Mkwara mzito.

Kirikou Wa Kwanza

JF-Expert Member
Joined
May 24, 2013
Posts
3,564
Reaction score
1,991
Kawa kawaida ndani ya daladala Mbagala, wakati konda akiendelea na zoezi la kuchukua pesa kwa abiria. Kuna kijana akamuibia nauli
mzee mmoja aliyekuwa kasimama kwenye siti za nyuma.

Konda alipomfikia mzee na kumuomba nauli, mzee alipoangalia nauli katika mifuko yake hakuiona. Mzee akatangaza, "Jamani alieniibia nauli
yangu anirudishie kabla sijafanya
nilichokifanya mwaka 1970...Narudia mara ya mwisho aliyeniibia nauli yangu anirudishie kabla sijafanya nilichokifanya mwaka 1970." Kijana aliyeiba nauli ya mzee huku
akitetemeka akasema, "Mzee nauli yako hii hapa halafu akauliza kwani ulifanya nini 1970?" Mzee akajibu, "Nilitembea kwa miguu kutoka
Mbagala mpaka posta."

Tehe tehe tehe abiria wote ndani ya daladala wakaangua kicheko!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…