya wananchi yanayofanywa na polisi yaliyothibitishwa na kamati iliyoundwa na prof Muhongo wameuwawa watu zaidi ya mia 100 na hawajalipwa fidia.
2. Malipo ya fidia ya ardhi maeneo ya Nyabichune, Mjini kati, Matongo, Murwambe na Nyamichele zaidi ya billion 22 hatujalipwa.
3. Maji hayapo kutokana na vyanzo vyetu kuchafuliwa na sumu ya mgodi na mpaka sasa mgodi haujawahi kutupatia maji safi hivyo kusababisha magonjwa na mifugo kufa mfano Mto Tigite
4. Vumbi la mgodi mawe ya baruti milio ya kutisha. Barabara mbovu. Sisi hatuwezi kuandamana kupongeza chochote kwasababu hakuna hata jambo moja kati ya hayo limejibiwa na makinikia ya rais hasa ukizingatia tulipojaribu kuingia mgodini baada ya rais kusema ni wezi tulikamatwa na wenzetu mpaka sasa wako ndani. Dc acha kutafuta umaarufu wa kijinga.
MASWALI YA MSINGI
1. Je, kwanini maandamano haya yanaandaliwa kwa siri? tena mkuu wa wilaya akiwa baani?
2. Hivi nchi hii serikali si imepiga marufuku mikutano ya hadhara na maandamano? DC Luoga yeye anatoa wapi kibali cha kuyafanya haya ?
3. Je, ni nani anatoa gharama za kusafirisha watu kutoka Tarime mjini kwenda Nyamongo? Na ni kwa manufaa ya nani?
4. Kwanini wananchi walazimishwe kushiriki kwenye maandamano ambayo hawayataki,kwa kuwa kero na vilio vyao vya siku zote mgodini hapo havijatatuliwa?
Serikali hii kwanini inaendesha nchi kwa double standards kwa kiwango hiki?
Maandamano hayo ya wanaccm ambayo wanatarajia kuyafanya hapo kesho katika eneo la *Nyamongo* ulipo mgodi wa dhahabu wa North Mara unaomilikiwa na kampuni ya Acacia yana lengo la kumpongeza Mwenyekiti wa ccm, rais JPM kwa kile Luoga anachodai kuwa ni hatua muhimu za kulinda rasilimali za madini.
Wananchi wanaoishi Nyamongo ambao wamekuwa wakikumbana na madhila ya mgodi wa North Mara wamekataa kushiriki maandamano hayo ya kipuuzi yenye lengo la kumjrnga kisiasa Mkuu wa wilaya mpenda kick.
Wananchi wa Nyamongo na Tarime kwa ujumla hatukubaliani na upuuzi unaopangwa kufanywa na Mkuu wa wilaya hapo kesho kwakuwa bado tuna malalamiko na madai ya msingi ambayo kwa muda mrefu serikali imeshindwa kuyapatia majibu.
Ukiacha hicho kikundi cha kihuni cha ccm, watu wa Tarime hawawezi kumpongeza rais kwasababu wana madai mengi ambayo hayajawahi kupatiwa ufumbuzi ambayo ni pamoja na;
1. Mauaji ya wananchi yanayofanywa na polisi yaliyothibitishwa na kamati iliyoundwa na prof Muhongo wameuwawa watu zaidi ya mia 100 na hawajalipwa fidia.
2. Malipo ya fidia ya ardhi maeneo ya Nyabichune, Mjini kati, Matongo, Murwambe na Nyamichele zaidi ya billion 22 hatujalipwa.
3. Maji hayapo kutokana na vyanzo vyetu kuchafuliwa na sumu ya mgodi na mpaka sasa mgodi haujawahi kutupatia maji safi hivyo kusababisha magonjwa na mifugo kufa mfano Mto Tigite
4. Vumbi la mgodi mawe ya baruti milio ya kutisha. Barabara mbovu. Sisi hatuwezi kuandamana kupongeza chochote kwasababu hakuna hata jambo moja kati ya hayo limejibiwa na makinikia ya rais hasa ukizingatia tulipojaribu kuingia mgodini baada ya rais kusema ni wezi tulikamatwa na wenzetu mpaka sasa wako ndani. Dc acha kutafuta umaarufu wa kijinga.
MASWALI YA MSINGI
1. Je, kwanini maandamano haya yanaandaliwa kwa siri? tena mkuu wa wilaya akiwa baani?
2. Hivi nchi hii serikali si imepiga marufuku mikutano ya hadhara na maandamano? DC Luoga yeye anatoa wapi kibali cha kuyafanya haya ?
3. Je, ni nani anatoa gharama za kusafirisha watu kutoka Tarime mjini kwenda Nyamongo? Na ni kwa manufaa ya nani?
4. Kwanini wananchi walazimishwe kushiriki kwenye maandamano ambayo hawayataki,kwa kuwa kero na vilio vyao vya siku zote mgodini hapo havijatatuliwa?
Serikali hii kwanini inaendesha nchi kwa double standards kwa kiwango hiki?